Wajue Wafilisti/Wapalestina

Jackwillpower

JF-Expert Member
Oct 4, 2017
2,301
3,411
Wafilisti ni watu walioishi Kaanani ambao waliokuwa maadui wakubwa sana wa Israeli enzi za agano la Kale. Hawa walikuwa ni kundi mojawapo la wenyewe wa nchi ile kabla ya Israeli kuifikia kutoka Misri.

Lakini wana wa Israeli walipokiuka maagizo ya Mungu ya kuwaua wenyeji wote wa miji ile yaliyoikuta,ili wamiliki, wao wakazembea hawakuwaua wote, kinyume chake wakawabakisha baadhi yao ikiwemo hawa wafilisti na ndio hao baadaye wakaja kuwa mwiba mkubwa sana kwao kama vile Mungu alivyowaambia.

Kipindi baada ya kipindi walikuwa wakiwashambulia waisraeli, na walipomlilia Mungu, (Waamuzi 10:7-8 ), basi Mungu aliwanyanyulia waamuzi wa kuwaokoa kutoka katika mateso yao, mfano Samsoni.

Wafilisti kwasasa ndio Wapalestina, unaowasikia pale mashariki ya kati, jina hilo lilizaliwa kutoka katika lugha ya wagiriki, ambao waliwaita wafilisti wapalestina. Na ndio mpaka sasa limezoeleka hivyo.

Wafilisti ni nchi gani?

Kama tulivyoona wafilisti ni watu waliokutwa Kaanani kabla ya wana wa Israeli, lakini sio taifa au nchi. Japokuwa enzi zile walikuwa na miji yao mikuu mitano nayo ni.

  1. Gaza,
  2. Ashdodi,
  3. gathi,
  4. Ashkeloni, na
  5. Ekroni
(1Samweli 6:17, Yoshua 13:3).

Walikuwa na wakuu/Wafalme wao watano pia kila mmoja na mji wake soma (Waamuzi 3:3). Sasa Miji hii yote ilikuwa kusini magharibi mwa taifa la Israeli.

Lakini Habari za wafilisti zinatufundisha nini?

Yapo mambo ambayo Mungu anaweza kutuagiza kufanya yakayazembea na madhara yake yakawa mpaka vizazi vya baadaye, kama vile tunavyoona hawa wafilisti/Wapalestina, hawakuwa mwiba tu kwa Israeli wakati ule..Bali hata sasa ni mwiba mkali sana..Kama wewe ni mfuatiliaji wa diplomasia za kimataifa utaweza kufahamu ni kitu gani kinaendelea pale Israeli saa hii , kila kukicha ni machafuko.

Hivyo tuwe makini sana na maagizo ya Mungu, anayotuagiza tusiyapuze hata kidogo,.


1621470104773.png
 
Kwahiyo Mungu alitaka wafilisti wafe wote kama wahutu walivyotaka watutsi wafe wote

1. Yaani MUNGU alitaka wapalestina wafe wote ili Israel akae kwa raha mustarehe?
2.Je MUNGU wa UPENDO ndo huyo huyo ?


NB: Imani ni jambo gumu

Kwa hyo Mungu aliagiza binadamu aue binadamu mwenzake ...

Dah bas Kaz ipo

Vp kuhusu AMRI YA 5 ya Mungu kea hyo anapingana na Amri zake ambayo anatuambia USIUE
Agano la Kale linaonyesha kwamba Wafilisti waliabudu miungu mitatu: Ashtorethi, Dagoni, na Baal-Zebubu-kila mmoja alikuwa na madhabahu katika miji mbalimbali (Waamuzi 16:23, 1 Samweli 31:10; 2 Wafalme 1:2). Matokeo ya akiolojia yanaonyesha kuwa askari wa Wafilisti walibeba sanamu za miungu yao katika vita (2 Samweli 5:21). Inaonekana, pia walikuwa watu washirikina

Wakanaani, walikuwa wamemkataa Mungu na sheria yake. Kulikuwa na mashahidi katika nchi hiyo kwa Wakanaani: Ibrahimu, Isaka, Yakobo, na familia zao. Walikuwa watu waliomfuata Bwana. hawakuwa wasio na hatia; Wakanaani walikuwa wamefilisika kimaadili na hawawezi kubadilika katika uovu wao.

