Walimu karibu wote uwezo mdogo

Walimu karibu wote uwezo mdogo

TEACOLTD Kwanza hongera kwa kuwa na ujasiri wa kuleta uzi huu maana sio viongozi wanaoongoza/simamia sekta ya elimu wala serikali kuu ilishawahi kukiri kuwa tuna tatizo la walimu wenye uweledi na kuwa na mkakati makhsusi wa kulitatua tatizo hilo.

Kimsingi yote uliosema ni kweli though naona Kuna simbilisi wanao comment kwa hoja zisizo na mashiko na nadhani ni kwasababu tu na wenyewe ama ndugu zao wamenufaika na huo mfumo ambao umetufikisha hapa kitaaluma.

Pili ualimu kama ilivyo kazi nyingine kama upolisi, jeshi hazichukuliwi serious na ndio imepelekea watu kuona hizi ni kazi za watu waliofeli, au kupata ufaulu duni hizi ndio kimbilio lao (kwa walimu wadau wameonyesha ufaulu na wako wanasoma wapi) Tatizo hili linaanzia primary huko ni zaidi ya time bomb watoto wanamaliza darasa la saba hawajui kusoma na kuandika but education system haijali, serikali ina focus kwenye enrolments, utawasikia tumevuka lengo la kuandikisha kwa 85% but does it make sense anyway! If at all these students finish std 7 and can't read and write! In 7yrs neither teachers themselves nor wasimamizi wa elimu has clue on what is going on! Halafu eti baada ya matokeo ya mitihani unakuja kutuambia watoto wameandika kat uni! !!!!!!

Hawa walimu wa shule za msingi hawawezi hata kufaulu ule mitihani wa darasa la saba kama ukiwapa wafanye sasa wanamfundisha nani? Hivyo Hivyo secondary wachukue walimu wa O-level wafanye mitihani wa kidato cha pili uone matokeo yake .

Elimu ni sekta ambayo inaelekea kuzimu TZ na si kwa bahati mbaya lakini ni matokeo ya makusudi ya serikali. Huwezi kuwa na serikali dhalimu iliyokosa hata haya , kama mtakumbuka awamu ya 4 pale watoto 60% walipofeli baada ya ku-acknowledge tatizo na kutafuta ufumbuzi serikali hatua iliyochukua ni ku-standardise matokeo ili tu kuwafool watanzania. Na IJULIKANE ni hao hao failures ndio waliobadilishiwa ufaulu na hatimae kuendelea na masoma na Leo/kesho ndio walimu so obvious mjinga atamfundisha mjinga mwenzake and we all know what will be the outcome!.

Leo mijadala mingi inajadili uwezo wa graduates wa Kitanzania(not only teachers) Kwamba hawana uwezo hata wa kujieleza wachilia mbali uwezo wa ku-deliver katika shughuli zao, the reasons ni kwamba Hawa si wengine ila ni matokeo ya huu huu uozo ambao for years umekua ukiendelea.

Ikumbukwe every child/person has the capacity to learn be it quicker or slow leaner it doesn't matter but it's upon the teacher to be able to;
1. Understand what he/she is supposed to teach (be conversant on the subject matter)
2. Be able to navigate that the class understand what he/she is teaching (teach-measure and evaluate)
3. Be warm, accessible enthusiastic and caring as it will open the desire for the students to ask where they don't understand
4. Set high expectations for all students
5. Inspire the students with his/her passion for education and for the course materials and constantly renews herself/himself as a professional on his/her quest in provide students with the highest quality education possible
6. Be able to "shift gear" -flexibility when a lesson isn't working. This kind of a teacher assesses his/her teaching throughout the lessons and finds new ways to present materials to make sure that every student understands the key concepts.

Mwisho serikali kupitia wizara husika andaeni walimu wenye sifa na sio utaratibu wa sasa wa mikakati zima moto. Let's be serious and select well qualified students for teaching career na sio failures ndo wanao kwenda ualimu na baadae kuja kufundisha watoto kwa level zote
Mkuu kada gani inachukua ufaulu mkubwa kuliko zote tuanzie ngazi ya cheti kwanza
 
walimu ka kaizirege wote wana one?

je wote wamesoma udsm?

wote wametoka familia bora?
 
  • Thanks
Reactions: cpt
Unajua kigezo cha ufaulu gani Kinahitajika kwa mtu kusomea degree ya ualimu chuo kikuu kama udsm ?? Ngoja nikusaidie usipende kukalili maisha hiyo fact yak ya kwanza haiko sawa mfano mzuri kwa udsm ili usomee ualim lazima uwe na division 1 ya point yoyote ile ,,, sasa unapokalili na kusema kusomea ualimu ni kwa waliofeli tengua kauli mkuu think critically
ndugu mwalimu nakushukuru rasmi kwa kuthibitisha hoja ya mtoa mada!
 
