tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,832
- 25,127
Wakuu naingia moja moja kwenye mada bila kuwachosha. Nawashangaa sana Wakatoliki na Waislamu kwa kukaa kimya hadi sasa huku askofu Gwajima akinyanyaswa bila wao kukemea wala kutoa tamko lolote kuhusu serikali kufunga Kanisa la Ufufuo na Uzima kihuni na bila kufuata utaratibu.
Walichokifanya serikali ni uhuni na uhujumu wa imani kwa kuingilia mambo ya kiimani. Sote tunajua serikali haina dini, hivyo haipaswi kuingilia mambo ya kiimani hata kidogo. Kama hawaelewi mahubiri ya Dr Gwajima ni bora wangehudhuria madhabahuni kwake wapate ufafanuzi wa kiroho badala ya kufunga kanisa kisiasa kwa kulizingira na mabaunsa wenye bunduki.
Miongoni mwa watu ambao Gwajima anawatetea ni mapadre na mashehe waliokwisha kutekwa na kuuawa. Tumeshuhudia majuzi mapadre na mashehe wanatekwa na kuuawa. Na siku chache zilizopita padre Kitima alinusurika kufa baada ya kupigwa rungu kichwani na mpaka sasa yupo mahututi hospitalini. Cha ajabu yule "mtu" aliyempiga rungu hadi sasa hatujasikia akifikishwa mahakamani.
Kwa upande wetu waislamu, mashehe wetu wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa bila sababu za msingi. Lakini cha kushangaza hadi sasa sio waislamu wala wakatoliki waliokemea wala kutoa tamko kuhusu haya mauaji yanayoendelea.
Ni lini hasa waislamu na wakatoliki mtaanza kupaza sauti kuhusu udhalimu wa serikali ya CCM kuingilia mambo ya dini kwa kutafsiri kipotovu mahubiri ya kibiblia wakitaka manabii na maaskofu wahubiri upagani ghairi ya imani? Hili halikubaliki. Waislamu na wakatoliki hebu amkeni kumekucha kabla nanyi hamjaanza kufungiwa.
Kumbuka huu ni kama mtego wa panya. Wakimaliza kufuta kanisa la Gwajima watakuja kufuta uislamu na ukatoliki ili nchi ibaki kwenye giza nene la kuabudu mizimu na mashetani kupitia damu za raia wasiokuwa na hatia wanaotekwa na kuuawa kila kukicha. Please wake up yourselves before being awakened!
MAONI YANGU
Haipingiki kuwa serikali imejaa wapagani na inaendeshwa kwa misingi ya kipagani. Gwajima ni mtu wa Mungu na anahubiri kwa uwezo wa roho mtakatifu. Katika biblia kuna amri inayokataza kuua. Hapa ndipo mahubiri ya Gwajima yamejikita kwa kukemea utekaji na mauaji ya raia wasiokuwa na hatia. Na amefafanua vizuri kuwa kama hawo wanaotekwa na kuuawa wana makosa ya jinai, basi wakamatwe wapelekwe mahakamani wafunguliwe mashtaka badala ya kuuliwa na kutupwa kama mbwa mahali pasipojulikana. Kosa la Gwajima ni lipi hapa? Ni kusimamia imani yake ya kiroho?
Ikiwa serikali inaingilia hadi amri kumi zilizomo kwenye biblia zisifundishwe makanisani, basi iifute kabisa biblia takatifu na kutunga biblia ya kipagani iwe inatumika makanisani. Hatuwezi kuvumilia kuona biblia takatifu ya kanisa inasiginwa na wapagani (serikali) tukiwa tumekaa kimya.
Walichokifanya serikali ni uhuni na uhujumu wa imani kwa kuingilia mambo ya kiimani. Sote tunajua serikali haina dini, hivyo haipaswi kuingilia mambo ya kiimani hata kidogo. Kama hawaelewi mahubiri ya Dr Gwajima ni bora wangehudhuria madhabahuni kwake wapate ufafanuzi wa kiroho badala ya kufunga kanisa kisiasa kwa kulizingira na mabaunsa wenye bunduki.
Miongoni mwa watu ambao Gwajima anawatetea ni mapadre na mashehe waliokwisha kutekwa na kuuawa. Tumeshuhudia majuzi mapadre na mashehe wanatekwa na kuuawa. Na siku chache zilizopita padre Kitima alinusurika kufa baada ya kupigwa rungu kichwani na mpaka sasa yupo mahututi hospitalini. Cha ajabu yule "mtu" aliyempiga rungu hadi sasa hatujasikia akifikishwa mahakamani.
Kwa upande wetu waislamu, mashehe wetu wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa bila sababu za msingi. Lakini cha kushangaza hadi sasa sio waislamu wala wakatoliki waliokemea wala kutoa tamko kuhusu haya mauaji yanayoendelea.
Ni lini hasa waislamu na wakatoliki mtaanza kupaza sauti kuhusu udhalimu wa serikali ya CCM kuingilia mambo ya dini kwa kutafsiri kipotovu mahubiri ya kibiblia wakitaka manabii na maaskofu wahubiri upagani ghairi ya imani? Hili halikubaliki. Waislamu na wakatoliki hebu amkeni kumekucha kabla nanyi hamjaanza kufungiwa.
Kumbuka huu ni kama mtego wa panya. Wakimaliza kufuta kanisa la Gwajima watakuja kufuta uislamu na ukatoliki ili nchi ibaki kwenye giza nene la kuabudu mizimu na mashetani kupitia damu za raia wasiokuwa na hatia wanaotekwa na kuuawa kila kukicha. Please wake up yourselves before being awakened!
MAONI YANGU
Haipingiki kuwa serikali imejaa wapagani na inaendeshwa kwa misingi ya kipagani. Gwajima ni mtu wa Mungu na anahubiri kwa uwezo wa roho mtakatifu. Katika biblia kuna amri inayokataza kuua. Hapa ndipo mahubiri ya Gwajima yamejikita kwa kukemea utekaji na mauaji ya raia wasiokuwa na hatia. Na amefafanua vizuri kuwa kama hawo wanaotekwa na kuuawa wana makosa ya jinai, basi wakamatwe wapelekwe mahakamani wafunguliwe mashtaka badala ya kuuliwa na kutupwa kama mbwa mahali pasipojulikana. Kosa la Gwajima ni lipi hapa? Ni kusimamia imani yake ya kiroho?
Ikiwa serikali inaingilia hadi amri kumi zilizomo kwenye biblia zisifundishwe makanisani, basi iifute kabisa biblia takatifu na kutunga biblia ya kipagani iwe inatumika makanisani. Hatuwezi kuvumilia kuona biblia takatifu ya kanisa inasiginwa na wapagani (serikali) tukiwa tumekaa kimya.