GE2025 Wakuu wa vyombo vya habari wahimiza amani kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025

GE2025 Wakuu wa vyombo vya habari wahimiza amani kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Wakuu wa vyombo vya habari na wahariri waandamizi nchini Tanzania wamekutana leo oktoba 25, 2025 katika jengo la Millenium Tower Jijini Dar es Salaam na kuzungumza na watanzania kupitia vyombo vya habari kuelekea uchaguzi mkuu oktoba 29, 2025.

Tukio hilo lilikuwa na dhumuni la kuwakabidhi waandishi wa habari azimio lao lililoandaliwa kwa lengo la kuwaasa watanzania kulinda amani, utulivu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu na kuwaomba kutoshiriki meza moja na wenye kauli zinazochochea kuvunjwa kwa amani


View: https://www.youtube.com/live/sxKRKH-U7MY

Azimio hilo limesomwa na mkuu wa wakuu wa vyombo vya habari TANGE likiwa limebeba mambo 11


===
  • Tanzania ilipata uhuru wake mwaka 1961 kupitia jitihada za majadiliano, mazungumzo na hoja za wanasiasa, wakipingana bila kupigana. Watanzania tuna wajibu wa kuendelea kujenga demokrasia yetu kwa majadiliano na hoja, tukipingana bila kupanga kupigana.

  • Demokrasia yetu bado ni changa. (Demokrasia siyo kama mtoto wa nyumbu anayezaliwa sasa na hapo hapo akaanza kukimbia kwa kasi kama wazazi wake). Demokrasia ni mchakato endelevu unaopaswa kujengwa kila siku kwa kuhakikisha kila hatua inalindwa na wadau wote.

  • Sisi Wakuu wa Vyombo vya Habari na Wahariri Waandamizi tuliokutana wiki hii, tunaamini katika kushamiri kwa demokrasia ya vyama vingi. Ni dhahiri kuwa vyombo vyetu vimetoa mchango mkubwa katika kuijenga na kuishamirisha demokrasia ya vyama vingi kwa miongo zaidi ya mitatu sasa.

  • Tuliripoti na hata kuandika tahariri pale vyama vya siasa viliposuguana hasa nyakati za uchaguzi na kusababisha vurugu, kama ilivyowahi kutokea Zanzibar mwaka 2001 baada ya Uchaguzi Mkuu.

  • Aidha, kwa muda mrefu vyombo vyetu vya habari vimeripoti sana matukio ya vurugu, uvunjifu wa amani, vita vya wao kwa wao na hata mauaji ya kimbari, kwenye mataifa mbalimbali ya Afrika, yaliyoathiriwa na siasa chafu na kuingiliwa na maadui wa nje. Kwa maneno mengine, machafuko, mateso na mauaji ya wananchi wasiokuwa na hatia katika nchi hizo, yalisababishwa na ubinafsi wa vikundi vya wanasiasa walioamua kutumia propaganda za kugawa watu, bila kujali maslahi mapana ya mataifa yao. Na ni dhahiri kuwa mataifa makubwa yakiwemo ya wakoloni yamekuwa yakichangia kuvuruga amani kwenye mataifa ya Afrika ili kuendeleza maslahi yao ya kiuchumi.

  • Katika siku za karibuni, hapa Tanzania tumesikia kauli zinazochochea chuki na shari, jambo ambalo haliakisi kabisa utamaduni wa Mtanzania. Kauli zinazohamasisha wananchi kufanya vurugu, kuchoma vituo vya mafuta, vituo vya polisi na mali nyingine, siyo tu ni kosa kisheria, bali ni kauli zisizoakisi Utanzania wetu na zinazopaswa kukemewa na kila Mtanzania.

  • Mataifa yaliyotumbukia katika machafuko ya kisiasa, vita vya wao kwa wao na mengine kukumbwa na mauaji ya kimbari, yalianza na kauli chochezi za mtu mmoja mmoja, baadaye vikundi na hatimaye zikatengeneza.

  • Zipo nchi nyingi, zikiwemo jirani zetu Rwanda na Kongo, kule Sierra Leone, Ivory Coast, Liberia, Somalia, Sudan na nyinginezo, ambazo zimebaki na makovu ya "Uwendawazimu wa Kihaldiki" ambayo, hata pale amani iliporejea (au itakaporejea), bado makovu hayo yataendelea kubaki kama sanamu ya kumbukumbu ya majuto!

  • Tanzania imekuwa kisiwa cha amani kwa sababu ya misingi iliyowekwa na waasisi wa Taifa letu na utamaduni wa kukaa katika meza ya mazungumzo ili kumaliza tofauti zetu. Na kwa sababu hiyo, kwa miaka mingi, Tanzania imekuwa ni makazi ya matumaini kwa wakimbizi wanaokimbia machafuko ya kisiasa na vita katika nchi zao.

  • Hivyo basi, Watanzania, kwa umoja wetu tukatae kuhudhuria karamu ya uchochezi wenye lengo la kutushawishi kulewa "Uwendawazimu wa Kiholaiki", ambao unaweza kulisambaratisha Taifa letu kama ilivyotokea katika mataifa mengine!

  • Sisi Wakuu wa Vyombo vya Habari na Wahariri Waandamizi tunaungana na viongozi wa dini na makundi mengine yaliyojitokeza kusisitiza umuhimu wa kutunza amani tunapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba.

1761386352213.png

1761386366204.png

Pia soma ~
Uchaguzi Mkuu wa 2025 na uadilifu wa Vyombo vya Habari Tanzania
 
Kwa hiyo media hazitoripoti upande wa pili kwa Wananchi kwa hofu ya kuvuruga amani. Nani anavuruga amani? yaani hata hawa wamewewesuka na maandamano yasiyokuwepo? Hivi nyakati hizi kuna media inaweza kuacha kuripoti habari fulani kwa wananchi wasijue halafu ikawa hivyo?
 
Pumbavu, account zinasoma matrilioni unadhani watakuwa na uchungu gani.
 
Ayubu na Balile wakakusanya wakuu wa media zote chapchapu wakasainishwa tamko lao la ajabu! dakika chache wakawa live na kumaliza jambo lao. Mbona nao wameingiwa na hofu ya maandamano yasiyokuwepo? kwa hiyo habari za maandamano hayo hazitaripotiwa na hizo media?! kwani ni wao tu ndio wana uwezo wa kuripoti habari hizo mpaka wafikie kutoa tamko lao? AMANI ipo tele na itaendelea kuwepo, palipo na haki pana amani
 
Wanakuja kusoma script ya Gerishoni
 
Wanasemaje!? Siwezi poteza muda na MB zangu kusikiliza hao KENGE..
nitaomba AI I summarise kwa ajili yangu
 
Uchaguzi utapita salama na maisha yataendelea! Hatuwezi kabidhi Nchi kwa wahuni na wenye mihemko ya balehe!!
 
propaganda
hizi proganda zinatakiwa zifanywe na media za ccm and alike na wale pro ccm tu, the rest media waachwe huru wajiamulie ni wapi watafanya propaganda. Labda kama nchi ingekuwa inakabiliana na propaganda za nje hapa ingekuwa sawa media zote ziungane dhidi ya propaganda za nje. Propaganda za humuhumu kwa wananchi kwa wananchi ni kituko
 
Media zingine hapa zimeburuzwa tu kusaini ili zisipate shida ila dhamiri zao zinawahukumu
 
Mbona wanasema hamna atakayeandamana? Nini kinawatoa mapangoni kwa zamu?
 
Video kwangu haijafunguka..

Yaani wanahabari wameungana kutuambia,
Nchi imeshinda tuzo ya uhabari wao?

Hii ilishawahi kutokea nchini Kabla?

Kuna mafunzo wanatoa ya kusomea cheti cha uhabari au nini haswaa?

Nawashwa nambieni basi tufurahie tuzo.
 
Ninamheshimu tu Mwalimu wangu Dokta Ryoba na Dada yangu Joyce Mhavile na niliyonayo Moyoni ngoja niyahifadhi.
joyce anasaini, uso wake na moyo wake hauna ushirikiano dhamiri inamhukumu, hapa kaburuzwa tu kama wenzake wengine wanavyoburuzwa na ayubu na balile. Mgeacha tu kila media iwe huru kuripoti maana waandishi ni wasomi wana maadili ya kazi yao na ni wazalendo wa nchi yao
 
Back
Top Bottom