Complicator
JF-Expert Member
- Aug 23, 2013
- 2,198
- 3,566
Kwa wasiojua historia ya huyu binti kwa kifupi ni kwamba alipata ajali ya kugongwa na gari akiwa katika mahafali yake ya elimu ya sekondari, ajali iliyompelekea kupata jeraha kwenye uti wa mgongo kisha ulemavu wa kupoza sehemu ya mwili wake.....
Kwenye siku ya walemavu ameandika haya
"Nilivyopata (JUM) jeraha la uti wa mgongo (ulemavu) ambao kupona kwake bado kunafanyiwa utafiti, ilinibidi niikubali hali hii mpya kwangu ya ulemavu.
Ilinibidi nianze kusoma na kujifunza kuhusu jerala la uti wa mgongo na yote yanayoizunguka hali hiyo. Mengine yalikuwa magumu kumeza lakini ndio tayari yalikuwa ya kwangu so nikayaelewa kama yalivyo bila ku-judge wala kuweka critics.
Ikafika muda nikawa najielewa na naujua mwili wangu kuliko nilivyowahi kuujua kabla sijapata JUM. JUM imefanya afya yangu iwe mgogoro lakini baada ya kujijua nikawa naitunza afya niliobaki nayo (A) naitunza mimi mwenyewe (B) naitunza kwa umakini mkubwa sana.
Mikono yangu haishiki, miguu haitembei, siwezi kukaa wala kujilaza mwenyewe, siwezi kwenda haja kawaida kama zamani hivyo kujitunza mimi mwenyewe ni ngumu kimtindo.
Lakini ndugu na jamaa mnaoona hii post, niliruhusiwa na wazazi wangu kuhamia kwangu nijitegemee mwenyewe kwa sababu hii kubwa; NAWEZA KUJITUNZA MWENYEWE. Sio kifedha wala sio ki-material.
Hivi sasa sasa naweza nikaishi na msaidizi yeyote yule ili mradi ana utayari. Najua kila kitu kuhusu mimi. Saa ngapi nilale, nile kipi, nipumzike staili gani, niogee sabuni gani, ninywe maji gani, nikalie kochi lipi, nioge mara ngapi nk nk.
Hio mifano niliyotaja inahitaji utayari wa mtu.
Mimi nikisema mama siwezi kuishi bila wewe sidanganyi ni kweli ni ngumu sana kuishi bila mama, nikisema siwezi kuhakikisha usafi wa mwili wangu umeenda sawa ni kweli kwasababu ni kweli sijisafishi mimi. LAKINI nilipokubali kujihusisha na maisha niliyonayo sasa, nimejikuta nikiweza yasiowezekana. Mimi pia narudisha utukufu kwa Mungu kwasababu sijui bado inawezekanaje lakini wapendwa Imewezekana mimi kujihudumia mwenyewe kwa HALI hii takribani miezi 13 sasa.
Tukiwa tunaadhimisha #internationaldisabilityday napenda kutoa wito kwa wenzangu wenye ulemavu ku-take part kwenye maisha yetu. Tuwe mstari wa mbele kujipenda na kujitunza. Tuwape ushirikiano wazazi na wapendwa wetu, na wote waliochagua kuwa upande wetu, tuwape wepesi.
Ni ngumu sana mwanzoni - ILA INAWEZEKANA. Na baadae ukizoea mimi ni shuhuda namba 1 nakuhakikishia sio ngumu kama tunavyodhani kabla hatujajaribu."
Kwenye siku ya walemavu ameandika haya
"Nilivyopata (JUM) jeraha la uti wa mgongo (ulemavu) ambao kupona kwake bado kunafanyiwa utafiti, ilinibidi niikubali hali hii mpya kwangu ya ulemavu.
Ilinibidi nianze kusoma na kujifunza kuhusu jerala la uti wa mgongo na yote yanayoizunguka hali hiyo. Mengine yalikuwa magumu kumeza lakini ndio tayari yalikuwa ya kwangu so nikayaelewa kama yalivyo bila ku-judge wala kuweka critics.
Ikafika muda nikawa najielewa na naujua mwili wangu kuliko nilivyowahi kuujua kabla sijapata JUM. JUM imefanya afya yangu iwe mgogoro lakini baada ya kujijua nikawa naitunza afya niliobaki nayo (A) naitunza mimi mwenyewe (B) naitunza kwa umakini mkubwa sana.
Mikono yangu haishiki, miguu haitembei, siwezi kukaa wala kujilaza mwenyewe, siwezi kwenda haja kawaida kama zamani hivyo kujitunza mimi mwenyewe ni ngumu kimtindo.
Lakini ndugu na jamaa mnaoona hii post, niliruhusiwa na wazazi wangu kuhamia kwangu nijitegemee mwenyewe kwa sababu hii kubwa; NAWEZA KUJITUNZA MWENYEWE. Sio kifedha wala sio ki-material.
Hivi sasa sasa naweza nikaishi na msaidizi yeyote yule ili mradi ana utayari. Najua kila kitu kuhusu mimi. Saa ngapi nilale, nile kipi, nipumzike staili gani, niogee sabuni gani, ninywe maji gani, nikalie kochi lipi, nioge mara ngapi nk nk.
Hio mifano niliyotaja inahitaji utayari wa mtu.
Mimi nikisema mama siwezi kuishi bila wewe sidanganyi ni kweli ni ngumu sana kuishi bila mama, nikisema siwezi kuhakikisha usafi wa mwili wangu umeenda sawa ni kweli kwasababu ni kweli sijisafishi mimi. LAKINI nilipokubali kujihusisha na maisha niliyonayo sasa, nimejikuta nikiweza yasiowezekana. Mimi pia narudisha utukufu kwa Mungu kwasababu sijui bado inawezekanaje lakini wapendwa Imewezekana mimi kujihudumia mwenyewe kwa HALI hii takribani miezi 13 sasa.
Tukiwa tunaadhimisha #internationaldisabilityday napenda kutoa wito kwa wenzangu wenye ulemavu ku-take part kwenye maisha yetu. Tuwe mstari wa mbele kujipenda na kujitunza. Tuwape ushirikiano wazazi na wapendwa wetu, na wote waliochagua kuwa upande wetu, tuwape wepesi.
Ni ngumu sana mwanzoni - ILA INAWEZEKANA. Na baadae ukizoea mimi ni shuhuda namba 1 nakuhakikishia sio ngumu kama tunavyodhani kabla hatujajaribu."