Wakivuta wao sigara, tukivuta sisi bangi!

Annina

JF-Expert Member
Nov 15, 2009
437
57
Miaka 2 iliyopita katika pitapita zangu maeneo ya sinza nilikutana na bango lenye ujumbe huu "wakivuta wao sigara, tukivuta sisi bangi". Ujumbe huu ulikuwa umebandikwa kwenye maskani ya vijana wa eneo hilo - maarufu kama kijiweni.

Leo nimeukumbuka usemi huu na nimeutafakari kidogo. Nimewakumbuka vijana wale wa kijiweni, ambao mara nyingi hakuna anaewapatiliza. Kwenye ujumbe huu wanaonekana kukata tamaa, hawaoni kama haki inatendeka na kwamba kuna matabaka ya "wao" na "sisi" - kwamba "wao" wakiiba kutoka hazina wanaombwa na kubembelezwa kurudisha walichoiba na kupongezwa kama vile ni mashujaa -maana ni "sigara", lakini "sisi" tukiiba kuku wa jirani kwa ajili ya kujikimu sheria inachukua mkondo wake maana ni "bangi"!

Wao wakisema uongo ulio dhahiri wanaitwa wanasiasa -sigara, sisi tukitoa maoni yetu tunaitwa wehu na kutakiwa kuthibitisha - bangi! Wao wakituingiza kwenye mikataba mibovu yenye dalili ya rushwa na kuliingiza taifa kwenye janga tunaambiwa ni vijisenti tu na pengine tunasumbuliwa na wivu wa kike - sisi tukichukua rushwa ya 5000/= tunaozea segerea!

Orodha ya wao na sisi ni ndefu... najiuliza kwa matabaka haya tunayoyajenga kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya tupo tayari kupokea matokeo yake?
 
Miaka 2 iliyopita katika pitapita zangu maeneo ya sinza nilikutana na bango lenye ujumbe huu "wakivuta wao sigara, tukivuta sisi bangi". Ujumbe huu ulikuwa umebandikwa kwenye maskani ya vijana wa eneo hilo - maarufu kama kijiweni.


Leo nimeukumbuka usemi huu na nimeutafakari kidogo. Nimewakumbuka vijana wale wa kijiweni, ambao mara nyingi hakuna anaewapatiliza. Kwenye ujumbe huu wanaonekana kukata tamaa, hawaoni kama haki inatendeka na kwamba kuna matabaka ya "wao" na "sisi" - kwamba "wao" wakiiba kutoka hazina wanaombwa na kubembelezwa kurudisha walichoiba na kupongezwa kama vile ni mashujaa -maana ni "sigara", lakini "sisi" tukiiba kuku wa jirani kwa ajili ya kujikimu sheria inachukua mkondo wake maana ni "bangi"!

Wao wakisema uongo ulio dhahiri wanaitwa wanasiasa -sigara, sisi tukitoa maoni yetu tunaitwa wehu na kutakiwa kuthibitisha - bangi! Wao wakituingiza kwenye mikataba mibovu yenye dalili ya rushwa na kuliingiza taifa kwenye janga tunaambiwa ni vijisenti tu na pengine tunasumbuliwa na wivu wa kike - sisi tukichukua rushwa ya 5000/= tunaozea segerea!

Orodha ya wao na sisi ni ndefu... najiuliza kwa matabaka haya tunayoyajenga kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya tupo tayari kupokea matokeo yake?

Hivi ile program ya tido mhando ya kumwanika juani raisi wetu ili tumuulize maswali bado ipo na itakuwa lini?
Swali hili itabidi ulili serve na kuuliza siku hiyo.Naogopa tu kwamba Tido ninaemjua atatayarisha program hizi tena 2010 karibu na uchaguzi! Anatafuta kumsafisha rafiki yake!
 
Mchukia fisadi,
asante, natamani ningejibiwa swali hili hata kwa njia ya hotuba za kila mwezi...
 
Hivi ile program ya tido mhando ya kumwanika juani raisi wetu ili tumuulize maswali bado ipo na itakuwa lini?
Swali hili itabidi ulili serve na kuuliza siku hiyo.Naogopa tu kwamba Tido ninaemjua atatayarisha program hizi tena 2010 karibu na uchaguzi! Anatafuta kumsafisha rafiki yake!
Hile sio really, huwa wana pre-filter maswali, na mengine huwa wanayatengeneza wao wenyewe.
Kuna mamluki huwa wanapiga simu kuonyesha kwamba ni live!
 
I have liked your version of sigara na bangi. Its true dat. Tabaka la wao na sisi bado ni kubwa sana miongoni mwa sisi Watanzania. Lakini wengi tunalazimika kwamba ndio mfumo halisi wa maisha yetu. Na jamii imeshajengwa kuamini hivyo. Yaani ukiwa kwenye madaraka makubwa, you can get away with anything and nobody will even complain. Just take a simple example ya kifo cha aliyekuwa makamu wa rais Dk. Omary Ally Juma. Runinga zilipoonyesha mandhari ya nyumbani kwake kule Zanzibar, watanzania wengi tulipigwa na butwaa. Kila mtu akawa anahoji, inakuwaje makamu wa rais anaishi maisha duni kiasi hicho? Wengi tulisahau kwamba huende huyu bwana alikuwa mwadilifu na alikuwa anaishi kwa kipato chake halali. Wengi tuliona kwamba si haki kwa kiongozi mkubwa kama yule wa nchi kuishi maisha ya chini kiasi kile. Mifano kama hii iko michache, lakini ipo. So, jamii imeshajijengea kwamba, ukiwa kwenye nafasi fulani kubwa, hasa serikalini, basi lazima uwe na maisha ya hali ya juu, hata kama hayaendani na kipato chako halali.
 
bangi na sigara yote ni jamii moja, hakuna yenye unafuu....stop smoking!
 
Hivi ile program ya tido mhando ya kumwanika juani raisi wetu ili tumuulize maswali bado ipo na itakuwa lini?
Swali hili itabidi ulili serve na kuuliza siku hiyo.Naogopa tu kwamba Tido ninaemjua atatayarisha program hizi tena 2010 karibu na uchaguzi! Anatafuta kumsafisha rafiki yake!
sikuwahi kuexperience CINSISTENCY kwenye uongozi wa awamu hii!huyu muheshimiwa ana mipango mingiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!mara nitahutubia wazee,mara hotuba,mara maswali mara hivi mara vile mara sijui nin!
smtmz MKAPA WAS GOOD BANA
 
Zero,
Umesema sawa, tatizo jamii inakuangalia kwa ulichonacho bila kujali umekipataje. Utu wa sasa ni kitu hata kama umeiba au kuua ili kupata ulichonacho. ndio maana kuna baadhi yetu linapokuja suala la pesa anaweza kumuuza hata mama yake mzazi mradi itamlipa
 
Hii inafanana na ule usemi wa kizaramo
kunya anye kuku,akinya bata kaharisha,,


ha ha ha sorry kwa nilio wa boa but ndo methali yenyewe.
 
Back
Top Bottom