Wakina mama: Chungeni sana kauli zenu

Wakina mama: Chungeni sana kauli zenu

Kuna jamaa yetu anatokea lile kabila la wababe,ambako wilaya tuu ni kanda maalum ya kipolisi, kwa sasa yuko jela

Alipewa kauli kama hzo, kilichofuata ni kumtenganisha yule mwanamke viungo vyote kwa panga, na aka jisalimisha polis mwenyew

Kwa kweli usipo kuwa mvumilivu unaweza kuta mnagawana majengo ya serikali, mmoja mochwari au hospital ,mmoja jela

Wanawake mbadilike kwa kweli na wanaume ukiambiwa kama hvo tuliza mzuka uskurupuke

Unifurahisha hapo pa kugawana majengo ya Serikali.! Mmoja mochwari mwingine gerezani...
 
Mpwa kwa jinsi ulivyoyatamka kwa ustadi hayo maneno inaonyesha...una uzoefu kwenye kuyatumia mara kwa mara....hongera....
Hapana,nimeyaona mengi Mkuu,kwanza mie akinza kunigombesha nalia,nikiona mdomo unazidi namsubiri atoke tuu,
nabeba wanagu kwetuu zogo siliwezi na Moyo wangu hauchukui tafrani hasa kugombana na mwanamme..
 
Ni kweli maneno kama hayo yanaumiza sana omba yasikukute! La muhimu ni kuwa na choice ya maneno unapoongea na mtu yeyote au mpenzi/mme.

Ila na wanaume ko na mipasho mpaka mtu anajuta kuolewa! Niliona kesi fulani mke na mme wamegombana hadi kutoana damu nilipouliza kisa, mke nini kilitokea akajibu kuwa mme alilala nje akarudi asubuhi mke alipouliza mme akamjibu "wewe ni nani kuniuliza maswali ya kijinga? Huyo mwanamke anakuhusu nn? Kwanza jione ulivyo na shape mbaya huna tofauti na mwanaume yakikushinda ondoka" hayo ndo majibu ya mwanaume. Mke alichukuwa kikombe paaaa usoni acha ugomvi uanze piganaaaa weee mwanaume kamung'ata mke mkono hadi nyama ikatoka. Ilikuwa ni kesi ya ajabu,

ushauri kwa wanaume sasa hivi kila mtu hukoo huru kijipimia! Ukiona mke unaetaka kumuoa hana shape unayoitaka muache coz naye ana type zake! Mnene na mwembamba vigezo na mashart kuzingatiwa.
 
Hata viongozi pia wachunge kauli zao....sisi tunatambua kauli za viongozi ni sheria/agizo/amri na tunamsaidia kutekeleza pale ambapo tunaona haitekelezwi.
 
Hizi Ndoa hizi......... Mlango wakuingilia kwenye hizi NDOA huwa unapambwa kwa maua, magari ya kifahari, farasi, bajeti kubwa kwenye kusherekea, vigelegele na vifijo kumbe ukishaingia unakutana na haya..... Basi sawa
 
Ninachojua ni kwamba, mwanamke hawezi kumtukana mwanaume bila sababu yoyote, mikwaruzano kwenye ndoa ipo ila inapofika mahali mmoja akazidiwa nguvu ndo hutumia madhaifu ya mwenzie kumuumiza na mara nyingi huwa ni ya kweli, nimeshawahi sikia kabisa mwanaume anamwambia mkewe ndo maana mamako alishindwa kuishi na mwanaume mmoja mimi ndo nitakuweza wewe??? Na hiyo ilikuwa ni kweli kabisa, sema yule baba alikuwa kashaonja kidogo. Kwa hiyo hayo maswala ya kauli yapo kwa pande zote mbili
 
Hapana,nimeyaona mengi Mkuu,kwanza mie akinza kunigombesha nalia,nikiona mdomo unazidi namsubiri atoke tuu,
nabeba wanagu kwetuu zogo siliwezi na Moyo wangu hauchukui tafrani hasa kugombana na mwanamme..

