Walimu karibu wote uwezo mdogo

Walimu karibu wote uwezo mdogo

Kama umesoma vyema hapo juu nadhani utakuwa umenielewa...waalimu wengi kama sio wote uwezo wao ni mdogo nikatoa na sababu tatu zinazopelekea mtu kuingia ualimu...hivyo kama ulisoma ualimu mwaka 2007 ukapata two ukaenda ualimu maybe ni sababu mbili zingine kama ni kweli

Tatizo lako umeoanisha neno uwezo wa akili na passing of national examinations. Sio wote wanaoshindwa ktk masaa 3 ya kutahiniwa somo wana uwezo mdogo. kuna many factors zinazoweza fanya mtu hasifanye vema kwenye mtihani. national exams kwanza sio reliable na valid measure ya kupima uwezo. hapo ndio ulipo ingia mkenge na kufikiri unachofikiri umekifanyia upembuzi yakinifu. Wapo walimu kwenye fani ya ualimu ni wazuri na wana uwezo mkubwa ila wali kosa opportunities za kudevelep potentials zao katika hatua fulani wakiwa mashuleni tokana na background zao au kukwamishwa na mzimu wa mitihani. Ingawa kweli pia wapo kundi la walimu ambao sio wazuri waliingia huko tokana na goli kupanuliwa kukawa ni mahali pa kuponea. kama hao walimu kama wana uwezo mdogo waliwezaje kukusaidia wewe hata ukafikiri umefanya utafiti. je hao maproffessor na ma-doctors si wamefundishwa na walimu unaofikiri wanao uwezo ndogo mpaka wakafikia hatua hizo?
 
Kwa alichaandika huyu mleta uzi itahitaji watu kama huyu 1000 kufikia uwezo wa mwl mmoja kwa kuunganisha akili zao..ameandika hovyo kabisa! Uwezo wake ni kama wa panzi!
 
Mna moyo mnaondelea kubishana na huyo mtu! Sababu zake amezitoa tatu, ikiwemo ya ufaulu hafifu, wepesi wa kupata ajira na kutokea familia maskini!

Sasa najiuliza mwaka 2005 nilichaguliwa kozi yake aliyosoma mtoa mada ya PSPA pale mlimani! lakini niliitosa baada ya kupata ushauri na kujichukulia zangu BAED! huku nikiwa na div.1.7(yeye ana div.1.9).

Mtoa mada anatambua (kama kweli ni msomi) ya kuwa zaidi ya asilimia 75 kwa sasa na wakati wetu ilikua asilimia 85 ya watanzania wote wanaishi kwa kutegemea kilimo tena cha jembe la mkono( hapa inamaanisha asilimia hizo za watanzania ni maskini kwa kuwa kilimo ktk nchi hii kimetelekezwa na siasa ndio kila kitu)

Sasa wewe kwa akili zako utaniona mimi niliyepata div1.7 ya hgl niliyechaguliwa PSPA na kuikacha eti nina uwezo mdogo kisa tu nimechagua ualimu ambao baada ya miaka 3 unamaliza na kuajiriwa! Yaani nisiangalie fursa nifuate tu mkumbo na sifa!! baadae niwasumbue ndugu na jamaa wanipe hela ya nauli nikafanye interview ambayo bila shaka sitafanikiwa kwa kuwa tu sina refarii wa kuniunganisha! Tuliyaona haya kule uhamiaji na sehemu nyingi yametamalaki.

Uwezo mdogo unapimwa kwa matokeo. Sekta zote ktk nchi hii watu wenye uwezo mdogo huwezi kuwakosa na sio walimu tu. Na huwezi kumlazimisha mtu afanye vile unavyotaka wewe. Au ulitaka wote tuliofaulu vizuri tukasomee hiyo pspa yako halafu tukimaliza tuanze kumaliza soli za viatu na bahasha zetu za kaki kutafuta kazi wakati tunafahamu mfumo wa ajira za upendeleo ktk nchi hii?

