Wakili Albert Msando ashikiliwa na Polisi baada ya kutoa taarifa ya hali ya maambukizi ya Corona na kuhamasisha waandishi kuandika ukweli

Wakili Albert Msando ashikiliwa na Polisi baada ya kutoa taarifa ya hali ya maambukizi ya Corona na kuhamasisha waandishi kuandika ukweli

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Koka Moita amesema Alberto Msando ameitwa kwa ajili ya Mahojiano ila ni mapema sana kusema ni mahojiano yanayohusu nini kwani hana taarifa kamili

Alipoulizwa kama kushikiliwa kwa Wakili Msando kunahusisha yale aliyoongea jana wakati wakati akikabidhi vifaa ya kujikinga na #COVID19, amesema hasema hana taarifa kamili na suala hiyo halijakaa sawa kuzungumzia

Aidha, amethibitisha kuwa Wakili Msando ameitwa Polisi kwa mdomo kama ambavyo alitumia yeye alitumia kuzungumza, na kuwa hakuna nguvu iliyotumika

Kamanda Moita amesema, “Kama ambavyo alitumia mdomo kuzungumza, na kuja Polisi pia imetumika kauli ya kumuita.” Amesema pia mahojiano yakikamilika atatoa taarifa

Jana wakati akigawa vifaa hivyo alisema “Ni kweli na niseme bila kuficha hali ni mbaya, kwa Arusha hali ni mbaya. Ndugu lazima mfike mahali muweke mguu chini mseme ukweli ili Wananchi, Serikali na kila anayehusika atambue tupo katika hali mbaya ambayo kila mmoja wetu anapaswa kuchukua hatua.”

Aliongeza, “Mkirudi nyuma na kuogopa kusema, tutazikana. Hii ndio nafasi yenu, tusipozungumza, msipo andika na kusema ngoja tutoke tukatafute ukweli na tuuseme, basi huu ugonjwa hautaondoka kirahisi.”


Pia soma: Albert Msando ‘amwaga’ vifaa vya Corona kwa wanahabari Arusha, adai hali ni mbaya sana - JamiiForums


Wanatuzuga tu ionekane kila mtu anaweza kukamatwa. Wamemuita wakanywe chai na kupiga nyungu.
 
Yaani hawa. Tatizo wanatuona sisi wananchi wajinga. Sasa mtu kusema Arusha Arusha ugonjwa umesambaa kuna kosa gani ?
Nafikiri sisi ni wajing ...., Sio wanatuona , maana yy Katoa maoni yake ambayo kikatiba anaruhussiwa
 
Screenshot_20200430-003836-1.jpg
 
Boss Return Of Undertaker Tunasikilizia ya Dj ......

Kamata Kamata ....



Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Koka Moita amesema Alberto Msando ameitwa kwa ajili ya Mahojiano ila ni mapema sana kusema ni mahojiano yanayohusu nini kwani hana taarifa kamili

Alipoulizwa kama kushikiliwa kwa Wakili Msando kunahusisha yale aliyoongea jana wakati wakati akikabidhi vifaa ya kujikinga na #COVID19, amesema hasema hana taarifa kamili na suala hiyo halijakaa sawa kuzungumzia

Aidha, amethibitisha kuwa Wakili Msando ameitwa Polisi kwa mdomo kama ambavyo alitumia yeye alitumia kuzungumza, na kuwa hakuna nguvu iliyotumika

Kamanda Moita amesema, “Kama ambavyo alitumia mdomo kuzungumza, na kuja Polisi pia imetumika kauli ya kumuita.” Amesema pia mahojiano yakikamilika atatoa taarifa

Jana wakati akigawa vifaa hivyo alisema “Ni kweli na niseme bila kuficha hali ni mbaya, kwa Arusha hali ni mbaya. Ndugu lazima mfike mahali muweke mguu chini mseme ukweli ili Wananchi, Serikali na kila anayehusika atambue tupo katika hali mbaya ambayo kila mmoja wetu anapaswa kuchukua hatua.”

Aliongeza, “Mkirudi nyuma na kuogopa kusema, tutazikana. Hii ndio nafasi yenu, tusipozungumza, msipo andika na kusema ngoja tutoke tukatafute ukweli na tuuseme, basi huu ugonjwa hautaondoka kirahisi.”


Pia soma: Albert Msando ‘amwaga’ vifaa vya Corona kwa wanahabari Arusha, adai hali ni mbaya sana - JamiiForums

 
Tego hilo, jamani ukiingia head head imekula kwako.

Kumbuka mwanaCCM kaitwa kuhojiwa kuhusu kauli yake "presumably" sasa nyie CHADOMO mlivyo na kiramga mkiitwa kistaarabu hivyo mtagoma na hapo ndipo mnapotoa mwanya wa yale Mambo yetu kutumika, kisha mnakuja huku jamii forums na kuanza kubwata sijui policcm sijui matakataka gani.

Sent using Jamii Forums mobile app
CHADOMO duh!😂😂😂

Mindset katika "PRIMITIVE domain" inafikirisha sana. Hivi hawa jamaa zinawatosha? No wonder zile data za Yericko kuhusu percentage kubwa ya WAJINGA SANA waliopo. Inatisha
 
Huu ni ujinga wa kupitiliza
Mtakamata wangapi?
Kwa nini mnaficha takwimu inawasaidia nini?
Msando jamaa zako hao umenaswa ulikuwa mstari wa mbele kuwasimanga Chadema
Tukisema kijani ni lost case muwe mnaelewa
Pole kwa maswahibu wakili naniliii
Umeeleza jambo zuri kwa lugha yenye ukakasi.
Covid-19 haina itikadi, na kinachotakiwa ni kuongea kama alivyofanya Wakili Msando na Mwenyekiti Freeman Mbowe.
Spika Ndugai anatakiwa azinduke na kutoa agizo Wabunge wote wachukuliwe vipimo ili walioambukizwa wawekwe karantini.
Kama hili lingefanyika mapema, labda Mama Rwakatare na Mhe. Ndassa wangekuwa bado wako hai.
Waziri Mkuu naye atoe agizo Viongozi wote wa Kiserikali wapimwe kutokana na shughuli zao za kukutana na watu.
Viongozi wa dini zote hali kadhalika.
Uhai wetu ni kila kitu na ni zaidi ya itikadi za vyama.
Hiki ni kipindi muafaka cha kupima UZALENDO WA KWELI.
Tusipuuze janga hili.
Mdharau mwiba, guu huota tende.
 
Alafu mwisho wa siku atakuja kuipigia ccm kampeni,alikubali kuingia katika ukoo wa panya kusifiasifia kila kitu.

Ukienda tofauti ndiyo hivyo.
 
ukiangalia vizuri kwa jicho la2 utaona kabisa msando si target yao, yule aliyeongea jana haswa ndiye wanaye mtafuta...
 
Back
Top Bottom