KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,883
- 40,053
Habari za wakati huu ndugu zangu.....natumaini sote tu wazima na baadhi waliopungukiwa uzima Mungu atawasaidia........
Kila mmoja wetu anafahamu ni jinsi gani ndoa zilivyojaa changamoto na mahangaiko mengi yanayozifanya ndoa kuwa ni muunganiko mgumu sana kuuingia......pengine wewe hapo msomaji unashughulikia moja ya changamoto hizo muda huu.....
Wakati mwingine mikiki mikiki ya ndoa hupelekea wanandoa kutofautiana kauli....utofauti unaowafanya wanandoa warushiane maneno.....na hapa ndipo hasa paliponifanya nitoe duku duku.....kwani hawa ndugu zetu sijui huwa wanakumbwa na ibilisi gani kwa muda huo kwani huwa hawachagui neno la kusema ilimradi tu liwe lenye kukuumiza wewe unayejibishana naye........
Ni maneno ambayo huamsha upya ugomvi na migogoro kila yakikumbukwa na yule aliyeambiwa....kwani ni mazito mmo na yanafedhehesha.....mfano; mwanamke anaweza akakuambia mbele ya kadamnasi kuwa..." Eti katika wanaume nawe ni mwanaume, umebakiwa kuvaa magauni tu" hii ni kauli mbaya sana na yenye kufedhehesha kama sio kudhalilisha...... Utasikia " kwanza hawa watoto sio wa kwako".........hizi ni baadhi ya kauli zinazolisha mengine kwani ni wanaume wachache wenye uwezo wa kuhimili kuziacha hizi kauli zipite hivi hivi ingawa zinachoma kama mtu aliyemeza kaa la moto......
Ndio maana matukio ya kuuwawa wanawake kinyama yanashamiri kila uchao....wanawake wanaopata ulemavu kutokana na vipigo vya waume zao wanaongezeka kila uchao.....ukichunguza kwa makini chanzo ni kauli mbovu za wanawake.......sio kwamba naunga mkono matukio ya ukatili wa kijinsia la hasha bali nawaasa wakina mama wawe makini na kila wakitoacho mdomoni mwao.....kwani bila ya kujua huleta matokeo mabaya sana.....kwani si kila mtu ana uwezo wa kustahimili kauli za kizalilishaji kama hizo.....kuna wale wanaume mashujaa wanaoweza kufunika kombe ili mwanaharamu apite na kuna baadhi wanaoonyesha hasira zao....hapo ndipo matokeo ya kauli chafu yanavyoonekana..........
N;B
WANAMUME WENZANGU TUJITAHIDI KUWA WASTAHILIMILIVU KATIKA NDOA KWANI KWA KUISHI NA MWANAMKE NI MTIHANI MKUBWA AMBAO MUNGU AMETUPA.......
Inapotokea umepishana kauli na mkeo usikae eneo.....ondoka uende mbali na eneo hilo lakini usiende bar kunywa pombe......
Kila mmoja wetu anafahamu ni jinsi gani ndoa zilivyojaa changamoto na mahangaiko mengi yanayozifanya ndoa kuwa ni muunganiko mgumu sana kuuingia......pengine wewe hapo msomaji unashughulikia moja ya changamoto hizo muda huu.....
Wakati mwingine mikiki mikiki ya ndoa hupelekea wanandoa kutofautiana kauli....utofauti unaowafanya wanandoa warushiane maneno.....na hapa ndipo hasa paliponifanya nitoe duku duku.....kwani hawa ndugu zetu sijui huwa wanakumbwa na ibilisi gani kwa muda huo kwani huwa hawachagui neno la kusema ilimradi tu liwe lenye kukuumiza wewe unayejibishana naye........
Ni maneno ambayo huamsha upya ugomvi na migogoro kila yakikumbukwa na yule aliyeambiwa....kwani ni mazito mmo na yanafedhehesha.....mfano; mwanamke anaweza akakuambia mbele ya kadamnasi kuwa..." Eti katika wanaume nawe ni mwanaume, umebakiwa kuvaa magauni tu" hii ni kauli mbaya sana na yenye kufedhehesha kama sio kudhalilisha...... Utasikia " kwanza hawa watoto sio wa kwako".........hizi ni baadhi ya kauli zinazolisha mengine kwani ni wanaume wachache wenye uwezo wa kuhimili kuziacha hizi kauli zipite hivi hivi ingawa zinachoma kama mtu aliyemeza kaa la moto......
Ndio maana matukio ya kuuwawa wanawake kinyama yanashamiri kila uchao....wanawake wanaopata ulemavu kutokana na vipigo vya waume zao wanaongezeka kila uchao.....ukichunguza kwa makini chanzo ni kauli mbovu za wanawake.......sio kwamba naunga mkono matukio ya ukatili wa kijinsia la hasha bali nawaasa wakina mama wawe makini na kila wakitoacho mdomoni mwao.....kwani bila ya kujua huleta matokeo mabaya sana.....kwani si kila mtu ana uwezo wa kustahimili kauli za kizalilishaji kama hizo.....kuna wale wanaume mashujaa wanaoweza kufunika kombe ili mwanaharamu apite na kuna baadhi wanaoonyesha hasira zao....hapo ndipo matokeo ya kauli chafu yanavyoonekana..........
N;B
WANAMUME WENZANGU TUJITAHIDI KUWA WASTAHILIMILIVU KATIKA NDOA KWANI KWA KUISHI NA MWANAMKE NI MTIHANI MKUBWA AMBAO MUNGU AMETUPA.......
Inapotokea umepishana kauli na mkeo usikae eneo.....ondoka uende mbali na eneo hilo lakini usiende bar kunywa pombe......