Uchaguzi 2020 Wako wapi Makada kindaki ndaki wa CCM?

Kuna mpuuzi hapa asubuhi ananiambia katoka kumpigia magufuli huko kanda ya ziwa ilihali nafahamu kabisa alikua na vigezo ila kanyimwa mkopo na pia hta akimaliza hiyo degree hana uhakika wa kupata mtaji (Kupitia zile 10% za halmashauri) ama kupata ajira sababu Private sector imekufa na serikali imeshindwa kuchochea uchumi.

Then najiuliza nyie watu mnajitambua kweli? Na sio ww tu ni waTZ kibao unakuta kapigika haswaa ila bado ni CCM? Fikiria wakulima waliopigika wa korosho, pamba, wafugaji huko meatu n.k huna ndugu huko? Huna ndugu mkulima ambaye anategemea jembe na serikali yenu imeshindwa kabisa kumsaidia kuattain kilimo cha kisasa? Huna ndugu kabisa aliyeumia na sera mbovu za kilimo?

Well uwe msafirishaji bidhaa nje, hivi kuwa mkweli tu mauzo yameshuka kuliko awamu iliyopita kwa mujibu wa takwimu za BOT. Sasa ww umeathirika pia ila unaenda mpigia kura Magu then tusikie siku mnakuja kulalamika hapa cjui TRA cjui mauzo cjui bureaucracy mpakani na blah blah zingine.

Kwa mentality hizi tutatawaliwa na CCM mpaka Yesu anarudi afu tutakuwa tunatafuta mchawi ni nani wa umaskini wetu.
Sawa mwamba.
Ila sasa Lissu hajathibitisha wala wewe umeshindwa kabisa kunithibitishia kwamba Lissu akiwa Rais masikini hawatakuepo na watu wote watapata kazi nchi nzima.
Au ungenipa hata kamfano kadogo kwa nchi za Africa zote zilizoshikwa na vyama pinzani mambo yapoje kwa sasa,tukianzia na hapo jirani Kenya,Zambia n.k?
 
Mzee Pascal Mayalla kwa dalili za awali ya yote yanayoendelea unaona kuna uwezekano wa mpinzani kushinda na kutangazwa?
Dalili za upinzani kushinda hazipo kwani dalili hizi zilijidhihilisha kwenye wakati wa kampeni na hata kabla ya kampeni kuanza.
Hakuna jinsi yoyote ya kuishinda ccm iliyojipambanua vyema kabisa kwenye uuzaji sera na mikakati ya kuwaletea watanzania mabadiliko ya kweli.
mtasingizia NEC,mtasingizia kuibiwa kura n.k lkn deep inside your heart,you know it,you have already lost the battle even before the beggining of the battle itself.
Baada ya uchaguzi huu,vyama hasa vikubwa vya upinzani vitakuwa na kazi ya kubadili sera,itikadi na mifumo yao ili iendane na siasa za sasa kama kweli vina nia ya kubaki kwenye ulingo wa siasa,vinginevyo
 
Hiki ndicho kinachokwenda kutokea, Amiri Jeshi wetu Mkuu aliitangazia dunia, uchaguzi utakuwa huru na wa haki, amani itatawala, na mshindi ndiye atatangazwa mshindi!.
Hatuutaki ule uhuni wa watu fulani zile chaguzi za nyuma, mtu aliyeshindwa anajitangaza alishinda kura zake zikaibiwa!.
Safari hii ni anayashindwa akubali kushindwa na kumpongeza mshindi.
P
Aliitangazia Dunia anayoiita Mabeberu? Uhuru wa taarifa kusambaa kwa kusababisha jam kwenye mtandao mpaka walioko ng'ambo wametoa tamko? Al Jazeera umeona jana kilichokua kinaendelea ila sababu waandishi kama wewe na wenzio mmekanyagwa na jiwe mmebaki kusifia ila ni wafungwa mnaoishi majumbani kwenu! Nkt
 
Sawa mwamba.
Ila sasa Lissu hajathibitisha wala wewe umeshindwa kabisa kunithibitishia kwamba Lissu akiwa Rais masikini hawatakuepo na watu wote watapata kazi nchi nzima.
Au ungenipa hata kamfano kadogo kwa nchi za Africa zote zilizoshikwa na vyama pinzani mambo yapoje kwa sasa,tukianzia na hapo jirani Kenya,Zambia n.k?
Kenya wamesogeza mamlaka kwa wananchi kupitia devolution kitu ambacho TZ tumeshindwa hadi kupelekea regional disparities yaani uchumi wa ilala pekee unazidi mikoa yote ya kusini. Ila unadhani kupitoa devolution leo hii mtwara isingenufaika na korosho zake ama Gesi asilia?

