Waislamu Tunadai nini Kwenye Katiba Mpya?

Kiukweli sasa waislam mmchoka kweli kweli mahakama ya kadh kadh mkianza hayo na ss tuanaanza kudai vyetu hosptal shule na nk mbona mmepewa majengo na serikal wakristo wametulia ingekuwa ninyi mngepga makelele mwaka wote kwani kuna msaada mzur kama kukombolewa kielem haya makelele haya

na ninyi mnapata mabilion kila mwaka kuptia MoU ndio mana mmetulia
 
Tunadai kila mmoja ajisalimishe kwa mola wake aliyemuumba. A silim.
kuhusu swala la MoU mi mwenyewe naona kuna tatizo, hivi baada ya hospitali kutoa huduma je kanisa huwa halibakiwi na chochote? au tuaminishwe zinajiendesha bila faida? nahisi kinachobaki ndio kile serikali inachotoa au sehemu yake kama pesa ya mishahara na uendeshaji kuhusu kujisalimisha kwa mola sio kila mtu ameumbwa na mola wengine tuna mungu wetu usitake kufanya huyo mola wako awe mungu wa kila mtu, kuhusu OIC nchi yetu ni ya dini nyingi na imani nyingi, na katika ufunguzi wa OIC huko senegal mfunguaji alisema islam is the only true religion and member states zina believe hivyo sasa kwa nchi ya dini nyingi hilo limekaaje?. nchi kama urusi na china zina uwakilishi OIC lakini sio member na sisi tunaweza kufanya the same thing. kuhusu vatican sioni shida mbona tanzania ina ubalozi na nchi za kidini kama vile Iran kwa nini vatican iwe taabu tukitumia jazba na emotions katika mambo yanayohitaji kufikiri hatufiki mbali
 
Waislamu Tunadai nini Kwenye Katiba Mpya?

Waislamu sehemu mbali mbali nchini wamekuwa wakiliuliza Jukwaa kuhusu ni yepi madai ya waislamu katika utoaji maoni yatakayokusanywa na tume? Yafuatayo ni baadhi ya madai yetu ya msingi kabisa na mengine mtaarifiwa baadae kupitia makongamano na vikao husika;-

  • Mahakama ya Kadhi iwepo nchini na iwekwe kwenye katiba .
  • Usekula wa dola ufafanuliwe maana kimaneno nchi haina dini lakini katika utendaji wa serikali nchini kama vile kuna dini inayopewa kipaumbele.
  • Uhusiano wa kimataifa Tanzania ijiunge na OIC vinginevyo uhusiano na Vatican pia uvunjike.
  • Uhuru wa ibada utambuliwe (hivi sasa kuna uhuru wa imani na si uhuru wa ibada kwani waislamu wanapotekeleza baadhi ya ibada wanabughudhiwa. Mfano, kusali sala tano kwa wanafunzi, maaskari na wafanyakazi, uvaaji wa hijabu, ufugaji ndevu, bunge kuendelea siku za ijumaa, mitihani kufanyika siku za sikukuu za Idi n.k.)
  • Haki za kimakundi ziainishwe, zitambuliwe na zitiwe katika katiba.
  • Sheria za Kiislamu zitambuliwe na ziheshimiwe. Sheria za Kiislamu za ndoa, mirathi na talaka na haki za wanawake ziheshimiwe.
  • Siku za mapumziko zizingatie imani za dini na siyo wakristo peke yao (Jumamosi – Wasabato, Jumapili – Madhehebu mengine ya Wakristo).
  • Ubaguzi wa kidini unaofanywa na serikali usiwepo. Mfano, serikali kuingia mikataba ya kutoa pato la taifa kwa wakristo kupiti MoU.
Haya ndiyo baadhi ya madai yetu katika mchakato wa katiba. Waislamu tudai madai haya na hayo mengine tutakayoyatoa.
Imetolewa na;
Sheikh Muhammad Issa


