Waingereza wamnanga Rais Kikwete!

Waingereza wamnanga Rais Kikwete!

Kwa nin i hawajamtimua mkutanoni aone aibu? watu kama hawa ni kuwazuia mlangon wasiingie
 
Mmmmm, jamani hizo comments hakika zinatuvua nguo watanzania, sitaki kuzisoma tena,
 
labda uwe mvivu wa kufikiri ndipo uungane
na waingereza ambao ktk siku za karibuni tumekataa maombi yao mengi kwani walitaka kumbuluza jk

Hey Mama porojo, Who, in this damn country do you think is gutsy enough to say "NO" to the Britons? Lest you have forgotten, I am reminding you that it is the same guy (JK) who once said I can not turn down the invitations from the British PM, no matter what Tanzanians say about his trips abroad.

Let me tell you, they only man, one and only who could dare say no to absolutely any world leader was the late Mwalimu Julius K. Nyerere, who had the gust of not swallowing his pride and bow down to colonialists.

I bet you are not following the leaders properly and your recording keeping is damned....

Don't tell me, and I don't wanna hear it again that's the fact that we denied the Britons some requests now they are blasting our president as a vengeance...noway...noway.
 
watanzania wenzangu hivi hamjabaini kuwa uhusiano wetu na uingereza unasuasua hata jk kapunguza safari za huko kisa hawataki kukataliwa jambo kila ombi lao wanataka tukubali

Mkuu, kumbe wewe ni m-Tz ???!!!
 
Uchambuzi huu, umenitisha sana na haya mambo tumekuwa tukiyapigia kelele kila siku Bungeni na nje ya Bunge! Sisi tunaonekana mafirauni hasa hawa mafisadi!! Hapa hakuna cha Uccm au Ucdm, sote tushikamane kuokoa taifa letu.....Sitaki wala sikubali upuuzi huu!!! Katika suala la uzalendo siangalii chama wala wala sura ya mtu...natetea maslahi ya Taifa langu na rasilimali zake!!

Ndg wana JF tushikamane katika hili!! AIBU SANA....Ndg zangu taifa letu lilikuwa na heshma mbele ya mataifa mbalimbali, tuliongozwa na sifa za kizalendo, umoja, mshikamano na amani. Rushwa enzi hizo ni mwiko na mataifa mbalimbali wanalijua hilo hakika. Hivi sasa tunanuka tena uvundo....HAPA, naomba kuishia hapa tafadhali, tutapelekana pabaya sasa!!!
Ndugu yangu Sendeka hali ndio hii lakini wengi hawataki kuitambua hapa tz....labda nikuulize swali...are you the Sendeka MP?i mean Christopher Ole Sendeka??kama ni wewe....big up.....ifike mahali sasa kwa kweli MPs(haswa wa ccm)waamke na kupigia kelele ufisadi kwa matendo yaani.......hivi wanajisikiaje wabunge wanapoenda kwenye majimbo yao na kuona watu wao wanavyoishi hovyo???...ifike mahali watanzania kila mtu kwa nafasi yake apambane na huu ugonjwa wa ufisadi kwa matendo jamani......leo hii tz eti rais anatoa amnesty kwa wezi wa EPA eti walirudisha fedha (wote wanajulikana serekalini)walizokwiba!!alafu wabunge wanaenda bungeni wanakaa vikao wanaona hili sawa???lo hii mtu mwizi anapata ubunge tz na watu wanaona sawa tu...tena wengine wanawapigia hata kampeni za urais!!! ndugu zangu iko siku maskini wa nchi hii wataamka na itakuwa mbaya saaana yaani.....hukumu yao itakuwa kiyama yaani..........
 
sendeka ana uchungu kweli.....hahahaha.siku hizi hakuna mshikamano mkuu....lakini uweli utabaki pale pale..katika mkutano wa davos kikwete ameliaibisha taifa
 
Uchambuzi huu, umenitisha sana na haya mambo tumekuwa tukiyapigia kelele kila siku Bungeni na nje ya Bunge! Sisi tunaonekana mafirauni hasa hawa mafisadi!! Hapa hakuna cha Uccm au Ucdm, sote tushikamane kuokoa taifa letu.....Sitaki wala sikubali upuuzi huu!!! Katika suala la uzalendo siangalii chama wala wala sura ya mtu...natetea maslahi ya Taifa langu na rasilimali zake!!

Ndg wana JF tushikamane katika hili!! AIBU SANA....Ndg zangu taifa letu lilikuwa na heshma mbele ya mataifa mbalimbali, tuliongozwa na sifa za kizalendo, umoja, mshikamano na amani. Rushwa enzi hizo ni mwiko na mataifa mbalimbali wanalijua hilo hakika. Hivi sasa tunanuka tena uvundo....HAPA, naomba kuishia hapa tafadhali, tutapelekana pabaya sasa!!!


mheshimiwa hali ndo hiyo...nchi imekosa dira kabisa sasa hiv kila mtu anatusema vibaya........chanzo cha yote haya ni kuwa rais mbovu
 
wewe yawezekana una matatizo ya akili, pamoja na ushaidi wote huo unaendelea kutete ujinga, kashifa zote juu ya serikali unaona ndo maisha bora anayopata mtanzania? Au na wewe ni mmoja wa mafisadi. Kaka tafakari!

nina mpango wa kutafsiri hizi comments na kuzisambaza kwa watanzania!
 
naomba tusome hizi comments objectively na tujifanyie assessment kuona where we stand as a nation coz chochote kinachosemwa kuhusu mzazi wako kinakuhusu pia
 
Mimi siamini kama ni kweli maoni haya yana uhusiano na kuburuzana au kuna maombi yao yamekataliwa, huyo jamaa ameongea ukweli na ingawa amempiga dongo Mheshimiwa Rais wetu, lakini ukweli upo wazi na kila mtu anayeupenda ukweli hawezi kuhusisha maoni hayo na chochote nje yake, ni maoni yanayojitosheleza kabisa, sisi ni mabwege, namaanisha viongozi wetu mishipa ya aibu imekatika, na sisi wananchi pia inawezekana tuna uoga wa virungu uliopindukia, Mungu tujaalie.
Mmmh, ukisoma zaidi comments zilizoendelea, wengine wamefikia hata kumwita Kikwete ni "Retards" Nimesikia hadi aibu kuisoma hii comment.
 
w3w.jpg


Kwanini kila Mwaka wa huu Mkutano Rais Wetu anajipeleka kwanini asipeleke mtu mwingine wa Tanzania wasikie mawazo Mengine ya Watanzania? angalia Kenya wana Waziri Mkuu wao Raila Odinga Oginga; Nigeria wana Waziri wa Fedha wao Ms Ngozi Iweje... Hawezi kubebe nchi Mwenyewe yeah anaweza kwenda nje kama atakavyo anapenda nje...
 
Mheshimiwa Sendika kuanzia sasa tambua wazi kuwa ukiwa kama sehemu ya kiongozi huyu nawe umevuliwa nguo!
 
Kwanini kila Mwaka wa huu Mkutano Rais Wetu anajipeleka kwanini asipeleke mtu mwingine wa Tanzania wasikie mawazo Mengine ya Watanzania? angalia Kenya wana Waziri Mkuu wao Raila Odinga Oginga; Nigeria wana Waziri wa Fedha wao Ms Ngozi Iweje... Hawezi kubebe nchi Mwenyewe yeah anaweza kwenda nje kama atakavyo anapenda nje...
anatafuta posho ya safari!
 
Nyerere aliwacha mtaji gani? Mimi sizijui.
Kwani wewe ni Kipofu?kwani hizo Rasilimali kama Dhahabu,Tanzanite,Uranium,Nyumba za watumishi wa Umma zilizouzwa nk nk huoni huvo vyote kama ni Mtaji?
 
Ndugu yangu JF, rais JK Mrisho ni rais wetu katika nchi yetu. Kusema kweli yeye ni handsome wala hilo halina ubishi, hata yule kijana wa Malkia wa Sheba hamfikii kwa uzuri. Kikwete anatoka nchi tajiri kuliko nchi zote za Ulaya, na hilo wazungu wanalifaham...lakini
  1. Kahudhuria mkutano huo uliokuwa na audience ya karibia wazungu wote! Kwanini wazungu wanalifuatilia sana sasa bara jeusi walilolikwibia hadi likachakaa?
  2. Mh Kikwete anaweza kuongea kiingeredha vizuri na kujieleza, tatizo lake kubwa ni kuelewa masuali yanayoulizwa papo kwa papo
  3. Mh Kikwete analo tatizo la pili kubwa sana, hana mtiririko wa logic, ni kama anaimba mashairi yasiyotoka moyoni mwake...
  4. Kusema kweli karibu viongozi wenziye wote walikuwa wakimwonea wivu kuweza kuongoza nchi tajiri, kubwa na yenye historia kubwa wakati ufahamu wake ni kidogo kiasi hicho
  5. Ameshindwa kujibu suali aliloulizwa kwamba: .. how quickly can you move IT education forwad in Africa... Kwakweli kuna wakati alikosa confidence hadi nikamhurumia. Mwisho wa siku hakuweza kujibu lile suali na akatoa maelezo ya miundo mbinu ya kuunganisha Burundi, Rwanda na Kongo na kuwakaribisha ofisini kwake kuja kuwekeza humo...
Tuseme ule ukweli, mheshimiwa rais angeweza kumtuma mtu mwingine pale kama Prof Lipumba, Mkapa au Mh Zito..hao wangeweza kufanya vyema zaidi.

Viongozi wenziye wamefanya vizuri zaidi. Zuma alikuwa ameandaa notice kama Kikwete lakini aliongea point na logical na akawa kama ni rais wa Africa yote. Siku zote nilikuwa namdharau sana yule mzee polygamist kumbe kichwa kumekaa vizuri. Rais Conde naye ameongea kwa lugha ya ki-Faransa lakini anafaham bara la Afrika linahitaji nini kwa sasa. Ameongea vizuri sana. Zenawi wa Ethiopia ana confidence ya kufa mtu, anajuwa kinachohitajika Afrika, amewapa ngumi za usoni wazungu live, ila alikosea kitu kimoja kwa kutowa maelezo yanayoonesha kungojea flow of ivestment directed to Africa baada ya Asia kutosheka...


Laira pia amefanya vizuri, alikuwa na confidence na flow, hakuwa na reading notice lakini aliniudhi kwa kueleza kuwa tunahitaji kusomesha watu ili kuvutia uwekezaji? Mimi siyo mchumi ... huenda alikuwa sahihi kwa wanauchumi, sijuwi. Na kuna wakati alisema kuwa the Arab spring is coming down south very fast if iclusivity and transformation is not implemented in our countries.. na hii aliisema kabla Mh Kikwete hajazungumza..

Huo ndio mtizamo wangu. Kwakweli Mh Kikwete kama anaweza kusoma upepo wa dunia na upepo wa ndani ya nchi yake anatakiwa kubadilika, kujifunza na kufanya kitu muhimu... vinginevyo ama ataishia kuwa kicheko baada ya utawala au huenda hatamaliza vizuri, ama nchi itaishia pabaya.
 
jk aliwakatalia ombi lao la kuwekeza kwenye urenium na kuleta balozi shoga llazima wamtukane kulipa kisasi

Acha ujinga wako, hivi kwanini hamtaki kukubali mnapoambiwa ukweli? Hakuna uhusianoa kati ya omba omba ya Kikwete na kuwakatalia balozi wao shoga kuja Tanzania; Mkweree ni omba omba kwasababu ana kichwa mfu na hivyo hana vision ya kuongoza nchi period.
 
mh?Ukweli unauma jamani,....JK mwenyewe aliwahi kusema mtu mzima ukivuliwa nguo basi chuchumaa.
 
Mhhhhh!
Hapo hakuna lakuongeza!
Baba yako mzazi anapotukanwa na jirani mbabe inabidi mtoto ukauke kama vile hujasikia kitu!...ngoja tuuchune kama hatujaona vile!
 
Back
Top Bottom