Hawawezi kukiri na watatukana sana, lakini upo sahihi sana. Asilimia kubwa ya walimu wa zama hizi ni VILAZA na hawana wito. Hatuotei, tunao mitaani huku ni ndugu, jamaa na marafiki zetu.
Sometime ukikaa unasikia "fulani" naye kawa mwalimu hadi unashtuka. Inasikitisha. Wengi wanabebwa na hizi ajira za mafungu zisizo na interview.
 
bora tuliopiga education na tuna hella zetu za kutosha...ajira full..full
 
  • Thanks
Reactions: cpt
Mkuu tuanzie ngazi ya cheti..ni kada gani inayochukua ufaulu mkubwa kuliko zote
Mkuu swali lako naweza kulijibu lakini nikawa siko realistic sana.
Mathalani katika kuhitimu kwangu kidato cha iv tuliofaulu kuanzia daraja laI-III wengi tuliendelea na kidato cha V na baadhi technical colleges km DIT,ATC,MTC etc kwa kipindi hicho.
Kwahiyo watu wote waliofaulu chini ya hapo wengi wao walienda ualimu(mpaka IV ya 28) kipindi hicho na wengine pengine walisomea kada mbalimbali kulingana na vigezo vya udahili kwa mujibu wa NACTE.
Sasa kwa muktadha huo, itoshe tu kusema kwamba wenye ufaulu hafifu ndo hao walienda kusomea ualimu na hatmae kuwa walimu.
Vivyo hivyo hata kwa wahitimu wa kidato cha VI.
Bila shaka umenielewa mkuu.
 
Nimeweka hapo awali ukifundishwa kupika haimainishi aliyekufundisha ataendelea kuwa zaidi yako, juhudi zako ndizo humfanya mtu ampite...mwalimu aliyenifundisha uwezo wake ndio uliishia pale ila kwa juhudi zangu nikampita...kwahiyo kama alimaliza form four akapiga four akapelekwa ualimu kisha akaja kufundisha shule ya msingi, mie mwanafunzi wake nikasonga mpaka chuo kikuu bado utasema mwalimu ni bright?! Asilimia kubwa ya waalimu uwezo upstairs ni mdogo
Na kingine mie sikusoma ualimu Bali nilisoma PSPA (Political Science and Public Administration)
Bonge la logic
 
Nakubaliana na wewe 100%.Nisiloelewa ni kwa nini mambo yafanywe hivi,huku tukijua kwamba mwalimu wa hivyo ataleta kihiyo.Nadhani kuna conspiracy hapo.Kwa nini tusiwalipe vizuri vijana intelligent wakapenda ualimu ili hatimaye watuletee product nzuri.Again an obvious conspiracy.
Habari wanajamvi?

Ashakum sio matusi ila leo nimeamua kuleta mada hii baada ya kufanyia utafiti binafsi kwa muda hivi.Kwanza nilianza kuambiwa na rafiki yangu enzi hizo 2012 pale UDBS kwamba asilimia kubwa kama sio wote waalimu uwezo wao ni mdogo upstairs nikakataa akanitaka nifanye utafiti binafsi.

- Walimu wengi kama sio wote hawakupenda kuwa waalimu ila ufaulu wao ndio ulipelekea wakose option na kujikuta kwa shingo upande wanadumbukia kwenye fani ya ualimu bila kupenda.

-Asilimia kubwa ya walimu hawakupenda kwenda ualimu ila ukiachilia mbali ufaulu kuwa hafifu pia urahisi wa kuajiriwa, hii inatokana na ajira kuwa ngumu hivyo wengi kukimbilia ualimu ili kutatua matatizo yao ya ajira.

-Uchumi mbovu umepelekea wengi kuishia kuwa waalimu, hapa nina maana zile familia ambazo hazina uwezo wa kumlipia mwanafunzi kusoma kitu anachokipenda hivyo kujikuta akisoma ualimu ili apate ufadhili wa serikali.

Naomba nisieleweke vibaya ila jaribu kufuatilia kwa umakini uje unaimbie mwanafunzi aliyepata division one nzuri kabisa akawa mwalimu, asilimia kubwa ya waalimu ni waliosoma arts au biashara kwakuwa wengi matokeo yao hayakuridhisha hatimaye option pekee ikawa ualimu.