source
jukwaa la waislamu

Mimi kwanza naamini kuwa mpaka mtu amejiunga na mtandao makini kama Jamii Forums atakuwa angalau ana elimu ya msingi kabisa ambayo ni ya sekondari. Kwa hawa jamaa kuleta hoja kama hii inaonyesha kuwa elimu yao haiwasaidii kabisa. Dunia nzima inajua kuwa
WAKRISTU WANA KATIBA YAO, BIBLIA NA WAISLAM WANAKATIBU YAO, KURAN TUKUFU. Tunatafuta hapa sasa ni katiba ya KISERIKALI NA WALA SI YA KIDINI. Watanzania tuamke tusonge mbele. Watu wa DINI wapo wataendesha mambo yao na sisi tusio wa dini tuendelee mbele na katiba yetu ya TANZANIA. Tuache UDINI, TUJENGE NCHI.
 
Ukiamua kuingia JF uwe tayari kuwa wazi na usionekane mtu anayetafuta huruma ya watu hapa. Me binafsi sina ugomvi na kikundi cha watu wa imani fulani kutaka nini kiwemo kwenye katiba ili mambo yao yaweze kwenda. Lakini tukumbuke katiba siyo ya dini fulani wala ya kikundi kidogo cha watu wanaohitaji matakwa yao yaingizwe ili waishi vizuri. Tukiuchukulia mchakato wa katiba kwa mtazamo huu hatuwezi kupata katiba ambayo italijenga Taifa, ila makundi ya watu. Kwa mfano, CCM wana mambo yao ambayo wangelipenda yawemo kwenye katiba ili waendelee kubakia madarani milele daima, CHADEMA nao wana yao ambayo wanapenda yaingie ili washike dola, CUF tayari walishawasilisha mswada wa katiba, siyo mawazo...no mswada wa katiba kwenye wizara ya Sheria na Katiba. Vivyo hivyo NCCR, Tadea, TLP, ADC, Wakatoliki, Waanglikana, Wasabato, AIC, TAG, Full gospel bible fellowship, waalimu, madaktari, wabunge, Wakulima, Wafugaji, Machinga, Mama lishe na kila aina ya kundi ambalo unalifahamu.

Sasa fikiria tukigawanyika katika makundi haya na kila kundi likaainisha mahitaji yake na ndiyo kikawa kilio chao....tutapata katiba ya aina gani? Hapo kutakuwa na katiba kweli au utakuwa utani tunaleta. Maana kwenye madai ya waislamu haujasema kuwa UMILIKI WA ARDHI, MATUMIZI MAZURI YA RASILIMALI, MADARAKA YA RAIS, TUME HURU YA UCHAGUZI, MUUNDO WA MUUNGANO, MUUNDO WA SERIKALI, SERIKALI IWE NA WIZARA NGAPI ZA KUDUMU NA UKOMO UWE WIZARA NGAPI, KAMA NI MUHIMU KUWA NA WAKUU WA WILAYA, DAS, RAS, NA WAKURUGENZI KATIKA ENEO MOJA LA KUFANYIA KAZI, VIPI HAKI ZA WATOTO, na mengine mengi ya msingi. Haya hayahusiani na kundi lolote miongoni mwa makundi ambayo nimeyataja hapo juu. Tukisema kila mmoja alizungumzie kundi lake, nani atazungumzia masuala ya kitaifa kama ambayo nimeyaainidha kwa herufi kubwa hapo juu. Hauoni kuwa tutakuwa hatulitendea haki taifa letu?

