Wakati nikiwa Sekondari nilikuwa kijana mpole na mwenye heshima sana

Mkulungwa01

JF-Expert Member
Jul 14, 2021
3,979
5,295
Mshana Jr natambua uwepo wako kaka yangu, na wote wana-JF.

Wakati nikiwa secondary nilikuwa kijana mpole na mwenye heshima sana kwa kila mtu(japokuwa mpaka sasa nina heshima), ilikuwa kama ni kula nikose mimi mwingine ale, nilikuwa jalala la kila mtu aliyejisikia kutoa matani yake(hata yale ya kumdhalilisha mtu).

Nimeishi maisha haya sana, nilikuwa muoga, na nilipenda kumfurahisha kila mtu, marafiki, jamaa na ndugu. Wanafunzi wenzangu wengi walikuwa wakinibeza na kunikejeli, hata wale ambao walikuwa wadogo kwangu walifanya hivyo.

Niliamini ndio ilikuwa njia nzuri ya kujichanganya na kuishi vema na watu, niliamini nisipokuwa hivyo basi siku nikipata shida nisingepata msaada kwa watu, niliamini siwezi kusimama peke yangu bila " 'kampani' ya watu.

Nilidhulumiwa, nilionewa na kusemwa vibaya kwa vitu ambavyo sikustahili kufanyiwa hivyo. Na sasa nipo chuo kikuu, hata sijui kwa nini nimekuwa 'mkaksi' na naogopwa kiasi hiki, baadhi ya watu wananisema pembeni kuwa sitaki kushirikiana na wenzangu, kuchangamana, sitaki utani n.k.

Sasa nimekuwa katili(kwenye vitu vya kipuuzi), sina huruma za kipuuzi, najipenda, najijali mimi kwanza, ninajiheshimu, sina utani na mazoea ya hovyo na pia ninatambua ninachokifanya. NAFURAHI KUOGOPWA NA KUWA KATILI, BORA KUWA 'MKAKSI' NA KATILI.
 
Mshana Jr natambua uwepo wako kaka yangu, na wote wana-JF.
Ishi maisha yako mkuu.

Sio lazima kila mtu akutanie na akuzowee,haya ndo maisha tunayoishi sisi kaka zako.

Kuna watu ukikaa nao unakuwa comfortable unapiga nao stori,unakuwa mcheshi unafurahi nao alafu hawa unaocheka nao ndio wanaenda kukutetea kwa watu wengine kwamba mbona kaka safuher hana shida tunapiga nae stori sana na ni mcheshi ?

Yaani ukiishi hivyo unapata watetezi wa kukusemea wakati wewe haupo,na wanakusemea bila kuwatuma.

Usijitenge na kila mtu tu,kuwa na watu wako kwwmba ukiwa nao unakuwa comfotabo mnacheka mnafurahi.

Usiwe comfortable na kila mtu.
 
Mshana Jr natambua uwepo wako kaka yangu, na wote wana-JF.

Wakati nikiwa secondary nilikuwa kijana mpole na mwenye heshima sana kwa kila mtu(japokuwa mpaka sasa nina heshima), ilikuwa kama ni kula nikose mimi mwingine ale, nilikuwa jalala la kila mtu aliyejisikia kutoa matani yake(hata yale ya kumdhalilisha mtu).
Kiuhalisia makuzi ndio yamekubadili na kuwa wewe wa leo na si yule wa jana ...ukiweza sasa balance hulka hizo mbili utoke na moja itakayokuwa roadmap yako mbeleni
Penye kustahili huruma fanya huruma
Penye kustahili ubabe fanya ubabe
Penye kustahili msaada toa msaada
Penye kustahili msimamo onesha wazi
Nknk
 
Mshana Jr natambua uwepo wako kaka yangu, na wote wana-JF.

Wakati nikiwa secondary nilikuwa kijana mpole na mwenye heshima sana kwa kila mtu(japokuwa mpaka sasa nina heshima), ilikuwa kama ni kula nikose mimi mwingine ale, nilikuwa jalala la kila mtu aliyejisikia kutoa matani yake(hata yale ya kumdhalilisha mtu).
Huu ni ujinga mfanyie mwanao ukatili utajuta uzeeni.

This is a learning issue make a U-turn
 
Kiuhalisia makuzi ndio yamekubadili na kuwa wewe wa leo na si yule wa jana ...ukiweza sasa balance hulka hizo mbili utoke na moja itakayokuwa roadmap yako mbeleni
Penye kustahili huruma fanya huruma
Penye kustahili ubabe fanya ubabe
Penye kustahili msaada toa msaada
Penye kustahili msimamo onesha wazi
Nknk
Shukrani kaka!
 
Bottomline hata maisha bado hujaanza kuishi..
Secondary na chuo most probably watu wako so genuine
Kuliko mtaani ambapo watu wanasimama kwenye ugali na sio kwenye haki..

Bado utajifunza sana zaidi ya hapo
Shukrani kaka!
 
Bottomline hata maisha bado hujaanza kuishi..
Secondary na chuo most probably watu wako so genuine
Kuliko mtaani ambapo watu wanasimama kwenye ugali na sio kwenye haki..

Bado utajifunza sana zaidi ya hapo
Tupeni nondo wadogo zenu sasa!
 
Changamoto(kiasi fulani) hutujenga,lakini changamoto zikizidi hutubadilisha katika namna hasi sana,hasa kama tunakosa mwongozo wa busara wa kuturudisha relini.

Angalia watu waliopitia maisha magumu sana,waliopitia kutendwa sana,waliopitia kunyanyaswa sana,waliopitia ukatili wa hali ya juu..wengi huishia kuwa na attitude ambazo sio nzuri.

Yatupasa kujifunza zaidi kuhusu changamoto tunazopitia na madhara yake,tutaweza kujifunza vyanzo vyake na namna ya ku'cope' nazo ili turudi kwenye mstari.
 
Huu ni ujinga mfanyie mwanao ukatili utajuta uzeeni.

This is a learning issue make a U-turn
Aliyekwambia sikuizi tunazeeka Nani mtoto wako mfundishe vitu vya msingi hasa msimamo na msimamo ni hasa katika makuzi yake mtoto akikosea mkanye tena Kwa kiboko aelewe ilo ni kosa asomee hiyo siyo ombi kwamba umdekeze yeye kusoma Baba asiye na misimamo ata mke anaweza kukutukana mbele ya mwanao na ukaona kawaida sababu ya ujingaa wa kujifanya unawatreat watoto vizuri wakuone wewe mwema Ila badaye waje wakusifie kwenye mitandao Kuwa hakuna kama Baba boy njia ya mwanaume ni mateso jitengenezee kesho yako mwenyewe bila kuangalia wanao watakuwa nn mbeleni
 
Mshana Jr natambua uwepo wako kaka yangu, na wote wana-JF.

Wakati nikiwa secondary nilikuwa kijana mpole na mwenye heshima sana kwa kila mtu(japokuwa mpaka sasa nina heshima), ilikuwa kama ni kula nikose mimi mwingine ale, nilikuwa jalala la kila mtu aliyejisikia kutoa matani yake(hata yale ya kumdhalilisha mtu).

Nimeishi maisha haya sana, nilikuwa muoga, na nilipenda kumfurahisha kila mtu, marafiki, jamaa na ndugu. Wanafunzi wenzangu wengi walikuwa wakinibeza na kunikejeli, hata wale ambao walikuwa wadogo kwangu walifanya hivyo.

Niliamini ndio ilikuwa njia nzuri ya kujichanganya na kuishi vema na watu, niliamini nisipokuwa hivyo basi siku nikipata shida nisingepata msaada kwa watu, niliamini siwezi kusimama peke yangu bila "
'kampani' ya watu.

Nilidhulumiwa, nilionewa na kusemwa vibaya kwa vitu ambavyo sikustahili kufanyiwa hivyo. Na sasa nipo chuo kikuu, hata sijui kwa nini nimekuwa 'mkaksi' na naogopwa kiasi hiki, baadhi ya watu wananisema pembeni kuwa sitaki kushirikiana na wenzangu, kuchangamana, sitaki utani n.k.

Sasa nimekuwa katili(kwenye vitu vya kipuuzi), sina huruma za kipuuzi, najipenda, najijali mimi kwanza, ninajiheshimu, sina utani na mazoea ya hovyo na pia ninatambua ninachokifanya. NAFURAHI KUOGOPWA NA KUWA KATILI, BORA KUWA 'MKAKSI' NA KATILI.
You are Introvent. Lakin pia Umekua hivyo kutokana na abuse ulizo experience shule
 
Aliyekwambia sikuizi tunazeeka Nani mtoto wako mfundishe vitu vya msingi hasa msimamo na msimamo ni hasa katika makuzi yake mtoto akikosea mkanye tena Kwa kiboko aelewe ilo ni kosa asomee hiyo siyo ombi kwamba umdekeze yeye kusoma Baba asiye na misimamo ata mke anaweza kukutukana mbele ya mwanao na ukaona kawaida sababu ya ujingaa wa kujifanya unawatreat watoto vizuri wakuone wewe mwema Ila badaye waje wakusifie kwenye mitandao Kuwa hakuna kama Baba boy njia ya mwanaume ni mateso jitengenezee kesho yako mwenyewe bila kuangalia wanao watakuwa nn mbeleni
Mtoto mchape saaana ila jua muda wa.kumtreat good

Usimfanyie ukatili "traumatize" utajuta

Biblia inasema "Mit 23:13

Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa."

Mit 22:15 SUV

Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali
 
Back
Top Bottom