Israeli walikuwa watu waliochaguliwa na Mungu, haki ya Bwana ilitumika kwao kama inavyotumika kwa mataifa mengine. Haki ya Mungu haionyeshi upendeleo. Katika Kumbukumbu la Torati 20:18, Bwana aliwaambia Israeli kuwa moja ya sababu za msingi kwamba jeshi lake lilikuwa kuangamiza mataifa mengi mbele yao ni ili wasiwafundishe kufanya kulingana na tabia zao zote za kuchukiza ambazo kuabudu miungu yao. na kuwafanya wamtendee dhambi Bwana.
 
Crazy God ever heard,yaani huyo Mungu ni wazimu na hafai yaani alijichagulia kakikundi ka wanywa mvinyo kutoka uru ya walkadayo na kuwapa mamlaka wanyang'anye ardhi ya watu kwa sharti et awaue wakazi wote hadi watoto na wanawake
Katili Sana huyo YHW Mungu wa islael aisee hivi kwanini asingewaongoza hao watu wake waje kusini ya misri nikimaanisha huku east Africa ambako kulikua na ardhi ya kutosha wakaja fyeka mapori na kutengeneza nchi mbaka akaamua kuwapeleka sehemu ya makazi ya watu wasababishe Vita na umwagaji damu ?
Fyeka Waamori,wagirgash,wafilisti,
wahivi,waakron na wengine wengi ili apole ardhi aiseee

Hizi dini za mashariki ya Kati na huyo Mungu wao ana walakini waafrika tuamke tuachane na huyo Mungu hafai kabisa
NB miungu yetu waafrika ilikua ya upendo Sana kabla hawa kenge kutoka middle East kuja kuharibu bongo za babu babu zetu,mwanzo walikua wanaishi kwa ushirikiano na upendo mkubwa ila hawa wavaa kobazi,kanzu na vilemba walipotua tu na majahazi yao biashara za kuuza watu zikaanza!
Walipokuja wagalatia ndio mweeee walitugawa kimakundi kabisaaaaaa

Wake up you black race!
Tunapigwa kamba!
 
Kwahiyo Mungu alitaka wafilisti wafe wote kama wahutu walivyotaka watutsi wafe wote

1. Yaani MUNGU alitaka wapalestina wafe wote ili Israel akae kwa raha mustarehe?
2.Je MUNGU wa UPENDO ndo huyo huyo ?


NB: Imani ni jambo gumu

Kwa hyo Mungu aliagiza binadamu aue binadamu mwenzake ...

Dah bas Kaz ipo

Vp kuhusu AMRI YA 5 ya Mungu kea hyo anapingana na Amri zake ambayo anatuambia USIUE
Ni kwamba mwanzoni, tunapaswa kuzingatia asili ya Mungu. Yeye ni Bwana aliye huru na ana haki kamili ya kutumia nguvu zake kwa njia yoyote atakayochagua. Yeye ndiye Muumba wa vitu vyote; kwa hivyo, ana haki kamili ya umiliki juu ya kila kitu. Ni hamu ya Mungu, na kusudi la Israeli kurithi nchi ya Kanaani. Mungu, ana haki za Muumba. Ni nani awezaye kumwambia, "Kwa nini umenifanya hivi? Je! Unafanya nini? Unafanya nini?"

Pili, Wakanaani hawakuwa watu wasio na hatia kwa njia yoyote ile waliposimama mbele za Mungu na Israeli. Je! Wakanaani walikuwa watu wa amani, waadilifu, na wanyofu?

Hiyo sivyo ilivyo. Wakati Mungu alimuahidi Abrahamu kwamba uzao wake utarithi nchi ya Kanaani, alisema haitafanyika hadi kizazi cha nne baada ya Ibrahimu kwa sababu uovu wa Waamori bado haujakamilika.

Walifanya mambo kama dhabihu ya watoto, uchumba, uasherati, ukahaba wa hekaluni, na matendo mengine mabaya.