Waalimu wengi wa science walifeli hapa naomba uniletee mwalimu ambaye ama alisoma PCM, PCB, PGM n.k akapata divion one au two akaenda kusoma ualimu? Wanaokuwa waalimu wengi huangukia kwenye point ya ufaulu mbovu darasani na ni wachache sana huangukia kuwa waalimu sababu ya uchumi wa familia ila wengi saaana walifeli.

Hata kama walijiendeleza na kuwa na masters still ukirudi nyuma utakuwa wengi walifeli, ndio maana nikasema asilimia kubwa kama sio wote uwezo wao ni mdogo.
 
Kada gani hapa nchini ambayo mtu aliyepata 3 hawezi kusomea...nitajie yoyote
Inategemea na chuo pia ushindani wa nafasi hiyo katika chuo hicho.
Chuo kama st joseph candidate aliyeopt kuchukua electronics qualifications zake zipo chini sana ukilinganisha na yule aliyepata admission UDSM.
 
Unajua wapi umeshindwa kunielewa?? Hivi unaanza vipi kufananisha mtu anayesoma ualimu wa biashara na arts kwa anayesoma engineering??? Ningekuona wa maana ungeweka points za anayesoma ualimu wa science kwa engineering au ualimu wa arts kwa anayesoma arts courses au ualimu wa biashara kwa courses za biashara badala yake unanichanganyia eti bachelor of arts in education points 5 out of 3 subjects kulinganisha na bachelor of engineering points 2 out of 3 subjects...Ukiangalia unaona yana mshabihiano????
Ndo maana umesema walimu wengi ni vilaza upstairs
 
Mkuu swali lako naweza kulijibu lakini nikawa siko realistic sana.
Mathalani katika kuhitimu kwangu kidato cha iv tuliofaulu kuanzia daraja laI-III wengi tuliendelea na kidato cha V na baadhi technical colleges km DIT,ATC,MTC etc kwa kipindi hicho.
Kwahiyo watu wote waliofaulu chini ya hapo wengi wao walienda ualimu(mpaka IV ya 28) kipindi hicho na wengine pengine walisomea kada mbalimbali kulingana na vigezo vya udahili kwa mujibu wa NACTE.
Sasa kwa muktadha huo, itoshe tu kusema kwamba wenye ufaulu hafifu ndo hao walienda kusomea ualimu na hatmae kuwa walimu.
Vivyo hivyo hata kwa wahitimu wa kidato cha VI.
Bila shaka umenielewa mkuu.
Mkuu umetoa maelezo pasipo kunijibu swali..nimeuliza katika ngazi ya cheti ni kada gani inayochukua ufaulu mkubwa kuliko nyingine
 
hii ndio tanzania bana, afu tunatokwa povu escrow, epa, sijui nini!
 
Inategemea na chuo pia ushindani wa nafasi hiyo katika chuo hicho.
Chuo kama st joseph candidate aliyeopt kuchukua electronics qualifications zake zipo chini sana ukilinganisha na yule aliyepata admission UDSM.
Owk kwa maelezo yako kumbe kuna mtu aliyesoma pcb anaweza kwenda kusoma udaktari kampala university or hubert kairuki wakati ufaulu wake ni mdogo kuliko mtu aliyesoma pcb na akaenda science education university of dar es salaam...sasa hapo kati ya huyo daktari na mwalimu nani mwenye ufaulu na uwezo mdogo????
 
Mkuu umetoa maelezo pasipo kunijibu swali..nimeuliza katika ngazi ya cheti ni kada gani inayochukua ufaulu mkubwa kuliko nyingine
Unaongelea failure kwa failure mkuu...hata kama wanachukua point 27 ualimu still ni four...halafu upande wangu mwanafunzi yeyote ambaye kamaliza four akapiga four akakimbilia chuo huwa namuita Kilaza...ninaowaongelea ni wale wamemaliza form six wakaingia chuo wanaoenda ualimu upstairs ni wabovu...so tambua hao unaowaongelea wote uwezo mdogo...ni sawa na aliyemaliza form six akafeli na kupata principal moja akakimbilia diploma, so tambua point asilimia kubwa waalimu ni wabovu upstairs
 
Unaongelea failure kwa failure mkuu...hata kama wanachukua point 27 ualimu still ni four...halafu upande wangu mwanafunzi yeyote ambaye kamaliza four akapiga four akakimbilia chuo huwa namuita Kilaza...ninaowaongelea ni wale wamemaliza form six wakaingia chuo wanaoenda ualimu upstairs ni wabovu...so tambua hao unaowaongelea wote uwezo mdogo...ni sawa na aliyemaliza form six akafeli na kupata principal moja akakimbilia diploma, so tambua point asilimia kubwa waalimu ni wabovu upstairs
Kumbe kada zote kwa ngazi ya cheti ni failure sasa kwanini umemuongelea mwalimu tu hujaongelea watu wakada nyingine huoni hapo unaonyesha tu kuwa unachuki zako binafsi na kada ya ualimu
 
Habari wanajamvi?