Pole sana mpwa....lakini wajukuu hawajambo....???
 
mwanamke anaebishana na mme wake au kumtolea maneno machafu ya dhihaka uyo hana hekima na kwao akufundishwa kua na heshima kwa mme wake.Dawa ni kumrudisha kwao wakamfundishe heshima.
Mkuu....
Yaani siku yakikukuta ndipo utakuja ujue kwamba maharage ni mboga ya serikani. Maana ukimwambia aende kwao, yeye anageuza njia na utasikia yupo kwenu.
Agghhhh.....
Ebu ngoja nijinyamazie tu mie..[emoji25]
 
Kuna wanawake ambao ni unbearable kabisa. Wanaongea ovyo, maneno machafu na hawana staha hata kidogo. Mimi nawalaumu hao wanaume kwa kukubali kuishi na watu waropokaji, lakini pia nawahurumia sana.

Kuishi na mtu asiye na break ya maneno, mtu ambaye hajui aongee nini, wapi na nani hafai kabisa. Nimeshuhudia sehemu fulani,I almost ran away. Unajuiliza, hivi huyu alilelewa na nani, nani ataweza kuishi nae, lakini ajabu anapata mtu "sahihi" kwake. Mpwa umesema jambo la maana sana.
 
Wanawake wa miaka hii wengi wako hivyo mkigombana anakimbilia kwa wazazi wake anadhani wao hawagombani na hata midomo yao haina break anaweza tamka lolote kwa wakati wowote na mahali popote
 
mwanamke anaebishana na mme wake au kumtolea maneno machafu ya dhihaka uyo hana hekima na kwao akufundishwa kua na heshima kwa mme wake.Dawa ni kumrudisha kwao wakamfundishe heshima.
Kwani mpk anakupa hayo maneno kaanza tu kama kichaa, unachochea moto halafu unalaumu joto[emoji2] [emoji2] [emoji2] .
mwanamke anaebishana na mme wake au kumtolea maneno machafu ya dhihaka uyo hana hekima na kwao akufundishwa kua na heshima kwa mme wake.Dawa ni kumrudisha kwao wakamfundishe heshima.
 
Kuna wakati mwengine hao wanaume nao ndio wanaanza wanakufanya uchefukwe na roho,mfano unaweza kukuta sms au mwanamke anakutumia sms kwenye cm yako na kukutukana au umefumani na sms ukimuliza anakwambia humfiki kwa lolote huyu mwanamke na wewe sinimekuo hiyo basi tuu,mwanamke utakua wewe? sasa hapo jamani mwanamke hakutolewa nyongo lazima akawambia na "na wewe sinakustahmilia tuu service mbovu hata huyo malkia anakulia pesa yako
lakini mbele huchezi nyuma hutisiki ebu nipishe mie kwenye wanaume nawewe unajiita mwanamme eeh? ebu nyamaza nikustiri babu weeeeeeeeeee.." lol
Hapo bora tugawane majengo ya serikali, sina roho ya kutunza hayo maneno
 
Habari za wakati huu ndugu zangu.....natumaini sote tu wazima na baadhi waliopungukiwa uzima Mungu atawasaidia........

Kila mmoja wetu anafahamu ni jinsi gani ndoa zilivyojaa changamoto na mahangaiko mengi yanayozifanya ndoa kuwa ni muunganiko mgumu sana kuuingia......pengine wewe hapo msomaji unashughulikia moja ya changamoto hizo muda huu.....

Wakati mwingine mikiki mikiki ya ndoa hupelekea wanandoa kutofautiana kauli....utofauti unaowafanya wanandoa warushiane maneno.....na hapa ndipo hasa paliponifanya nitoe duku duku.....kwani hawa ndugu zetu sijui huwa wanakumbwa na ibilisi gani kwa muda huo kwani huwa hawachagui neno la kusema ilimradi tu liwe lenye kukuumiza wewe unayejibishana naye........

Ni maneno ambayo huamsha upya ugomvi na migogoro kila yakikumbukwa na yule aliyeambiwa....kwani ni mazito mmo na yanafedhehesha.....mfano; mwanamke anaweza akakuambia mbele ya kadamnasi kuwa..." Eti katika wanaume nawe ni mwanaume, umebakiwa kuvaa magauni tu" hii ni kauli mbaya sana na yenye kufedhehesha kama sio kudhalilisha...... Utasikia " kwanza hawa watoto sio wa kwako".........hizi ni baadhi ya kauli zinazolisha mengine kwani ni wanaume wachache wenye uwezo wa kuhimili kuziacha hizi kauli zipite hivi hivi ingawa zinachoma kama mtu aliyemeza kaa la moto......

Ndio maana matukio ya kuuwawa wanawake kinyama yanashamiri kila uchao....wanawake wanaopata ulemavu kutokana na vipigo vya waume zao wanaongezeka kila uchao.....ukichunguza kwa makini chanzo ni kauli mbovu za wanawake.......sio kwamba naunga mkono matukio ya ukatili wa kijinsia la hasha bali nawaasa wakina mama wawe makini na kila wakitoacho mdomoni mwao.....kwani bila ya kujua huleta matokeo mabaya sana.....kwani si kila mtu ana uwezo wa kustahimili kauli za kizalilishaji kama hizo.....kuna wale wanaume mashujaa wanaoweza kufunika kombe ili mwanaharamu apite na kuna baadhi wanaoonyesha hasira zao....hapo ndipo matokeo ya kauli chafu yanavyoonekana..........

N;B
WANAMUME WENZANGU TUJITAHIDI KUWA WASTAHILIMILIVU KATIKA NDOA KWANI KWA KUISHI NA MWANAMKE NI MTIHANI MKUBWA AMBAO MUNGU AMETUPA.......

Inapotokea umepishana kauli na mkeo usikae eneo.....ondoka uende mbali na eneo hilo lakini usiende bar kunywa pombe......

HUU UZI UAMBATANE NA PICHA TAFADHALI MKUU!
 
Ukitaka kushinda vita ya maneno na mwanamke hilo usahau ndugu yangu KikulachoChako hawa viumbe hujihisi kila mara wanaonewa sasa tahadhari ya kwanza ni kutoruhusu vita ya maneno.Sisemi tusijadiliane nao la hasha kuna mwisho wa mjadala kisha inaanza vita nae atajaribu kutumia silaha hiyo aone kama itakuumiza huenda mbali na kukwambia hata hawa watoto sio wako ilhali ni wa kwako ila anataka uumie si mpo vitani.
hakuna kitu kinauama kama kutukanana na mwanamke,mimi nilishasema siwez kuweka battle ya maneno na mwanamke baada ya kuzalilishwa mbele za watu na mwanamke mmoja(though niliishia kumvimbisha domo ikawa kesi).naavoid sana hcho kitu,sometimes nikiona vita inataka kuanza nakaa kimya sijibu kitu.
 
Ushimen na wewe pia ni miongoni mwao
Ukirudi talaka yako ipo mezaniiii…(kidding)
Sijui kwanini nimefungua huu uzi aiseeee....
Nimejikuta nakumbuka neno ambalo nilikua nikilitumia sana (nahitaji private time).
Lakini chakushangaza ndipo ilikua kama nachochea kuni kwenye kijinga cha moto agghhhh...[emoji16]
Niliposema nitoke, basi nilifuatiwa na SMS, MMS za maneno na matusi kama mvua......
Mwisho nikaona nitafute pakua napata pumziko aiseeee.....
Ebu ngoja niishie hapa maana nahisi mapigo moyo kuanza kunienda kwa kasi
k
 
Back
Top Bottom