KERO Responded Wakulima wa tumbaku Mpanda Kati walalamikia makato ya 3% na kutolipwa fedha zao

KERO Responded Wakulima wa tumbaku Mpanda Kati walalamikia makato ya 3% na kutolipwa fedha zao

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Wakulima wa zao la tumbaku kutoka Chama Cha Msingi Cha Ushirika Cha Wakulima wa Tumbaku Mpanda Kati, Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamelalamika kutolipwa fedha zao hadi hivi sasa licha ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kutoa maagizo kwamba kabla ya siku kuu ya Nanenane Wakulima wote wanatakiwa kulipwa.




Leo Jumatatu August 11, 2025, Baadhi ya Wakulima hao wakiwa katika Ofisi ya Chama Cha Msingi hicho mbali na kulalamikia kutolipwa fedha zao na kuwa chama pekee mkoani Katavi ambacho Wakulima wake hawajalipwa pia wamelalamikia nyongeza ya makato ya fedha ya asilimia 3 kinyume na utaratibu wa vikao.

Meneja wa Chama cha Msingi hicho baada ya kutafutwa alisema yuko benki kwa ajili ya kushughulikia matatizo hayo ya wakulima.

Kusoma ufafanuzi zaidi, bofya hapa ~ Zaituni Tembo: Kweli hatujawalipa Wakulima wa Tumbaku, kwa sasa hivi tuna Bima ya Mkopo kutoka Benki ya NMB

Pia soma ~ DC Tanganyika aagiza Wakulima wa Tumbaku walipwe haraka iwezekanavyo fedha zao
 
sio 3% ya malipo mkulima mwongo mwongo hii n 3% iko kwenye mkataba kama bima ya zao (yeye anaita bima ya ajali)

hii bima ya ajari itakuwa kwenye mkataba unapo ingia mkataba na benki ni umekubali masharti ya kulipia hii bima

sasa dola kushuka si ndo shilingi kuimarika hataki shilingi ipande thamani (kiukweli fedha inapungua maaa kama ulikuwa na dola mia badala upate 2,600 utapata 2,400)

hawa wakulima wawe wanahudhuria mikutano na vyama vyao vitoe semima za mara kwa mara ili kujenga uelewa tofauti na hapo itaonekana kama ni wizi na ujanja ujanja
 
Back
Top Bottom