Wakuu tupunguze ubinafsi

Mzee wangu aliniambia kwamba "huwezi kumfanya mtu aendelee (kumtoa mtu) mtu anajiendeleza mwenyewe"
Hii kauli sasa hivi naiona ya ukweli 100%. Wewe unaweza kuwa na uweza na ukawa hadi unatuma pesa kijijini ili watu wajenge na waanzishe miradi lakini siku ukirudi unakuta yule uliyemtumia ameongeza mke wa pili na hakuna mradi wowote..
Au unamlipia mtu ada likizo anarudi na 0 kitu pekee alichoweza ku-achieve ni kunyoa kiduku kichwani.
Sasa watu wa hivyo utawapa msaada gani?? Ndugu wa hivyo usipoangalia wanaweza kukurudisha kwenye circle of poverty tu. Kwahio kitu bora cha kufanya ni kutembea na wale wanaoweza kupokea msaada wako na kuufanyia kazi wawe rafiki , au hata ndugu wa mbalii.

NB. Cha muhimu wazazi usiwasahau tu. Lakini ndugu wengine kama hawana akili ya kujiendeleza wenyewe hata ukiwa unawapa mil 10 kwa mwezi utakuwa wameongeza wake na kulewa tu.
Kwa nini inakuwa hivyo,wanakuwa hawana uchungu na unachowapatia au ni kutaka kurudishana nyuma tu?
 
Kama unaakili timamu fahamu fika hakuna binadam aliyefanikiwa akiwa peke yake bila ya kupata msaada either direct or indirect kutoka kwa wazazi, ndugu, watu baki au jamii inayomzunguka kwa ujumla.

Hivyo basi tukumbuke sana fadhila na ihsani, tuache roho mbaya kwa kujitahidi kutoa kadri ya uwezo wetu katika kila tutakacho ruzukiwa na Muumba.

Ndio maana katika dini zote husisitiza sadaka na (zaka) fungu la kumi na sadaka au zaka ile iliyobora zaidi huanzi ngazi ya familia, ukoo, majirana na jamii kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom