[h=2]Waislamu Tunadai nini Kwenye Katiba Mpya?[/h]Waislamu sehemu mbali mbali nchini wamekuwa wakiliuliza Jukwaa kuhusu ni yepi madai ya waislamu katika utoaji maoni yatakayokusanywa na tume? Yafuatayo ni baadhi ya madai yetu ya msingi kabisa na mengine mtaarifiwa baadae kupitia makongamano na vikao husika;-
Imetolewa na;
Sheikh Muhammad Issa
source
jukwaa la waislamu
- Mahakama ya Kadhi iwepo nchini na iwekwe kwenye katiba .
- Usekula wa dola ufafanuliwe maana kimaneno nchi haina dini lakini katika utendaji wa serikali nchini kama vile kuna dini inayopewa kipaumbele.
- Uhusiano wa kimataifa Tanzania ijiunge na OIC vinginevyo uhusiano na Vatican pia uvunjike.
- Uhuru wa ibada utambuliwe (hivi sasa kuna uhuru wa imani na si uhuru wa ibada kwani waislamu wanapotekeleza baadhi ya ibada wanabughudhiwa. Mfano, kusali sala tano kwa wanafunzi, maaskari na wafanyakazi, uvaaji wa hijabu, ufugaji ndevu, bunge kuendelea siku za ijumaa, mitihani kufanyika siku za sikukuu za Idi n.k.)
- Haki za kimakundi ziainishwe, zitambuliwe na zitiwe katika katiba.
- Sheria za Kiislamu zitambuliwe na ziheshimiwe. Sheria za Kiislamu za ndoa, mirathi na talaka na haki za wanawake ziheshimiwe.
- Siku za mapumziko zizingatie imani za dini na siyo wakristo peke yao (Jumamosi Wasabato, Jumapili Madhehebu mengine ya Wakristo).
- Ubaguzi wa kidini unaofanywa na serikali usiwepo. Mfano, serikali kuingia mikataba ya kutoa pato la taifa kwa wakristo kupiti MoU.
Imetolewa na;
Sheikh Muhammad Issa
source
jukwaa la waislamu