Hivi waislamu mkipewa mahakama ya kadhi ndiyo kero zenu zitaisha? Tanzania ikijiunga na OIC, muislamu wa Kagera na Kigoma vijijini wananufaika nini na OIC? Au ni ulaji wa Mashekh tu? Na najiuliza kama mtaruhusiwa kupumzika na kutokufanya kazi siku ya ijumaa kero zinakuwa zimeisha? Mbona mimi mkristu Jumapili napiga kazi kama kawaida? Dini ni mapokeo tu...hapo awali kabla ya waarabu na wazungu hatukuwa na Ijumaa, Jumamosi wala Jumapili, tulikuwa tunafanya kazi kila siku za juma na mambo yetu yalikuwa safi kuliko hata sasa ambapo tunajifanya watu wa Mungu ilihali hatuzifuati amri zake...nini dini bwana? Angalia nchi ambazo zimejipambanua kuwa za kidini, Iraq, Iran, Libya, na sasa Sudan kaskazini, Yemen, Syria, Afghanstan na nyingine nyingi, mambo siyo shwari huko...kila siku watu wanakufa kama mbwa...!

Nashauri...tuangalie na tuchangie mambo ya msingi kwenye tume ya katiba. Tukileta mambo ya udini, wengine wataleta mambo ya ukanda, tutafika mbali na kuleta mambo ya ukabila ya Ukijiji, Hatutabaki salama. Tuzungumzie mambo ambayo yanatufanya kuwa wamoja kama watanzania. Dini kila mtu ana yake na wengine hawana kabisa na wanaishi, tena maisha mazuri bila stress, dini zenyewe za sasa, wachungaji, mapadri na mashehe wamekuwa wachumia tumbo...hakuna lolote...

Mwalimu Nyerere alisema, najua utapinga kwa sababu wewe Muislamu...."Hakuna dhambi mbaya kama dhambi ya ubaguzi. Haiishi tu kusema wewe ni mkristo na mimi ni muislamu. Ukimaliza kusema mimi Mtanganyika na wewe Mzanzibar, tukifika pemba tutasema wewe Mpemba na mimi Muunguja, huku bara tutasema wewe wa Kaskazini na mimi wa kusini, Hata kwenye dini, leo unajiita muislamu na kuwaorganize waislamu mambo yenu...siku yakitokea ya kutokea, utasema wewe mshiha...na mimi msuni...wewe muislamu wa tabora na mimi wa mwanza....hadi makanisani....wote ni wakristo...lakini tutasema wewe mkatoliki, na mimi mlutheri...tutabaguana hadi kwenye familia zetu, na tukicheza na dhambi hii, tutaanza kubagua hadi viungo vya miili yetu....wewe mkono wa kushoto na wewe wa kulia." Dhambi ya ubaguzi siyo nzuri...

Maji yanatuunganisha wote, Maliasili zetu kama misitu, wanyama, madini, gesi, mafuta na makaa ya mawe yanatuunganisha wote kama watanzania. Tukipata katiba nzuri yenye mgawanyo mzuri wa madaraka, kupunguza madaraka ya rais, kuunda tume huru ya uchaguzi kuondoa wakuu wa wilaya, kutengeneza serikalil za majimbo, wote waislamu na wakristo tutafaidika na haya mambo...siyo habari za mahakama za kadhi, kuvaa hijabu, kuabudu...haya nimapokeo tu, yajadiliwe misikitini yaishie huko...sasa tukifikia kuweka kwamba sasa kuvaa hijabu ruksa...kwenye katiba, inakuwa nchi ya Kiislamu sasa. Au tuseme sasa Mahakama ya kadhi hiyo, serikali itagharamia....na wakristo wakidai yao....? Nani atasema serikali haina dini tena? Tuache hii mambo....Asante, naamini utakuwa umenielewa vyema.

TOGETHER WE CAN BRING THE CHANGES WE NEED...YES WE CAN...TUACHE UDINI...TANZANIA MBELE KAMA TAI...MENGINE YANAFUATA.....