Na sisi tumekua wajanja! tupo huku kitambo, tunafaulisha sana tu wanafunzi, familia zetu zimepata unafuu, watoto wanasoma tena shule za st., mshahara kila mwezi, tumejenga, tunadrive, nk. na natoa rai kwa watu wote wanaotokea familia maskini kama mimi mkienda vyuoni someeni course ambazo mtapata ajira mapema ili mziokoe familia zenu na msihadaike na watu wa aina hii! mtajuta!! nchi hii ina matatizo mengi yanayoirudisha nyuma yakiwemo upendeleo na kubebana. Maisha ni akili yako tu.

Mimi hata nimuone msukuma mkokoteni siwezi kumdharau kwa kuwa ana ilisha familia yake kwa jasho lake na mimi sihusiki. Tuwe na utamaduni wa kuheshimu kazi za watu wengine na tusikwazane.
Mkuu umeongea kwa uchungu sana ,ila yote uliyoyasema ni kweli
 
Hahahahahah unenifurahisha sababu umeongea kikoro zaidi yangu, nimeingia pale 2010 na nafahamu nilichokiandika mpaka hivi leo nafahamu waliotandika three wamejaa pale UDSM hivyo acha kuongea kishabiki bila reference
Huwezi kusoma ualimu UDSM kama hujapata Division one kuanzia 2010 Nina uhakika soma hii 2015/2016
45bc28e7969f3b7d12a879034d09893e.jpg
d8649eb316f034d8be708c70b5edd28f.jpg
bd88356bb1b767066d8626f66e0ed30b.jpg

Nenda kaulize sio kubwabwaja tu hapa wewe ni nani kwani hadi unadharau walimu
Lazima na B+ B+ B nenda uhakikishe
 
Habari wanajamvi?

Ashakum sio matusi ila leo nimeamua kuleta mada hii baada ya kufanyia utafiti binafsi kwa muda hivi.Kwanza nilianza kuambiwa na rafiki yangu enzi hizo 2012 pale UDBS kwamba asilimia kubwa kama sio wote waalimu uwezo wao ni mdogo upstairs nikakataa akanitaka nifanye utafiti binafsi.

- Walimu wengi kama sio wote hawakupenda kuwa waalimu ila ufaulu wao ndio ulipelekea wakose option na kujikuta kwa shingo upande wanadumbukia kwenye fani ya ualimu bila kupenda.

-Asilimia kubwa ya walimu hawakupenda kwenda ualimu ila ukiachilia mbali ufaulu kuwa hafifu pia urahisi wa kuajiriwa, hii inatokana na ajira kuwa ngumu hivyo wengi kukimbilia ualimu ili kutatua matatizo yao ya ajira.

-Uchumi mbovu umepelekea wengi kuishia kuwa waalimu, hapa nina maana zile familia ambazo hazina uwezo wa kumlipia mwanafunzi kusoma kitu anachokipenda hivyo kujikuta akisoma ualimu ili apate ufadhili wa serikali.

Naomba nisieleweke vibaya ila jaribu kufuatilia kwa umakini uje unaimbie mwanafunzi aliyepata division one nzuri kabisa akawa mwalimu, asilimia kubwa ya waalimu ni waliosoma arts au biashara kwakuwa wengi matokeo yao hayakuridhisha hatimaye option pekee ikawa ualimu.

Waalimu wengi wa science walifeli hapa naomba uniletee mwalimu ambaye ama alisoma PCM, PCB, PGM n.k akapata divion one au two akaenda kusoma ualimu? Wanaokuwa waalimu wengi huangukia kwenye point ya ufaulu mbovu darasani na ni wachache sana huangukia kuwa waalimu sababu ya uchumi wa familia ila wengi saaana walifeli.