Wakanaani, walikuwa wamemkataa Mungu na sheria yake. Kulikuwa na mashahidi katika nchi hiyo kwa Wakanaani: Ibrahimu, Isaka, Yakobo, na familia zao. Walikuwa watu waliomfuata Bwana. hawakuwa wasio na hatia; Wakanaani walikuwa wamefilisika kimaadili na hawawezi kubadilika katika uovu wao.

Israeli walikuwa watu waliochaguliwa na Mungu, haki ya Bwana ilitumika kwao kama inavyotumika kwa mataifa mengine. Haki ya Mungu haionyeshi upendeleo. Katika Kumbukumbu la Torati 20:18, Bwana aliwaambia Israeli kuwa moja ya sababu za msingi kwamba jeshi lake lilikuwa kuangamiza mataifa mengi mbele yao ni ili wasiwafundishe kufanya kulingana na tabia zao zote za kuchukiza ambazo wamezifanyia miungu yao. na kuwafanya wamtendee dhambi Bwana.
 
1. Yaani MUNGU alitaka wapalestina wafe wote ili Israel akae kwa raha mustarehe?
2.Je MUNGU wa UPENDO ndo huyo huyo ?


NB: Imani ni jambo gumu
Yeah Mungu alitaka ibada yake isichafuliwe na ibada ya Baali. Kama alivyoeleza mwenye uzi Israel iliagizwa kuuwa watu wote lakini hawakutii mwisho wa siku Mungu akawaambia kama mmewaacha watakuwa mwiba katika mbavu zenu.(unajua mwiba ulivyo) ndio mpaka leo
 
Ni kwamba mwanzoni, tunapaswa kuzingatia asili ya Mungu. Yeye ni Bwana aliye huru na ana haki kamili ya kutumia nguvu zake kwa njia yoyote atakayochagua. Yeye ndiye Muumba wa vitu vyote; kwa hivyo, ana haki kamili ya umiliki juu ya kila kitu. Ni hamu ya Mungu, na kusudi la Israeli kurithi nchi ya Kanaani. Mungu, ana haki za Muumba. Ni nani awezaye kumwambia, "Kwa nini umenifanya hivi? Je! Unafanya nini? Unafanya nini?"

Pili, Wakanaani hawakuwa watu wasio na hatia kwa njia yoyote ile waliposimama mbele za Mungu na Israeli. Je! Wakanaani walikuwa watu wa amani, waadilifu, na wanyofu?

Hiyo sivyo ilivyo. Wakati Mungu alimuahidi Abrahamu kwamba uzao wake utarithi nchi ya Kanaani, alisema haitafanyika hadi kizazi cha nne baada ya Ibrahimu kwa sababu uovu wa Waamori bado haujakamilika.

Walifanya mambo kama dhabihu ya watoto, uchumba, uasherati, ukahaba wa hekaluni, na matendo mengine mabaya.

Wakanaani, walikuwa wamemkataa Mungu na sheria yake. Kulikuwa na mashahidi katika nchi hiyo kwa Wakanaani: Ibrahimu, Isaka, Yakobo, na familia zao. Walikuwa watu waliomfuata Bwana. hawakuwa wasio na hatia; Wakanaani walikuwa wamefilisika kimaadili na hawawezi kubadilika katika uovu wao.

Israeli walikuwa watu waliochaguliwa na Mungu, haki ya Bwana ilitumika kwao kama inavyotumika kwa mataifa mengine. Haki ya Mungu haionyeshi upendeleo. Katika Kumbukumbu la Torati 20:18, Bwana aliwaambia Israeli kuwa moja ya sababu za msingi kwamba jeshi lake lilikuwa kuangamiza mataifa mengi mbele yao ni ili wasiwafundishe kufanya kulingana na tabia zao zote za kuchukiza ambazo wamezifanyia miungu yao. na kuwafanya wamtendee dhambi Bwana.
kwa hiyo ndugu huyo Mungu muweza wa yote alishindwaje kuwabadilisha hao makabila washenzi ili waifute njia njema?
Kwanini alishindwaje kuwapiga mkwara kwa ishara kuu ili wabadilike Kama walikua hawaamini katika Mungu YHW
Kwa ishara kuu kabisa ilitosha kuwabadilisha hao watu waachane na miungu wengine hapo wa kulaumiwa Nani Kati ya kutokujua kwao na huyo Mungu?