Sasa sera kuu ya CHADEMA ni devolution kupitia serikali za majimbo/kanda ili kufikisha maendeleo kwa glassroots.

Hiyo ni eneo moja tu mind you lakini limeleta faida lukuki kwa jirani zetu.

Lissu naamini atabadilisha vitu vingi sababu hana affiliation zozote na yeyote aliyepo madarakani sio kma JPM mpaka leo alishindwa wadaka wezi wa Escrow ama EGMA kisa ni bureaucrats wake.

Mind you Lissu atataka kuprove a point ili ajizatiti madarakani na kuepuka kuwa one term President so lazima tu atafanya reform zote alizoahidi.

Pia historia yake ya uadilifu inambeba kma angekua fisadi au hana ufanisi tungemtilia shaka. Ila sababu taasisi zote alizopita kaacha impact then tuamini hawezi shindwa akiwa ikulu.

Kiufupi he'll improve alipoishia Magufuli ili asirudie makosa aliyopinga. Na usilinganishe na wapinzani wa huko Zambia ambao 90% walitoka CCM zao, ila Lissu ni pure opposition 100%
 
Dalili za upinzani kushinda hazipo kwani dalili hizi zilijidhihilisha kwenye wakati wa kampeni na hata kabla ya kampeni kuanza.
Hakuna jinsi yoyote ya kuishinda ccm iliyojipambanua vyema kabisa kwenye uuzaji sera na mikakati ya kuwaletea watanzania mabadiliko ya kweli.
mtasingizia NEC,mtasingizia kuibiwa kura n.k lkn deep inside your heart,you know it,you have already lost the battle even before the beggining of the battle itself.
Baada ya uchaguzi huu,vyama hasa vikubwa vya upinzani vitakuwa na kazi ya kubadili sera,itikadi na mifumo yao ili iendane na siasa za sasa kama kweli vina nia ya kubaki kwenye ulingo wa siasa,vinginevyo
Hapa tu ndio mnashangaza, sasa kma mnajua ushindi ulikua obvious kulikua na haja gani ya kumfungia mtu kampeni, kuengua wagombea, kukataa kuapisha mawakala?
Hata upinzani uje na sera gani kma CCM mtaendelea kucheza rafu za uchaguzi basi tutegemee comment za namna hii kila mwaka.
 
Niko kituoni na washirika wenzangu muda sasa. Kimya kimya lakini hamasa kubwa moyoni.

Iziraeli atupishilie mbali.

Tunataka haki. Inshallah kutokana na haki amani hapa itatamalaki tu.

Sala zetu kote haki na ikatendeke tukiwakumbuka wale wote waliotutangulia kwa kusimama na haki.

Nimekuwa naangalia nyuzi mbali mbali tangia jana, hata huko kwenye mitandao mingine ambako bila VPN ni kweusi. Ma lb7, mataga na mshabiki nguli wa chama mboga mboga wote wamepotea.

Au labda hawataki kutumia VPN kuitikia mapenzi ya chama chetu? Au nao ni mshabiki wa hii mitandao kupotea ikibidi moja kwa moja?

Eeh mola wetu mshindi na akatangazwe mshindi.

Amani na ikawe na kila mpenda haki.

Tunayo siku ndefu leo inshallah.
Amebaki yule choko wao mkuu paskalina mayala, akiendeleza nyuzi zake za kulamba matercore mabwana zake
 
Mbuzi kweli wewe.....
Watu tunatumia dedicated internet wewe unaongea upuuzi wa ufipa...
Alafu tuko tunahamasishana huku mitaani sasa wewe endelea hamasisha kwenye vpn...wakati luna pini..sijui unamhamasisha nani..
Bavicha mko nyuma sana aisee
Mbuzi babakooooo
 
Sawa mwamba.
Ila sasa Lissu hajathibitisha wala wewe umeshindwa kabisa kunithibitishia kwamba Lissu akiwa Rais masikini hawatakuepo na watu wote watapata kazi nchi nzima.
Au ungenipa hata kamfano kadogo kwa nchi za Africa zote zilizoshikwa na vyama pinzani mambo yapoje kwa sasa,tukianzia na hapo jirani Kenya,Zambia n.k?
Waswahili wanamsemo usemao,kheri nusu shari kuliko shari kamili,au zimwi likujualo alikuli likakwisha.

Kheri kuendelea na ccm hii iliyoamua kutubu makosa iliyowatendea watanzania na kuamua kuwatumikia kupitia JPM kuliko hao walanguzi wa siasa ambao sasa wamewageuka watanzania na kuwa watetezi wa mabepari kwa kuikingia kifua mikataba yote ya kidhalimu iliyolitafuna Taifa hili,wakizunguka dunia nzima wakilisema vibaya Taifa hili na hata kuyashawishi Mataifa yavunje mahusiano na kutunyima misaada.

Kusuka mipango ya kutaifisha mali za Taifa hili( ndege).
Na leo wanataka kutugawa kwa kutuletea selikali za majimbo ambazo zimesababisha majirani zetu kenya waendelee kutafunwa na ukabila.

Wanataka kumaliza raslimali zote za Taifa hili kwa kuziweka rehani ili kuendesha nchi,vizazi vijavyo havitakuta urithi wowote.

Na mwisho wanataka kutuvunjia muungano utafikiri hiyo ndio itakuwa suluhu ya umaskini wa mtanzania.Ukishavunja muungano maana yake hata maadui wasiolipenda Taifa hili umewafungulia milango
 
Kenya wamesogeza mamlaka kwa wananchi kupitia devolution kitu ambacho TZ tumeshindwa hadi kupelekea regional disparities yaani uchumi wa ilala pekee unazidi mikoa yote ya kusini. Ila unadhani kupitoa devolution leo hii mtwara isingenufaika na korosho zake ama Gesi asilia?

Sasa sera kuu ya CHADEMA ni devolution kupitia serikali za majimbo/kanda ili kufikisha maendeleo kwa glassroots.

Hiyo ni eneo moja tu mind you lakini limeleta faida lukuki kwa jirani zetu.

Lissu naamini atabadilisha vitu vingi sababu hana affiliation zozote na yeyote aliyepo madarakani sio kma JPM mpaka leo alishindwa wadaka wezi wa Escrow ama EGMA kisa ni bureaucrats wake.

Mind you Lissu atataka kuprove a point ili ajizatiti madarakani na kuepuka kuwa one term President so lazima tu atafanya reform zote alizoahidi.

Pia historia yake ya uadilifu inambeba kma angekua fisadi au hana ufanisi tungemtilia shaka. Ila sababu taasisi zote alizopita kaacha impact then tuamini hawezi shindwa akiwa ikulu.

Kiufupi he'll improve alipoishia Magufuli ili asirudie makosa aliyopinga. Na usilinganishe na wapinzani wa huko Zambia ambao 90% walitoka CCM zao, ila Lissu ni pure opposition 100%
Umenipa hoja za hisia zaidi kuliko uhalisia wa mambo,ungenipa mfano wa nchi za Africa zilizopata maendeleo sababu ikawa ni mfumo wa majimbo.
Nikupe mfano mdogo tu wa kushindwa kwa Chadema kuongoza nchi kabla hata awajakabidhiwa.

Chama kilichopokea ruzuku ya chama na kuchangisha fedha wabunge kwa miaka 5 kinakosa ofisi nzuri ya makao makuu ya chama?

Kwanini Lissu mpenda haki kashindwa kupigania michango ya rambirambi za marehemu Mawazo wa Geita zilizolowa na Mbowr na swahiba wake Mrema?

Hivi bwashee kweli hazina ya fedha za nchi kweli ziwe chini ya Mbowe kama waziri mkuu kama mwenyewe anavyojitabiria?

Rasimali za nchi ziwe chini ya Lissu ambae hata aking'twa na mbu anasema kwa mabeberu,Lissu sindo atakuwa dalali wa mkubwa kugawa rasilimali za nchi yetu?
 
Hapa tu ndio mnashangaza, sasa kma mnajua ushindi ulikua obvious kulikua na haja gani ya kumfungia mtu kampeni, kuengua wagombea, kukataa kuapisha mawakala?
Hata upinzani uje na sera gani kma CCM mtaendelea kucheza rafu za uchaguzi basi tutegemee comment za namna hii kila mwaka.
Hakuna mgombea aliyefungiwa kufanya kampeni pasipo yeye kukiuka sheria na taratibu za uchaguzi.Unaapisha vp mawakala wasiokidhi vigezo?utakuwa unavunja sheria na kusababisha malumbano kwa vyama vingine.
Kifupi fuata taratibu wanazofuata wenzako,hutapata usumbufu huo.
Kumbuka adhabu unayopewa kwa kukiuka taratibu,ni haki kwa wenzako😄.Fuata sheria ili upate haki.
 
Umenipa hoja za hisia zaidi kuliko uhalisia wa mambo,ungenipa mfano wa nchi za Africa zilizopata maendeleo sababu ikawa ni mfumo wa majimbo.
Nikupe mfano mdogo tu wa kushindwa kwa Chadema kuongoza nchi kabla hata awajakabidhiwa.
Chama kilichopokea ruzuku ya chama na kuchangisha fedha wabunge kwa miaka 5 kinakosa ofisi nzuri ya makao makuu ya chama?
Kwanini Lissu mpenda haki kashindwa kupigania michango ya rambirambi za marehemu Mawazo wa Geita zilizolowa na Mbowr na swahiba wake Mrema?
Hivi bwashee kweli hazina ya fedha za nchi kweli ziwe chini ya Mbowe kama waziri mkuu kama mwenyewe anavyojitabiria?
Rasimali za nchi ziwe chini ya Lissu ambae hata aking'twa na mbu anasema kwa mabeberu,Lissu sindo atakuwa dalali wa mkubwa kugawa rasilimali za nchi yetu?
Devolution sio hisia ntakutumia hpa Pdf kuonyesha faida za devolution kenya kwenye kila kipengele kuanzia regional disparity, economic inclusion, econ growth... n.k
Kuhusu nchi zenye majimbo kufeli sio sababu ya majimbo ila unakuta ufanisi mdogo au ufisadi ila sio kwamba ile sera imefeli. But ukifanya everything right hku una mfumo wa majimbo, trust me maendeleo lazima yapae.

Hazina zipo chini ya watumishi watiifu ambao hawana chama. Sio kwamba Mbowe atakua governor wa BOT au katibu mkuu wa wizara ya fedha so tusichanganye utaalamu na siasa.

Pesa iliwekezwa kwenye CHADEMA ni msingi na nadhani umeona kanda zote zina ofisi za kisasa kuanzia ya kati hadi serengeti mpka kaskazini so hilo ndio lilikua lengo la miaka hii 5 kwamba CHADEMA iwekeze pesa zote kwa glassroots.
Nadhani pia uliona zile Pick up zilizonunuliwa pamoja na pikipiki kwa kila ofisi za kanda na mikoa ili kusaidia logistics. Kanda zimeimarishwa sana ndio maana mawakala wa vitup vyote na wagombea wa kata zote Tz walipatikana (Exclude zenji na Walioenguliwa).

Kwahiyo sio kweli kwamba hela zimepotea. Na ndio maana Lissu hakuna siku aliishiwa hela za kampeni toka anaanza otherwise tungehoji kuna wizi.

Rambirambi za mawazo ni porojo tu mbona zilikabidhiwa na lema mbele ya Tv. More so binti yake alichukuliwa kwenda kusomeshwa na huyo huyo Lema then hizi poroji zinatoka wapi?

Lissu akipewa uenyekiti (which is imminent) tutashuhudia reforms nyingi tu ndani ya chama. So usimhukumu kwa nafasi ya sheria tu ila mpime ssa ambapo ni vice wa Mbowe kma atafeli kitu.
 
Mbuzi kweli wewe.....
Watu tunatumia dedicated internet wewe unaongea upuuzi wa ufipa...
Alafu tuko tunahamasishana huku mitaani sasa wewe endelea hamasisha kwenye vpn...wakati luna pini..sijui unamhamasisha nani..
Bavicha mko nyuma sana aisee

Dedicated internet ndiyo hii inayokuwa kura za wizi kama zile za kawe au hizi za kwenye vifurushi au za chini ya miguu?