Ashakum sio matusi ila leo nimeamua kuleta mada hii baada ya kufanyia utafiti binafsi kwa muda hivi.Kwanza nilianza kuambiwa na rafiki yangu enzi hizo 2012 pale UDBS kwamba asilimia kubwa kama sio wote waalimu uwezo wao ni mdogo upstairs nikakataa akanitaka nifanye utafiti binafsi.

- Walimu wengi kama sio wote hawakupenda kuwa waalimu ila ufaulu wao ndio ulipelekea wakose option na kujikuta kwa shingo upande wanadumbukia kwenye fani ya ualimu bila kupenda.

-Asilimia kubwa ya walimu hawakupenda kwenda ualimu ila ukiachilia mbali ufaulu kuwa hafifu pia urahisi wa kuajiriwa, hii inatokana na ajira kuwa ngumu hivyo wengi kukimbilia ualimu ili kutatua matatizo yao ya ajira.

-Uchumi mbovu umepelekea wengi kuishia kuwa waalimu, hapa nina maana zile familia ambazo hazina uwezo wa kumlipia mwanafunzi kusoma kitu anachokipenda hivyo kujikuta akisoma ualimu ili apate ufadhili wa serikali.

Naomba nisieleweke vibaya ila jaribu kufuatilia kwa umakini uje unaimbie mwanafunzi aliyepata division one nzuri kabisa akawa mwalimu, asilimia kubwa ya waalimu ni waliosoma arts au biashara kwakuwa wengi matokeo yao hayakuridhisha hatimaye option pekee ikawa ualimu.

Waalimu wengi wa science walifeli hapa naomba uniletee mwalimu ambaye ama alisoma PCM, PCB, PGM n.k akapata divion one au two akaenda kusoma ualimu? Wanaokuwa waalimu wengi huangukia kwenye point ya ufaulu mbovu darasani na ni wachache sana huangukia kuwa waalimu sababu ya uchumi wa familia ila wengi saaana walifeli.

Hata kama walijiendeleza na kuwa na masters still ukirudi nyuma utakuwa wengi walifeli, ndio maana nikasema asilimia kubwa kama sio wote uwezo wao ni mdogo.
wewe ni mwongo mimi ni mwl wa BIO/CHEM nilisoma PCB na nikapata div ii, nikasoma chuo Bsc Edu. nikiwa na teaching subjects 2, na nikasoma Msc Env sc. na napeta kwa kufundisha watoto
 
Kumbe kada zote kwa ngazi ya cheti ni failure sasa kwanini umemuongelea mwalimu tu hujaongelea watu wakada nyingine huoni hapo unaonyesha tu kuwa unachuki zako binafsi na kada ya ualimu
Kama ulinifuatilia vyema nilitoa sababu kadhaa za wengi kukimbilia ualimu...halafu pili wengi wanaomaliza kidato cha nne na kufeli wengi wabovu kichwani, tukubaliane hakuna kufeli kwa bahati mbaya au kufaulu kwa kubahatisha...hivyo basi hao wakishafeli ndio linakuja swala la familia kama lina uwezo wa kusimamia show mpaka amalize chuo kama hawawezi vilaza hawa hukimbilia udhamini wa wizara ya elimu na kupangiwa vyuo na hatimaye vilaza hawa humaliza na kusubiri kupangiwa shule kama wanavyosubiria kupangiwa wa sasa....
Hebu nijuze swala moja hivi iwapo mpo wawili mnasoma HKL halafu matokeo kutoka umefaulu na kupiga one ya tano na mwenzako akapiga three suppose ni 14 unadhani wewe utaenda kusoma education chuo?? Kama ni ndio basi linakuja swala la familia kwamba ukitaka kusoma law hutapata mkopo hivyo itakulazimu kusoma ualimu ila yule wa three hana option kwakuwa amefeli...kwahiyo tukubaliane waalimu wengi wabovu upstairs
 
Sasa hata baada ya kuandika hayo lengo kuu ni lipi?
1.chuki kwa walimu
2.hasira za kukosa ajira
3.wivu kwa kuwa walimu wanapata ajira moja kwa moja na wewe upo mtaani huna kazi?
4.kuuambia umma kwamba walimu ni ma failures na wajinga kitaaluma?
5.dharau kwa kada zingine kwa vile wewe upo kada yenye heshima na mshahara mzuri zaid kuliko ualimu? Nk
Lakini haohao wenye marks hizo hizo na failure zao ndio walio kupa kiburi cha wewe ku type hapa na kuwadharau, hakuna msomi yeyote asiye pitia mikononi kwa mwalimu hivyo unacho kifanya wewe nikutukana wazazi wako baada ya kukuzaa na kukukuza, ni sawa na kukata daraja baada ya kuvuka mto ukidhan unaukomoa mto wakati wa kurudi uta hitaji daraja tena,, nadhan hata watoto wako hawata muhitaji mwalimu utawafundisha wewe na ukisha kuwa mfundishaji na wewe pia utakuwa umesha imgia kwenye kundi la walimu hasa tukitafsiri sahihi maana ya neno "MWALIMU"

Naweza sema mimi ni mwalimu na ni failure kama ulivyo sema lakini wanafunzi walio pita mikononi mwangu wengine ni engineer wengine ma Dr. Wengine walimu kama mimi na wengine wako kwenye fani zingine mbalimbali ,na wengine wanadharau kazi hii kama wewe ufanyavyo baada ya kuvuka

lakini wametoka kwenye mikono ya failure mimi kama sema yako.
Lakini pia unatakiwa kujua kuwa ualimu ni kazi inayo hitaji watendaji , na wala sio kazi ya class fulani, niseme ufinyu wako wa mawazo ndio ulio pelekea kufikiri hivyo na kuandika ulicho andika kwa vile ulitumia upande mmoja tu katika hoja yako hiyo

Neno mwalimu nineno lenye upana sana labda ulishindwa ku categorise huo ualimu unao usema ni upi maana hata wanao hubiri injili na kufundisha mafundisho ya mwenyezi mungu pia huitwa walimu

Lakini pia kwa kusema walimu wana uwezo mdogo ni katika lipi?
Maana kwa mfumo wetu wa elimu ulivyo bado haitosh kutambua uwezo katika uhalisia wake maana elimu hii hata mtu akiiiba mtihani au akapewa majibu ya mtihani hata kama hajui kusoma wala kuandika ingawa ana A kwa upande wako huyo ndio mwenye uwezo.ref darasa la saba anaye pata A masomo yote lakin hata kusoma kwa ufasaha kwake ni tatizo.lakini ana ufahuri mzuri kwenye cheti na hii sio huko tuu ipo hata shule za sekondari hadi vyuo.

Uwezo wa kitaaluma umegawanyika katika makundi mengi sana hivyo huwezi kutumia kigezo kimojaa kutoa majibu ya uwezo mdogo au mkubwa kama mtafiti ,maana kwa hoja yako hiyo umesha utia najisi huo utafiti wako

Na kwanini labda umeiona kada ya ualimu pekee ndio imekusanya failures na sio kada zingine? Maana kuna kada zingine hadi wenye ziro wako kazini na wanalipwa mshahara na serikali na ni watendaji wazuri mno kuliko hao wenye 1,2,3 nk. Lengo lako kuu lilikuwa ni lipi hadi ukapata wazo la kuwasakama walimu kwa hoja na kinadharia zaidi kuliko uhalisia?

Lakini hongera pia kwa utafiti wako wa kihisia kuliko uhalisia.
Hivi kwa nini walimu wengi wana jishtukia sana ikisemwa fani yao kuliko fani nyingine,na wanalalamika sana mfano jeshi wengi wanaenda ambao hawakufaulu sana kuliko hata hao walimu lakini huwezi kukuta wanalalamika eti isingekua sisi kuilinda nchi na kuwa na amani wewe usingesoma na kuwa na kazi flani unakuta mtu anapiga education bachelor ukimuuliza unasoma nini anakwambia nazuga zuga na education si unajua ualimu ni daraja tu ya kupitia!!!!!huwa inanishangaza sana sijui nini kimewafanya wasijiamini hivi
 
Mkuu umetoa maelezo pasipo kunijibu swali..nimeuliza katika ngazi ya cheti ni kada gani inayochukua ufaulu mkubwa kuliko nyingine
Zipo nyingi tu mkuu. Mathalani kada ya sheria na teknologia ngazi ya cheti min. entry qualifications ni kubwa ukilinganisha na ualimu.
 
Back
Top Bottom