Hata kama walijiendeleza na kuwa na masters still ukirudi nyuma utakuwa wengi walifeli, ndio maana nikasema asilimia kubwa kama sio wote uwezo wao ni mdogo.
Sasa wewe uwezo mdogo unahusianaje na ulichoandika
Uo uwezo mdogo kiakili au kifedha
 
Sasa umefanya utafiti gani wakati ukipambanishwa kwa hoja unaleta visingizio
 
naomba nikusaidie ndugu..
hayo mawazo yako ni ya kizamani..
sasa hivi kuna rundo la walimu ambao walipata division one kwa pande zote mbili..
mimi binafsi nina division one na nachukua ualimu.
 
Huyu mleta mada ni mtu mwenye stress za maisha. Mara nyingi watu kama mleta mada ni wale ambao pesa hawana na kujifariji kwa vyeti alivyo navyo. Kusema waalimu hawako vizuri upstairs kisa matokeo ya form six ni tusi lisilovumilika. Kwenye haya maisha jifunze kutoropoka. Mleta mada pambana upate hela acha ujingaujinga wa kuandika ushuzi mtandaoni. Kwa hiyo kozi uliyosoma kama una ajira jihesabie ni mtu mwenye bahati kuliko wote duniani. Kuna wenzako wana hiyo public administration wanasota hatari.
 
Ok. Tukubali kwamba mwalimu alifeli form four ndio akaenda ualimu. Baadae akajiendeleza hadi bachelors au masters kama ulivyodai. Sasa kama alimudu haya masomo ya bachelor au masters bado unamuita upstairs zero? Umejaribu kuchanganua factors zinazofanya watu kuwa na division walizonazo walipokuwa sekondari? au unadhani ni akili tu? Mfano kuna form za necta unatakiwa ujaze kama unadhani factors nyingine haziko sawa ili usifanye mtihani fulani na kama ukifanya ni at your own risk. Ingekuwa division za sekondari ndio zinaakisi moja kwa moja uwezo wa kiakili wa mwanafunzi basi hao wenye division one wasingepata disco chuo au wenye division three wasingepata first au second class chuo. Katafiti tena.
 
Habari wanajamvi?

Ashakum sio matusi ila leo nimeamua kuleta mada hii baada ya kufanyia utafiti binafsi kwa muda hivi.Kwanza nilianza kuambiwa na rafiki yangu enzi hizo 2012 pale UDBS kwamba asilimia kubwa kama sio wote waalimu uwezo wao ni mdogo upstairs nikakataa akanitaka nifanye utafiti binafsi.

- Walimu wengi kama sio wote hawakupenda kuwa waalimu ila ufaulu wao ndio ulipelekea wakose option na kujikuta kwa shingo upande wanadumbukia kwenye fani ya ualimu bila kupenda.

-Asilimia kubwa ya walimu hawakupenda kwenda ualimu ila ukiachilia mbali ufaulu kuwa hafifu pia urahisi wa kuajiriwa, hii inatokana na ajira kuwa ngumu hivyo wengi kukimbilia ualimu ili kutatua matatizo yao ya ajira.

-Uchumi mbovu umepelekea wengi kuishia kuwa waalimu, hapa nina maana zile familia ambazo hazina uwezo wa kumlipia mwanafunzi kusoma kitu anachokipenda hivyo kujikuta akisoma ualimu ili apate ufadhili wa serikali.

Naomba nisieleweke vibaya ila jaribu kufuatilia kwa umakini uje unaimbie mwanafunzi aliyepata division one nzuri kabisa akawa mwalimu, asilimia kubwa ya waalimu ni waliosoma arts au biashara kwakuwa wengi matokeo yao hayakuridhisha hatimaye option pekee ikawa ualimu.
Waalimu wengi wa science walifeli hapa naomba uniletee mwalimu ambaye ama alisoma PCM, PCB, PGM n.k akapata divion one au two akaenda kusoma ualimu? Wanaokuwa waalimu wengi huangukia kwenye point ya ufaulu mbovu darasani na ni wachache sana huangukia kuwa waalimu sababu ya uchumi wa familia ila wengi saaana walifeli.