I like this!!!

 
na ninyi mnapata mabilion kila mwaka kuptia MoU ndio mana mmetulia
hayo mabilioni ambayo waislam wanadai wakristo wanapewa kupitia hospitali na mashule, ukienda kwenye hospitali hizo utakuta waislam kibao wamevaa ushungi na wengine kanzu wameenda pale kutibiwa...hahaha, mashule waislam pia wanasoma huko...tatizo lipo tu kwasababu ya wivu...wanaona kama wanaonewa....wao waislam hawajakatazwa kujenga mashule ili nao wafaidi kama kufaidi kupo...basi kama ndo hivyo msije kabisa kwenye mahospitali yetu, msije kabisa kwenye mashule yetu kaeni tu mkatibiwe kwa waganga wa kienyeji mashehe wauza uchawi huko misikitini....akili za watu kama hawa (wachache wanaowachafua na waislam wengine wengi ambao wana akili zuri tu) ni za kipunga sana na hawata weza chochote hata tukibadilisha chuo kikuu udsm leo tukafukuza wakristo wote tukawapa iwe chuo cha waislam tu...mwaka mmoja tu kitakuwa kimeharibika kushika mkia duniani...tatizo la kutumia zaidi dini na imani kuliko reality katika ulimwengu ambao tunaishi ndani ya dini na imani tofauti wote tukiwa na haki zote katika dunia hii hii moja, kama hatutaishi kwa kuvumiliana ni ngumu sana.....unatakiwa unapoishi usifikiri dunia hii ni ya kiislam, kuna na watu wengine pia, usifikiri wewe tu ndo mwenye haki..kuna wengine pia wana haki zao....pambafuuuuuuuu
 
huu ni upummbavu wa chuo kikuu cha morogoro. waislam wa aina hii akili zao ni za kipummmbavu sana....ndo maana mnadharaulika.

Huwa najiuliza sana; Je, tatizo ni Uslamu au Wanazuoni wa Kiislamu? Hebu tuangalie mfano wa nchi zinazoitwa za Kiislamu, zina advantages gani zaidi ya ukandamizaji na neema kwa watawala? Raia wa nchi hizo wanafaidishwa na mfumo huo?
 
na ninyi mnapata mabilion kila mwaka kuptia MoU ndio mana mmetulia

Hiyo MoU inamsaidia nani? Wakristo ndo wanaotibiwa kwenye hizo hospitali?Mkoa, Wilaya na Kijiji unachotoka, Serikali ina hospitali ngapi na Wakristo wanazo ngapi?
 
wewe ndio MPUMBAVU USIELEWA

Wakristo wapo bze kusambaza makanisa ya ukweli vijijini, kujenga vyuo vikuu vya ukweli bila kutegemea majengo ya serikali, kuhakikisha shule zao za sekondari watoto wanafaulu kwa kiwango cha kimataifa na mabo mengine ya mendeleo kwa manufaa ya kila mtanzania. Cha kushangaza watu walio kalia akili wanadai mahakama??? (Wao wanafikiria kuhukumu tu kupitia mgongo wa serikali.
Unajua waislam walio wengi hawajui maana hasaa ya mahakama ya kadhi na utendaji wake. Dada zetu mlio zaa zaa na vidume visivyo eleweka subirini kupigwa mawe hadi mfe kwa kosa la kuzini. Chezea sharia weye!Hamjiulizi kwa nini kenya walifutilia mbali hiyo mahakama?

Mnazungumzia yale marahisi kupokelewa na wasio dig deep mbona hamzungumzii impact ya sharia kwa ndoa kati ya muislam na mkristo. Mjane mkristo aliyekua na ndoa ya serikali anaruhusiwa kuridhi mali za mmewe kwa mujibu wa sharia? Watoto je kama walifuata dini ya mama wanaruhusiwa kurithi mali ya baba yao kipenzi? Au ndo mali zitaenda kwa wafuga ndevu.

Midevu hamkatazwi kufuja kama ilivyo kwa wafuga rasta. Ila tu maofisini tunazitambua kama uchafu.

Let us unite kuwa piga vita mafisadi papa katika nchi yetu, tuungane kudai mahakama itakoyo mhukumu raisi na watendaji wake kwa ubadhilifu wa mali ya umma na si kufagilia udini.
 
