Wakali wa IT, Application Hii Inahitajika Sana Dar es Salaam!

Wakali wa IT, Application Hii Inahitajika Sana Dar es Salaam!

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,280
Waungwana wa jukwaa hili, Hamjambo wote?

Nionavyo, jiji la dar linahitaji mapinduzi makubwa ya kiteknolojia kwenye eneo la usafiri wa barabarani. Watu wa dar wataishi na foleni mpaka lini?

Tunafahamu sana kwamba foleni zinaangamiza uchumi, maisha ya familia, afya za watumia barabara nk. Madhara ya foleni huenda yangepungua sana iwapo mwenye gari/daladala/ usafiri angefahamu ni njia ipi salama ya kupita isiyokuwa na foleni kubwa.

Ufahamu ungewezekana kama pangekuwepo na ka-application fulani kwenye simu kanakokuonesha ni route gani kuanzia hapo ulipo inayofaa kupita.

Kuna mdau alikuja hapa na wazo hilo HAPA ila sijui kama alifanikiwa. Kusema kweli application ya aina hiyo ni muhimu sana kwa dar es salaam.

Je, wataalamu wenye uwezo wa kuunda app itakayoitwa 'Nmlioko hapa JF, mmeshaliwazia jambo hili?
 
Wazo lako lilishafanyiwa kazi na watu kupelekea kila kitu kunakohusika lakini mpaka leo kimya tokea 2012. Unafuatalia lakini hakuna anayejali wala kukupa jibu lenye msimamo.
 
Sasa hiyo app itahamishia foleni sehemu hizo ambazo inasema hazina foleni,mwarobaini wa foleni dar ni kuboresha miundombinu tu.
 
Wazo lako ni zuri sana, ila bila serikali kuwajibika katika kuboresha barabara/miundo mbinu bado hiyo application itakuwa haisaidii
 
Tatizo sio serikali wala sio developers..

Tatizo ni wabongo wenyewe, wako very local, tengeneza apps mpya yoyote for as long as haihusiani na udaku au ngono huwezi pata watu. Mtu utajikuta unatumia pesa ndefu kulipia servers na muda wa kutosha kudevelop application kwa watanzania lakini audience utakayokutana nayo hutoamini,

kulipia servers za kutosha kama una active users kumi ishirini per day huwezi chomoka. Wengi bado wanataka kuishi kizamani kidogo, smartphone ina facebook, whatsapp kazi kwisha. JF isingekua na jukwaa la mapenzi leo hii ingekua na active users less than buku kila siku.
 
Foleni za dar 90% ni predictable inajulikana kabisa ubungo, magomeni, tazara nk kuna foleni. Inabidi kuwe na barabara za juu kwenye makutano ya barabara atleast itasaidia.

Even ukitengeneza apps itasaidia kidogo sana kwa yale maeneo ambayo hayana foleni za kutabirika
 
Back
Top Bottom