Wakazi wa Itumbi Chunya tunahitaji lami

Itumbi nimefika, watu binafsi wamejitahidi sana kupaendeleza. Mahitaji muhimu yapo na kila aina ya biashara ipo utadhani upo Mwanjelwa. Wana Itumbi wakipatiwa huduma muhimu za kijamii wanaweza kuipiku Matundasi au hata Makongolosi.

Vuteni subira maana kwa Tanzania wanatangulia watu kuishi mahali, maendeleo yanawafuata baadaye. Ilipaswa yatangulie maendeleo ya huduma za msingi, hasa miundombinu ndipo waingie watu.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
Kuipiku Makongolosi sizani. Labda Watu wa Makongolosi wawe wamebweteka.
 
kuleni vumbi kwanza huku mkishangilia TOZO ili tuwajengee lami mwakani... hakuna kitu chepesi chepesi hapa duniani.
 
Mkuu tusubiri kwanza barabara ya kutoka Mbalizi,mkwajuni mpaka saza kwanza halafu tutaiangalia na hiyo
Huko pia ni tatizo maana eneo hilo pia lina mashamba mengi sana ya dhahabu ukiachia mbali plantation kubwa ya dhahabu ya mwekezaji Shanta hapo Saza Mkwajuni kwa kweli nakuunga mkono ianze hii kisha ifuate ya Itumbi hii ni muhimu zaidi kwa sababu inaunganisha Mbeya na Wilaya ya Chunya na Mkwajuni ambako pia kunalimwa dhahabu nyingi sana
 
Itumbi ilistahili kupatiwa umeme wa TANESCO tangu miaka 15 iliyopita.
Wamechelewesha sana, hicho kijiji kingekuwa mbali sana kimaendeleo sasa ivi.
Kuna mwekezaji hapa anaitwa APEX analima dhahabu ya kutosha tena kwa teknolojia rafiki isiyotumia zebaki lakini anapoteza tija pakubwa kwa kutumia dizeli nyingi kuwasha majenereta 24/7 ili azalishe....waharakishe umeme hawa TANESCO ili huu mji uongeze tija kwa uchumi
 
Back
Top Bottom