Ulipigwa na TOT Taarabu,aliimba Ally Star....
Kaka nilichanganya na Nyama ya bata maana ni mwimbaji mmoja na bendi ni moja
nadhani unaitwa ZUMBUKUKU/ZUMBWEKUKU
Ni kweli kabisa, wimbo umeimbwa naTOT Taarab, umetungwa, umetiwa muziki na umeimbwa na Ally Star, unaitwa Kala hasara (Mdogo wa kimo unamambo wewe).
wakuu nashukuru kwa michango yenu nimekipata kitu kinaitwa [TABLE="class: wsite-not-footer, width: 2584"]
[TR]
[TD]
Sikutegemea wala sikudhani kama una mambo. Japo hauvumi kumbe umo?
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
wakuu na kitu chenyewe ndo hiki!ama kweli google iko juu unaweza ingia kwenye hiyo link ukasikiliza kitu kama wakipenda pia!!
KIITIKIO:
Ama kweli mlezi wako alokulea, Kala hasara
Ama kweli mwalimu wako alokufundisha, Kala hasara
Ama kweli mzito wako alokulea, Una mambo
Ama kweli mchumba wako ulompata, Kala hasara
Mdogo wa kimo una mambo wewe, una mambo wewe, una mambo
Nimeshaamini chochote kizuri hakikosi kasoro
Mama mkata umoja kala hasara huyo
Mtega uchumi kumbe nawe umo
Japo hauvumi kumbe nawe umo
Huko mitaani umepewa jina waitwa mama huruma we
Sikutegemea wala sikudhani kama una mambo
Wala hufanani na jambo la mtoto, una mambo wewe
Kila uonacho, Wakitolea macho wataka kukichukua
Japo siyo chako, Wakitolea macho wataka kukichukua
MABETI
1. Nilidhani mimi chanda Na wewe ni pete yangu
Nikawa ninakupenda Kukuona u mwenzangu
Kumbe nimefuga donda Lilowashinda wenzangu
Ikawa wagawa tenda Hata kwa rafiki zangu
Ikawa wagawa tenda Hata kwa wadogo zangu
Toka bibi fanya nenda Bora niishi kivyangu
Mimi sili vya kuvunda Hili ni zindiko langu
Wewe si mtu ni sanda Na hofu uhai wangu
2. Si kama nakutania Nakueleza bayana
Kwa kweli sikudhania Kama huna maana
Kumbe wewe kisinia Kote unajulikana
Umekuwa zabania Kugonganisha mabwana
Wewe siwakutania Wengi wanapongezana
Wanavyokugombania Kama mpira wa kona
Umegeuka gunia Kubeba kila aina
3. Mambo yako yanatanda Yazagaa kama wingu
Hupumziki kuranda Kutwa kucha wanguwangu
Unachokijua kwenda Huoni hata uchungu
Mgongo umekupinda Kwa kutaka vya uvungu
Pepo aliekupanda Hapungwi hata kwa nyungu
Nakuambia utakonda Huwezi ulimwengu
Umekuwa paka nunda Wa kunusanusa vyungu
4. Duka lako la asali Sasa linanuka shombo
Waja wamekutapeli Usiyepitwa na jambo
Hivi sasa huna dili Yanakuendea kombo
Ukipewa bia mbili Umekwisha huna nyimbo
Wajanja wenye akili Wanakuuza kimombo
Hujui lile na hili Kazi kufuata mkumbo
Umegeuka egoli, Hupigwi la mgambo
Source: Sikutegemea wala sikudhani kama una mambo. Japo hauvumi kumbe umo? - wavuti.weebly.com