Hospitali ya bugando 90% ya uendehsaji wake unatoka serekalini,wauguzi,madaktari,wafagiaji,madawa,ujenzi,na nk, vyote hivyo vipo chini ya serikali na hapo ni kodi ya watanzania wote bila kujali ni mkristo,muislamu,mpgani,mhindu,nk. na mgonjwa akifika pale hatibiwi bure kuna gharama ambazo baadhi ya watu hushindwa kuzilipa na kudiliki kupita ktk nyumba za ibada hasa misikitini ili kuweza kupata fedha za kulipa hgalama hizo, SUALI, JE FAIDA YA MAPATO YA HOSPITALI HIYO HUINGIA KANISANI AU SEREKALINI?JE SERIKALI HAIWEZI KUJENGA HOSPITALI ZAKE AU KUPANDISHA BAADHI YA HOSPITAL ZA MIKOA KUWA RUFAA?JE MABILIONI YA FEDHA YANAYOPELEKWA HUKO NI YA WAKRISTO PEKEE?
 
OIC ni moja ya taasisi ambazo zina manufaa na waislamu na hata wasio waislamu,kwani hutoa mikopo katika serikali za nchi masikini pasina riba,hivyo pale manposema ya kwamba tuangalia maslahi ya taifa katika katiba,kwani OIC ikitoamikopo hiyo itanufaisha waislamu peke yake?
 

Mimi kwanza naamini kuwa mpaka mtu amejiunga na mtandao makini kama Jamii Forums atakuwa angalau ana elimu ya msingi kabisa ambayo ni ya sekondari. Kwa hawa jamaa kuleta hoja kama hii inaonyesha kuwa elimu yao haiwasaidii kabisa. Dunia nzima inajua kuwa
WAKRISTU WANA KATIBA YAO, BIBLIA NA WAISLAM WANAKATIBU YAO, KURAN TUKUFU. Tunatafuta hapa sasa ni katiba ya KISERIKALI NA WALA SI YA KIDINI. Watanzania tuamke tusonge mbele. Watu wa DINI wapo wataendesha mambo yao na sisi tusio wa dini tuendelee mbele na katiba yetu ya TANZANIA. Tuache UDINI, TUJENGE NCHI.

Jenga hoja sio kukimbilia kusema udini,tofautisha hoja za dini na udini, sio kila manung'uniko ni udini,hivi mmasai akidai katengwa kwenye mfumo wa Elimu utasema ukabila? Kama hoja zao sio sahihi waelimishwe kitaalam,Madai ya Waislam ni kwa serikali sio Kanisan iache Serikali ipangue hoja na kitendo cha kushoboka kujibia Serikali ni ushahid wa kimazingira wa ukweli wa Madai yaoq
 
huu ni upummbavu wa chuo kikuu cha morogoro. waislam wa aina hii akili zao ni za kipummmbavu sana....ndo maana mnadharaulika.

JAMANI HII NDIYO SABABU MAWAZIRI WETU KARIBIA WOTE NI WEZI NA hawajui kujenga uchumi. Maana wanatuona tunaweka mbele fahari za kidini katika katiba badala ya kujenga katiba ambayo italinda na kujenga uchumi Imara. Lazima kwanza tujiulize kuwa , tumejifunza nini na Raisi wa nchi kuwa na nguvu kupita Bunge na mahakama? Halafu vile vile tujiulize ni madhala gani tumejipatia kutokana na kufuata siasa za ujama na kujitegemea kwa kulazimishwa?

Vile vile tujiulize hivi ni kwa nini wansiasa wetu kila kukicha nchi za kiarabu zinapopigwa na marekani au Israel huwa wnawatukana wamarekani na waisraelkwaniaba ya waarabu?

Tukiwa na mawazo ya uchungu na majibu yake kutokana na kujifunza huko, ndipo tutajenga katiba imara.