Hata kama walijiendeleza na kuwa na masters still ukirudi nyuma utakuwa wengi walifeli, ndio maana nikasema asilimia kubwa kama sio wote uwezo wao ni mdogo.

Unamuongelea mwalimu yupi ? Msingi, Sekondari au Chuo? Nahisi unachuki na wengi uliokuwa unasoma nao waliokuwa vipanga wanakuzidi wamekuwa walimu. Alafu hiyo kozi uliyosoma wewe, pale UD enzi zetu walikuwa wanasoma waliokosa kabisa uchaguzi wa kozi zingine,ilikuwa ni Altenative to life hasa kwa mtoto wa kiume kama wewe. Na wengi waliosoma kozi kama yako background yao hawakuwa wazuri darasani wengi tia maji tia maji walivyokuwa sekondari, so usijione unauwezo kuzidi walimu. Pia uwezo wa mtu ni zaidi ya Division.
 
Mkuu wewe unasoma? au ulisoma? Division 3 asome law yaani LLB? Mimi sijasoma hiyo law, masomo yangu ni ya sayansi na nimesoma miaka ya nyuma, lakini competition iliyopo kwenye hiyo LLB hasa kwa vyuo vinavyotambulika kama University of Dar es salaam sidhani. Labda inawezekana maana siku hizi vyuo vimekua kila mahala, vingine hata kwenye magodown ya bia. Tuseme ukweli tu, education entry points zake ni za chini ukilinganisha na kozi zingine.

Kitu nimekiona watu hata pale kwenye ukweli ulio wazi kabisa hawataki kukubali kwa sababu tu mtu yuko upande huo. Kila kitu kimekua ni siasa, mtu akiambiwa chama chake kina mapungufu hata umshikie bastola hawezi kukubali. Hivi kweli mtu anaweza kukataa kwamba ualimu ni kozi inayochukua wenye ufaulu mdogo? Najua utamaduni wa kukipenda chako ni muhimu, lakini pale unaposemwa ukweli watu wakubali. Hivi kuna uele ualimu wa grade III yaani baada ya form 4 mtu anaenda kusoma chuo cha ualimu aje afundishe primary (nasikia wameiondoa hiyo kitu au wanampango wa kuindoa), mtu aliyepata Division one atakwenda kusoma kweli hiyo UALIMU DARAJA LA III?


Hakuna mwenye Division one atakwenda kosoma ngazi ya cheti(certificate) kwa field yoyote, iwe ualimu,uhasibu, sheria n.k Rudini mkachunguze na kulinganisha zaidi katika ngazi zote kuanzia certificate mpaka degree kwa field zote entry point zipoje. Ikiwezekana mlete ushahidi wa vyuo mbalimbali msiongee kwa maneno tu. Na ualimu sio grade III pekee.
 
TEACOLTD Kwanza hongera kwa kuwa na ujasiri wa kuleta uzi huu maana sio viongozi wanaoongoza/simamia sekta ya elimu wala serikali kuu ilishawahi kukiri kuwa tuna tatizo la walimu wenye uweledi na kuwa na mkakati makhsusi wa kulitatua tatizo hilo.

Kimsingi yote uliosema ni kweli though naona Kuna simbilisi wanao comment kwa hoja zisizo na mashiko na nadhani ni kwasababu tu na wenyewe ama ndugu zao wamenufaika na huo mfumo ambao umetufikisha hapa kitaaluma.

Pili ualimu kama ilivyo kazi nyingine kama upolisi, jeshi hazichukuliwi serious na ndio imepelekea watu kuona hizi ni kazi za watu waliofeli, au kupata ufaulu duni hizi ndio kimbilio lao (kwa walimu wadau wameonyesha ufaulu na wako wanasoma wapi) Tatizo hili linaanzia primary huko ni zaidi ya time bomb watoto wanamaliza darasa la saba hawajui kusoma na kuandika but education system haijali, serikali ina focus kwenye enrolments, utawasikia tumevuka lengo la kuandikisha kwa 85% but does it make sense anyway! If at all these students finish std 7 and can't read and write! In 7yrs neither teachers themselves nor wasimamizi wa elimu has clue on what is going on! Halafu eti baada ya matokeo ya mitihani unakuja kutuambia watoto wameandika kat uni! !!!!!!

Hawa walimu wa shule za msingi hawawezi hata kufaulu ule mitihani wa darasa la saba kama ukiwapa wafanye sasa wanamfundisha nani? Hivyo Hivyo secondary wachukue walimu wa O-level wafanye mitihani wa kidato cha pili uone matokeo yake .

Elimu ni sekta ambayo inaelekea kuzimu TZ na si kwa bahati mbaya lakini ni matokeo ya makusudi ya serikali. Huwezi kuwa na serikali dhalimu iliyokosa hata haya , kama mtakumbuka awamu ya 4 pale watoto 60% walipofeli baada ya ku-acknowledge tatizo na kutafuta ufumbuzi serikali hatua iliyochukua ni ku-standardise matokeo ili tu kuwafool watanzania. Na IJULIKANE ni hao hao failures ndio waliobadilishiwa ufaulu na hatimae kuendelea na masoma na Leo/kesho ndio walimu so obvious mjinga atamfundisha mjinga mwenzake and we all know what will be the outcome!.

Leo mijadala mingi inajadili uwezo wa graduates wa Kitanzania(not only teachers) Kwamba hawana uwezo hata wa kujieleza wachilia mbali uwezo wa ku-deliver katika shughuli zao, the reasons ni kwamba Hawa si wengine ila ni matokeo ya huu huu uozo ambao for years umekua ukiendelea.

Ikumbukwe every child/person has the capacity to learn be it quicker or slow leaner it doesn't matter but it's upon the teacher to be able to;
1. Understand what he/she is supposed to teach (be conversant on the subject matter)
2. Be able to navigate that the class understand what he/she is teaching (teach-measure and evaluate)
3. Be warm, accessible enthusiastic and caring as it will open the desire for the students to ask where they don't understand
4. Set high expectations for all students
5. Inspire the students with his/her passion for education and for the course materials and constantly renews herself/himself as a professional on his/her quest in provide students with the highest quality education possible
6. Be able to "shift gear" -flexibility when a lesson isn't working. This kind of a teacher assesses his/her teaching throughout the lessons and finds new ways to present materials to make sure that every student understands the key concepts.

Mwisho serikali kupitia wizara husika andaeni walimu wenye sifa na sio utaratibu wa sasa wa mikakati zima moto. Let's be serious and select well qualified students for teaching career na sio failures ndo wanao kwenda ualimu na baadae kuja kufundisha watoto kwa level zote


Huyu mbwiga sijamuelewa! Mwl km anafundisha somo la kiswahili akipewa mtihani wa kidato cha pili unasema hawezi kuufanya? Njoo hapa nikutafutie swali hata la drs la 7 tuone kama utaliweza!
 
Huu utafiti nimeukubali,ni kweli kabisa asilimia tisini kama sio wote walimu walikuwa vilaza darasani au walikosa sifa za kusoma vitu vingne



Bila shaka mna stress za maisha nyie! Tuambie kazi yako hapa! Kama sio walewale wa GS halafu unajiona kiiiiichwa wkt ss tulikuachia ww mburura
 
Huu utafiti nimeukubali,ni kweli kabisa asilimia tisini kama sio wote walimu walikuwa vilaza darasani au walikosa sifa za kusoma vitu vingne



Bila shaka mna stress za maisha nyie! Tuambie kazi yako hapa! Kama sio walewale wa GS halafu unajiona kiiiiichwa wkt ss tulikuachia ww mburura
 
Huyo aliyekufindisha hiyo course chuoni naye ni mwalimu kwahiyo nayeye uwezo wake ni mdogo! Mburura kweli ww
 
Ufaulu nini? Je kuna uhusiano kati ya ufaulu na utendaji wako? Nini maana ya taaluma?bila shaka mtoa mada umri wake ni mdogo naomba asamehewe bure.
 