Kweli popoma litaendelea kuwa popoma tu.
 
Watanzania Twendeni tukamsulubu huyu msaliti wa Nchi kutoka Ubeligiji
Hiki ndicho kinachokwenda kutokea, Amiri Jeshi wetu Mkuu aliitangazia dunia, uchaguzi utakuwa huru na wa haki, amani itatawala, na mshindi ndiye atatangazwa mshindi!.
Hatuutaki ule uhuni wa watu fulani zile chaguzi za nyuma, mtu aliyeshindwa anajitangaza alishinda kura zake zikaibiwa!.
Safari hii ni anayashindwa akubali kushindwa na kumpongeza mshindi.
P
Teuzi hazipatikani kwa kupiga magoti.
 
Hiki ndicho kinachokwenda kutokea, Amiri Jeshi wetu Mkuu aliitangazia dunia, uchaguzi utakuwa huru na wa haki, amani itatawala, na mshindi ndiye atatangazwa mshindi!.
Hatuutaki ule uhuni wa watu fulani zile chaguzi za nyuma, mtu aliyeshindwa anajitangaza alishinda kura zake zikaibiwa!.
Safari hii ni anayashindwa akubali kushindwa na kumpongeza mshindi.
P
Hovyooo...eti nawe unajiita msomi....kafie mbali
 
Niko kituoni na washirika wenzangu muda sasa. Kimya kimya lakini hamasa kubwa moyoni.

Iziraeli atupishilie mbali.

Tunataka haki. Inshallah kutokana na haki amani hapa itatamalaki tu.

Sala zetu kote haki na ikatendeke tukiwakumbuka wale wote waliotutangulia kwa kusimama na haki.

Nimekuwa naangalia nyuzi mbali mbali tangia jana, hata huko kwenye mitandao mingine ambako bila VPN ni kweusi. Ma lb7, mataga na mshabiki nguli wa chama mboga mboga wote wamepotea.

Au labda hawataki kutumia VPN kuitikia mapenzi ya chama chetu? Au nao ni mshabiki wa hii mitandao kupotea ikibidi moja kwa moja?

Eeh mola wetu mshindi na akatangazwe mshindi.

Amani na ikawe na kila mpenda haki.

Tunayo siku ndefu leo inshallah.
Wewe hangaika na barabara ya Benako Lusahunga tu! Magu mshindi leo
 
Hiki ndicho kinachokwenda kutokea, Amiri Jeshi wetu Mkuu aliitangazia dunia, uchaguzi utakuwa huru na wa haki, amani itatawala, na mshindi ndiye atatangazwa mshindi!.
Hatuutaki ule uhuni wa watu fulani zile chaguzi za nyuma, mtu aliyeshindwa anajitangaza alishinda kura zake zikaibiwa!.
Safari hii ni anayashindwa akubali kushindwa na kumpongeza mshindi.
P
Najizuia sana kutamka lugha ambayo utaiona ni matusi kwako. Labda nikuulize, haya yanayoendelea sasa hivi nchi nzima kuanzia hapo Kawe wewe unayaona ni ya fahari kwa kujitangazia ushindi?
Binafsi sipendi violence lakini kwa yanayoendelea nikisikia Mkurugenzi mmoja kapigwa panga la kichwa sitahudhunika kamwe!
Hiyo itakuwa zawadi murua kwake
 
Niko kituoni na washirika wenzangu muda sasa. Kimya kimya lakini hamasa kubwa moyoni.

Iziraeli atupishilie mbali.

Tunataka haki. Inshallah kutokana na haki amani hapa itatamalaki tu.

Sala zetu kote haki na ikatendeke tukiwakumbuka wale wote waliotutangulia kwa kusimama na haki.

Nimekuwa naangalia nyuzi mbali mbali tangia jana, hata huko kwenye mitandao mingine ambako bila VPN ni kweusi. Ma lb7, mataga na mshabiki nguli wa chama mboga mboga wote wamepotea.

Au labda hawataki kutumia VPN kuitikia mapenzi ya chama chetu? Au nao ni mshabiki wa hii mitandao kupotea ikibidi moja kwa moja?

Eeh mola wetu mshindi na akatangazwe mshindi.

Amani na ikawe na kila mpenda haki.

Tunayo siku ndefu leo inshallah.
Mungu ndiye Mtetezi
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom