Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,563
- 7,321
Hii wiki wakenya wameandamana na kutishia vurugu baada ya wanaharakati wa Kenya kukamatwa na wengine kufukuzwa Tanzania hivi majuzi kwa sababu ya kutaka kuhudhuria kesi ya Tundu Lissu.
Baada serikali ya Kenya kuimarisha ulinzi katika ubalozi wa Tanzania jijini Nairobi, Wakenya wengi wameshangazwa Ofisi za Balozi za Tanzania kuwa katikati maeneo ya kibiashara (CBD - Central Business District) tena ikiwa imekodi vyumba kwenye jengo la kibiashara la Java House au jina lingine ni Reinsurance Plaza katika Ghorofa ya 9, katika barabara ya Taifa (Taifa Road), Jengo ambalo lina ofisi nyingi za kibiashara. Ukilinganisha na Balozi nyingi zilizo na majengo yake Binafsi katika mitaa kama Runda, Gigiri, Riverside Drive, Lavington, Upper Hill na mingineyo.
Wakenya wanahisi hatukupaswa kukodi vyumba kwenye jengo la kibiashara badala yake tulipaswa kuwa na Jengo letu la ubalozi wetu
Baada serikali ya Kenya kuimarisha ulinzi katika ubalozi wa Tanzania jijini Nairobi, Wakenya wengi wameshangazwa Ofisi za Balozi za Tanzania kuwa katikati maeneo ya kibiashara (CBD - Central Business District) tena ikiwa imekodi vyumba kwenye jengo la kibiashara la Java House au jina lingine ni Reinsurance Plaza katika Ghorofa ya 9, katika barabara ya Taifa (Taifa Road), Jengo ambalo lina ofisi nyingi za kibiashara. Ukilinganisha na Balozi nyingi zilizo na majengo yake Binafsi katika mitaa kama Runda, Gigiri, Riverside Drive, Lavington, Upper Hill na mingineyo.
Wakenya wanahisi hatukupaswa kukodi vyumba kwenye jengo la kibiashara badala yake tulipaswa kuwa na Jengo letu la ubalozi wetu