Hahahahaaa unajipooza bure Ndugu...sijaanza Leo, nimemaliza 2013 na ninachokiongea nina ushahidi nacho asilimia kubwa ya waalimu wanaangukia vipengele vitatu ila kikubwa ikiwa ni matokeo mabovu
Teh teh teh mkuu umechukuliwa mrembo na ticha nini, mbona unawakomalia hivyo walimu.
angalau ukumbuke walikufundisha ukafika unapoona ni pa maana kuliko walipo tena wewe umemaliza shule juzi tu, ukiambiwa mzee wako alifundishwa na walimu wa UPE Sijui yani std 7.
Research yako haiongezi thamani ya jamii yetu, add value or just chill.

Mimi sio mwalimu ila naitambua thamani ya mwalimu, unajua mwalimu ni mtu pekee anayejivunia mafanikio ya mtoto wa mtu mwingine bila kinyongo au unafiki? Walimu wanajivunia kufaulu kwa watu mnaojiona leo wa maana kuliko wao.
 
Habari wanajamvi?

Ashakum sio matusi ila leo nimeamua kuleta mada hii baada ya kufanyia utafiti binafsi kwa muda hivi.Kwanza nilianza kuambiwa na rafiki yangu enzi hizo 2012 pale UDBS kwamba asilimia kubwa kama sio wote waalimu uwezo wao ni mdogo upstairs nikakataa akanitaka nifanye utafiti binafsi.

- Walimu wengi kama sio wote hawakupenda kuwa waalimu ila ufaulu wao ndio ulipelekea wakose option na kujikuta kwa shingo upande wanadumbukia kwenye fani ya ualimu bila kupenda.

-Asilimia kubwa ya walimu hawakupenda kwenda ualimu ila ukiachilia mbali ufaulu kuwa hafifu pia urahisi wa kuajiriwa, hii inatokana na ajira kuwa ngumu hivyo wengi kukimbilia ualimu ili kutatua matatizo yao ya ajira.

-Uchumi mbovu umepelekea wengi kuishia kuwa waalimu, hapa nina maana zile familia ambazo hazina uwezo wa kumlipia mwanafunzi kusoma kitu anachokipenda hivyo kujikuta akisoma ualimu ili apate ufadhili wa serikali.

Naomba nisieleweke vibaya ila jaribu kufuatilia kwa umakini uje unaimbie mwanafunzi aliyepata division one nzuri kabisa akawa mwalimu, asilimia kubwa ya waalimu ni waliosoma arts au biashara kwakuwa wengi matokeo yao hayakuridhisha hatimaye option pekee ikawa ualimu.

Waalimu wengi wa science walifeli hapa naomba uniletee mwalimu ambaye ama alisoma PCM, PCB, PGM n.k akapata divion one au two akaenda kusoma ualimu? Wanaokuwa waalimu wengi huangukia kwenye point ya ufaulu mbovu darasani na ni wachache sana huangukia kuwa waalimu sababu ya uchumi wa familia ila wengi saaana walifeli.

Hata kama walijiendeleza na kuwa na masters still ukirudi nyuma utakuwa wengi walifeli, ndio maana nikasema asilimia kubwa kama sio wote uwezo wao ni mdogo.

!
!
Bahati mbaya ukakuta huyo mwalimu pia ni sisiem ndio balaa.. Anakuwa na uwezo kama wa kupe au akizidi sana wa kuku
 
Back
Top Bottom