Wale ambao hatutaoa kamwe tujadili namna ya kuhudumiwa uzeeni

Rwaz

JF-Expert Member
May 3, 2013
1,969
3,320
1610017213228.png
Ni hali halisi kuwa kupanga ni kuchagua. anayeoa na asiyeoa ni suala la mizani hiyo lakini ni ukweli usiopingika kuwa faida kubwa ya mwenza ni kwamba haujawai kuwepo mbadala wa mke/mme katika huduma za sirini hasa ukiumwa. ndugu na marafik huyeyuka mda wowote. upweke nao huleta kifo cha mapema.

Hata hivyo tuko katika nyakati za ndoa hatarishi tena za kukusababishia maradhi, msongo au kifo cha mapema kiasi kwamba hata mafanikio mengine kama mali na fedha yasiwe na tija kwako hapa duniani.

Basi kama tunakubaliana asiyeoa/asiyeolewa amejiepusha na mengi imebaki ni miundombinu gani mhusika na jamii tuwekeane ili ukifika hatua ya kuhitaj usaidizi nguvu zimekata bado uzipate. Nashauri tuanze na BIMA ya kutunza wazee. itasaidia sana. ikibidi ukizeeka pesa zako zikuogeshe, zikusafishe, zikulishe bila kulia lia kwa kila mtu awe ndugu au rafiki na jamaaa tena wanaotamani ufe wale vyako.

Tufike mahali jamii iaminishe kizazi cha leo na kesho kuwa ndoa si lazma wala si mafanikio(bali mafanikio ni kuishi vyema katika ndoa hiyo). Kuzaa si lazma hata unyanyasaji wa kijinsia utapungua hata wanaoweka ukosefu wa ndoa kwenye mikosa watapumua. KWA MAANA JAMBO MUHIMU KATIKA MAISHA NI MOJA TU ...KUWA NA FURAHA!

Pia soma:
Kwani lazima kuoana?
Mambo ya kuzingatia katika kuchagua mwenza wa maisha
 
Tatizo ni kutojua baada ya kufa unakuweje! kujiua hakujawai kuwa rahis kama ulivochapa. wahehe nawaogopa sana mimi. Hebu tupeane mikakat kuhusu sera, sheria,na mipango. mf napendekeza makampun makin yaanzishe BIMA ya kutunza wazee kwa hadhi zao.
 
Mwaka Jana niliskitika sana baada ya kutafakari kwa tukio LA kutambulishwa ukweni na kuanza kuwaza mawazo kutoka kwa pepo mchafu aitwae ndoa
Nakushukuru sana bidada kwa kuonesha makucha mapema hivyo ubaki mzazi mwenzangu tu


Na Mimi kama mwenyekiti wa hiki chama cha bachelor forever (BF) naunga mkono hoja ya katibu wangu


haya nakalibisha wajumbe kuweza kuchangia chochote kile ili kuweza kudumisha na kukuza chama chetu


BF hoyeeee3


Karibuni wajumbe
 
Na sisi tutakaochelewa kuoa pia mtupe mbinu za kusavaivu.
wewe sasa kama una mpamgo wa kuoa na uanelekea 40 shika kalam na karatasi, piga hesab za mtoto wa kwanza hadi anamaliza chuo utakuwa age gani, na last born utakuwaje. utajikuta kuna hatar ukafa hujawai kuishi. unahangaika na familia tu! ila kama utashupaza shingo bas niongeze tu USIOE BINTI AU DADA MDOGO KUIFURAHISHA NAFS KUWA UMERUDI UJANANI. utaishi kwa tabu ya hofu ya kuibiwa na hofu ya underperformance kias kwamba katakupelekesha ka mke dogo dogo utakufa mapema mno. oa mkubwa mwenzio. kama ameachika ni added advantage.
 
Nikajua unawasaidia hawa jamaa zako wafanye mchakato tu mapema iwezekanavyo, wasije kutaabika wakatutoka mapema
 
wewe sasa kama una mpamgo wa kuoa na uanelekea 40 shika kalam na karatasi, piga hesab za mtoto wa kwanza hadi anamaliza chuo utakuwa age gani, na last born utakuwaje. utajikuta kuna hatar ukafa hujawai kuishi. unahangaika na familia tu! ila kama utashupaza shingo bas niongeze tu USIOE BINTI AU DADA MDOGO KUIFURAHISHA NAFS KUWA UMERUDI UJANANI. utaishi kwa tabu ya hofu ya kuibiwa na hofu ya underperformance kias kwamba katakupelekesha ka mke dogo dogo utakufa mapema mno. oa mkubwa mwenzio. kama ameachika ni added advantage.
Sijakuelewa hapo uliposema kuna hatar ukafa hujawai kuishi
 
Tafuta pesa za kutosha vinginevyo uzee itakuwa ni shughuli pevu.
pesa ndo msingi wa kila kitu, kila mipango. usisahau kuwa unaweza kuwa na pesa ukazeeka ndo ikakutesa mana utazungukwa na wanaoitaka hiyo pesa. hata kukupumzisha kabla ya wakati waile vzuri.
 
Sijakuelewa hapo uliposema kuna hatar ukafa hujawai kuishi
kufa bila kuishi ni hali ya kuwa na majukum yasiyoisha kias kwamba kila ukimaliza hili upumzike kula matunda ya kazi ya mikono yako(UISHI), unajikuta una jukum linakusubiri la muhim. ni kama kufikisha miaka 70 bado unasomesha. kuna age uanze kula ulichopanda. usiwe na jukum lisiloepukika km ujenzi wa makaz, kusomesha, biashara ya kusafiri, kuoa/kuolewa. utaishi mda mrefu zaid.
 
pesa ndo msingi wa kila kitu, kila mipango. usisahau kuwa unaweza kuwa na pesa ukazeeka ndo ikakutesa mana utazungukwa na wanaoitaka hiyo pesa. hata kukupumzisha kabla ya wakati waile vzuri.

Hivi siku hizi kuna huduma ya nyumba za kutunza wazee huko Tanzania? (nursing homes)..kama hakuna tafuta familia hata kama ni ku adopt, unaweza ukawa na pesa uzeeni na ukawa mpweke,mwenye sononi...na kama hamna huduma ya nursing home nani atakutunza?? lazima ufikiri hizo trade offs kabla ya ku make decision not to have a family.
 
Mtakuwa mnajinyea na hakuna wa kuwaosha mnathamani marafiki watakuwa wanawapita tu kama hawawaonj
Dooh..Kuna Mama mmoja Miaka kama 57...anahaingaika na mume wake 66.. dialysis kila Baada ya siku moja...na hospital yenyewe Benjamin Mkapa...ipo mbaaali karibia Km 20 from anapoishi
 
Back
Top Bottom