Nauliza tu mkuu!
 
kwa hiyo ndugu huyo Mungu muweza wa yote alishindwaje kuwabadilisha hao makabila washenzi ili waifute njia njema?
Kwanini alishindwaje kuwapiga mkwara kwa ishara kuu ili wabadilike Kama walikua hawaamini katika Mungu YHW
Kwa ishara kuu kabisa ilitosha kuwabadilisha hao watu waachane na miungu wengine hapo wa kulaumiwa Nani Kati ya kutokujua kwao na huyo Mungu?

Nauliza tu mkuu!
Kaka Mungu sio mjinga kama binadamu, Mungu haangalii sura anaangalia ndani ya moyo. Mpaka afanye maamuzi hayo alishaona mioyo yao sio ya kubadilika.

Ungekuwa wewe ungeangalia sura na kuanza kubagua
 
Kwahiyo Mungu alitaka wafilisti wafe wote kama wahutu walivyotaka watutsi wafe wote
Nahisi hivo hivo Ila tu Kama mungu hakuwaumba na hawapendi kabisa,....Kwan wafilist walimkosea Nini mungu kiasi Cha mungu kuagiza wauawe na wasiwepo kabisa?, Hizi hadithi za watu flan kujimegea priority zinanikera Sana , Mara sijui jackob alipendwa na mamaake kiasi baraka zikaibwa , Mara sijui alinunua baraka za uzao wa kwanza kwa mkate kakaake aalipokuwa na njaa (manake alikuwa mkaa nyumbani na ni mchoyo hata kwa Kaka kumuuzia chakula na anapendwa na mama) , yaan sielew elew mrad tu kujimegea shavu, hivi mungu wa Israel hawahusu parestina?, Vipi kuhusu sisi tusio waisrael Wala waparestina?....sizan Kama mungu ni mbaguzi, I
 
kwa hiyo ndugu huyo Mungu muweza wa yote alishindwaje kuwabadilisha hao makabila washenzi ili waifute njia njema?
Kwanini alishindwaje kuwapiga mkwara kwa ishara kuu ili wabadilike Kama walikua hawaamini katika Mungu YHW
Kwa ishara kuu kabisa ilitosha kuwabadilisha hao watu waachane na miungu wengine hapo wa kulaumiwa Nani Kati ya kutokujua kwao na huyo Mungu?

Nauliza tu mkuu!
MUNGU SIO DIKTETA AKULAZIMISHE UMUABUDU KINGUVU

Halafu watu hawabadiriki kwa ishara

Mathayo 12:38-41 BHN​

Kisha baadhi ya waalimu wa sheria na Mafarisayo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.” Naye akawajibu, “Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara, lakini hamtapewa ishara isipokuwa ile ishara ya nabii Yona. Jinsi Yona alivyokaa siku tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha. Watu wa Ninewi watatokea wakati wa hukumu, nao watakihukumu kizazi hiki kwamba kina hatia. Maana Waninewi walitubu kwa sababu ya mahubiri ya Yona, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Yona!
 
Nahisi hivo hivo Ila tu Kama mungu hakuwaumba na hawapendi kabisa,....Kwan wafilist walimkosea Nini mungu kiasi Cha mungu kuagiza wauawe na wasiwepo kabisa?, Hizi hadithi za watu flan kujimegea priority zinanikera Sana , Mara sijui jackob alipendwa na mamaake kiasi baraka zikaibwa , Mara sijui alinunua baraka za uzao wa kwanza kwa mkate kakaake aalipokuwa na njaa (manake alikuwa mkaa nyumbani na ni mchoyo hata kwa Kaka kumuuzia chakula na anapendwa na mama) , yaan sielew elew mrad tu kujimegea shavu, hivi mungu wa Israel hawahusu parestina?, Vipi kuhusu sisi tusio waisrael Wala waparestina?....sizan Kama mungu ni mbaguzi, I
Alikua na kusudi lake,ila kwa sasa kashatoa pazia lile la kutenganisha binadamu. Kwa sasa kila mtu anafuata sheria zake anakubalika naye
 
Back
Top Bottom