Somalia baada ya vita na kukaa bila nchi kwa miaka ishirini, leo hii wamejifunza mengi sana . Zuri walilojifunza ni kuhakikisha katiba yao haimpi madaraka makuu raisi wao kamwe. Bunge wamelipa nguvu. Mahakama wameipa nguvu. Na raisi kapewa kipande chake. Sasa ona hata somalia inatuacha kwa kujenga good governance.

Tuangalie maslahi ya uchumi kwanza na sio dini.
 
sawa ulichokisema lakini hatuwezi kutafuta maslahi ya inch ikiwa ndani ya inch kunawatu wanaangalia maslahi ya dini yao cha kwanza tuweke usawa ndani ya dini zote ili tuweze kudai maslahi ya inch yetu.kwa nini wengine waonewe na wengine wanufaike na inch ambayo tunasema haina dini ni mbaya sana kwa inch km hii ambayo inakuwa na wimbo uzuri wa amani,tuwemakini lkn muda si mrefu huu wimbo unaweza kubadilika ghafla
 
nakubaliana na ulicho kisema lkn kuna umuhimu wakujua nini maana ya dini kama utalifahamu uwezi kutenganisha dini na siasa tujitahidi kusoma tusilete fikra finyu nakusema tutenganishe siasa na dini!!!!
 
hUU upunguani umetoka wapi tena karne hii ..yaani bado mmekalia maswala ya udini tu hapa badala ya kuangalia mambo ya kimaendeleo..ndio maana huku pwani mji umejengwa na wageni tu..bure kabisa..mtakalia kutuwangia usiku na kuswali milele halafu pepo hamtaiona kwa ajili ya kutofanya kazi..
 
Hospitali ya bugando 90% ya uendehsaji wake unatoka serekalini,wauguzi,madaktari,wafagiaji,madawa,ujenzi,na nk, vyote hivyo vipo chini ya serikali na hapo ni kodi ya watanzania wote bila kujali ni mkristo,muislamu,mpgani,mhindu,nk. na mgonjwa akifika pale hatibiwi bure kuna gharama ambazo baadhi ya watu hushindwa kuzilipa na kudiliki kupita ktk nyumba za ibada hasa misikitini ili kuweza kupata fedha za kulipa hgalama hizo, SUALI, JE FAIDA YA MAPATO YA HOSPITALI HIYO HUINGIA KANISANI AU SEREKALINI?JE SERIKALI HAIWEZI KUJENGA HOSPITALI ZAKE AU KUPANDISHA BAADHI YA HOSPITAL ZA MIKOA KUWA RUFAA?JE MABILIONI YA FEDHA YANAYOPELEKWA HUKO NI YA WAKRISTO PEKEE?
hapa nakuunga mkono, lazima hizi hospitali zinapata faida swali ni je faida hizo zinaenda wapi. kama sio kwenye kujenga maparokia
 
OIC ni moja ya taasisi ambazo zina manufaa na waislamu na hata wasio waislamu,kwani hutoa mikopo katika serikali za nchi masikini pasina riba,hivyo pale manposema ya kwamba tuangalia maslahi ya taifa katika katiba,kwani OIC ikitoamikopo hiyo itanufaisha waislamu peke yake?
hapa kujiunga na OIC kwa ajili ya mkopo sikuungi mkono kabisa, kwa mfano msimamo wa OIC kuhusu israel unajulikana sasa unataka taifa zima liwe na msimamo huo wakati watu wengi hawatauunga mkono si kutakuwa na mgawanyiko!. mi nafikiri tujiunge kama observers tu
 
Ni kweli lkn kwa nini haya yapo? Na kwa nini wengine wakose? Na wengine wapate? Suala la udini tanzania liliasisiwa mwl.nyerere na ndiyo maana waislam wanatakakulifuta.je wajua chanzo cha kuwepo mapumziko siku ya jumamosi na jumapili.



"no right to say without research"
 
Back
Top Bottom