Waitara atamba, adai Heche hana nyumba Tarime, anaishi kwa mama yake, asema anamsubiri kwa hamu uchaguzi wa 2025

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
12,004
20,681
Tarime haijawahi kupoa!

Mbunge Waitara, akihojiwa na kituo Cha tv Cha Dar24 ametamba kwamba hawezi kubabaishwa na mwanafunzi wake kisiasa, John Heche, na kwamba atamchakaza kwenye uchaguzi wa 2025.

Waitara ametamba kwamba John Heche hana nyumba Tarime, na kwamba anaishi kwa mama yake, hivyo hana msaada wowote kwa wanatarime. Waitara ameeleza kwamba ni aibu kwa Mila za kikurya kwa kijana wa umri wa Heche kungangania kwenye nyumba ya mama badala ya kujitegemea kwa kujenga ya kwake.

Waitara ambaye alikuwa anaongea kwa uchungu mfanano wa wenye kijacho,amejiapiza kutokimbia Jimbo na kwenda ukonga na anadai Tarime ni nyumbani kwao.

Waitara alielezea kwamba Heche hajaacha maendeleo yoyote Jimboni, zaidi ya umasikini uliotopea

 
Acheni ujinga kwani nyumba ndiyo inaoongoza wananchi au mtu. Kwani nyumba ni moja ya sifa za kuteuliwa kuwa Mbunge? Mmesahau Mbunge wa Kwale nchini Kenya aliyefanya kampeni kwa mkokoteni wa punda akiwa hana hata Banda lakini leo ni Jimbo lake limepigiwa mfano wa kuigwa kwa kasi ya maendeleo. Anayelala na mgonjwa ndiye anajua Hali yake.
 
Hamjui Heche vizuri.

Heche ana nyumba kubwa sana tu Mwanza mitaa ya Nyegezi-Majengo mapya , na nyumba yake imetizamana na ya moja ya moja ya wakurugenzi wa SUMA JKT. Ukiwa hapo stend kuu ya Mwanza, bodaboda yoyote ukimwambia akupeleke kwa HECHE ni faster tu.

Yeye ajitahidi kujikita kwenye hoja za msingi.
 
Hamjui Heche vizuri.

Heche ana nyumba kubwa sana tu Mwanza mitaa ya Nyegezi-Majengo mapya , na nyumba yake imetizamana na ya moja ya moja ya wakurugenzi wa SUMA JKT. Ukiwa hapo stend kuu ya Mwanza, bodaboda yoyote ukimwambia akupeleke kwa HECHE ni faster tu.

Yeye ajitahidi kujikita kwenye hoja za msingi.
Kwani Mwanza ni kwao
 
Hamjui Heche vizuri.

Heche ana nyumba kubwa sana tu Mwanza mitaa ya Nyegezi-Majengo mapya , na nyumba yake imetizamana na ya moja ya moja ya wakurugenzi wa SUMA JKT. Ukiwa hapo stend kuu ya Mwanza, bodaboda yoyote ukimwambia akupeleke kwa HECHE ni faster tu.

Yeye ajitahidi kujikita kwenye hoja za msingi.
Kwani Waitara na Heche kwao ni Mwanza?
 
Hamjui Heche vizuri.

Heche ana nyumba kubwa sana tu Mwanza mitaa ya Nyegezi-Majengo mapya , na nyumba yake imetizamana na ya moja ya moja ya wakurugenzi wa SUMA JKT. Ukiwa hapo stend kuu ya Mwanza, bodaboda yoyote ukimwambia akupeleke kwa HECHE ni faster tu.

Yeye ajitahidi kujikita kwenye hoja za msingi.
Jimboni kwake ana makazi?
 
Acheni ujinga kwani nyumba ndiyo inaoongoza wananchi au mtu. Kwani nyumba ni moja ya sifa za kuteuliwa kuwa Mbunge? Mmesahau Mbunge wa Kwale nchini Kenya aliyefanya kampeni kwa mkokoteni wa punda akiwa hana hata Banda lakini leo ni Jimbo lake limepigiwa mfano wa kuigwa kwa kasi ya maendeleo. Anayelala na mgonjwa ndiye anajua Hali yake.
Jinga kweli, hata Nyerere hakuwa na nyumba kwao
 
Back
Top Bottom