Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 11,549
- 7,487
Habari ya mwaka mpya waungwana.
Nimekuwa nikitatizwa sana na hili jambo,naombeni wenye uelewa wanisaididie ili na wengine wenye interest ya kujua wanufaike.
Nataka kujua,ile "tochi" ya matrafiki wa barabarani inatumia principle gani kudetect speed ya gari.Je ni image ya ile moving object(gari) au change in sound frequency ya object towards an observer (ile tochi)? Au ni nini hasa?
Haiwezi kuwa doppler effect kwa sababu gari zinaweza kufika kwenye eneo la proximity ya camera hata zikiwa zaidi ya mbili au tatu. Doppler effect inashughulika na sauti ya kitu, hivyo katika mazingira kama hayo sidhani kama hizo kamera ziko sophisticated kiasi hicho cha kuwa na uwezo wa kuchanganua frequencies za object tofauti tofauti na hatimaye kuweza ku-judge kuwa hii frequency ni ya gari hii na siyo ya ile. Sababu gari zote zaweza kuwa hata Yutong 4, mbili zime-overspeed halafu mbili zimekimbia kawaida. Katika mazingira kama haya, ukitumia doppler effect, utajuaje? Nadhani inatumia speed ya object, ila sina uhakika, I'm just arguing from logic!
