Wahusika Fanyeni Mengine Biashara Hii ni Ngumu Kuizuia

tatanyengo

JF-Expert Member
Mar 30, 2011
1,134
280
POLISI imeanzisha operesheni kaMambe ya kupambana na biashara ya ukahaba Mji wa Moshi na tayari wanawake zaidi ya 150 wanaouza miili yao wametiwa mbaroni.

Vifungu 145,146 na 147 vya kanuni ya adhabu cape 16 kama vilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, vinaharamisha biashara ya ukahaba siyo kwa mwanamke tu, hata mwanamme anayefanya nao mapenzi.
Ingawa vifungu hivyo havijaweka adhabu, lakini vikisomwa pamoja na kifungu namba 35 cha sheria hiyo, inatamka bayana kuwa mtuhumiwa anaweza kufungwa miaka miwili jela, faini au vyote viwili.


Pia, chini ya sheria hiyo anayegeuza nyumba yake au chumba chake au eneo lake kwa njia yoyote ile ili litumike kwa shughuli za ukahaba, anatenda kosa na anaweza kufungwa hadi miaka miwili jela.


Hata hivyo, baadhi ya wanawake hao wamekuwa wakifikishwa mahakama ya mwanzo na kushtakiwa kwa kosa la uzururaji, kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa moja kwa moja wa kosa la ukahaba.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa kutokana na kashkashi hiyo, wanawake hao sasa wamebuni mbinu mpya ambapo huingia ndani ya klabu hizo na kukaa kama wateja wakiwa na chupa za bia zenye maji.


Baadhi ya wateja wakiwamo wanaume walioko kwenye ndoa, nao wamebuni mbinu mpya ambapo ‘humalizana’ na wanawake hao kwenye magari wanayoegesha kwenye giza nje ya klabu hizo.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alithibitisha kuendelea kwa operesheni hiyo akisema ilianza wiki nne zilizopita na itakuwa endelevu hadi vitendo hivyo vitakapokoma.
 
UJASIRIAMWILI siku hizi ndo biashara/ ajira isiyohitaji MICHETI MIZITO, KUJUANA, TAJI MKUBWA. Mtu akiamua tu anaanza business!!!! Mungu tuipshie!!!!
 
Mmmh.
Ukiona hivyo ujue wateja wako wengi ndio maana biashard ya ukahaba imeshamiri.
Serikali haina budi kuihalalisha tu kwani ni moja ya vyanzo vya mapato kwa watz.
 
Badala ya kupambana na matakataka sokoni kule na upungufu wa maji safi wanaleta longolongo. Kuna mnunua kahaba anabakwa ama wanaenda na hela zao mkononi?
Polisi wakikosa maandamano ya chadema wanaanza kukosa kazi na kufanya vitu hovyohovyo!
 
UJASIRIAMWILI siku hizi ndo biashara/ ajira isiyohitaji MICHETI MIZITO, KUJUANA, TAJI MKUBWA. Mtu akiamua tu anaanza business!!!! Mungu tuipshie!!!!
umenena mkuu mkuu babaaa! Mkuu maqumazan! Hii biashara haizuiliki na wala haitoweki kirahisi ktk jamii. marekani pamoja na na kuwa na aina kumi na moja ya jeshi la polisi, nao wameshindwa kuwabana . Huko Ulaya wameamua kuhalalisha.

Ukienda mexico na latin america yote kila hoteli unayolala kuna directory zenye majina na simu zao . wewe unanyanyua simu na kuita toto linakuja bila wasi x 2! Tanzania hatuna haja ya kuhalalisha maana ndoa nyingi sana zitavunjika. Polisi waendelee kuwabana bana tuu ili nao waone kuwa wafanyacho si kizuri.

hii yote ni ukosefu wa ajira kwa vijana na watu kuingia ktk ulimwengu wa materialism. Hii biashara ya ngono itafikia mahla pabaya kama serikali ikizidi kukaa kimya. Maana watajitokeza watu waitwao Pimp daddy na kuanza kumili wanawake kwa kuwauza kwa pesa. maana Pimp dady wao huiba sana wanawake wenye umri mdogo na kuwalazimisha kuuza miili yao kwa pesa. Utakuja kuta hata kupata ma house girl ni vigumu kama pimp dady wakiingia vijijini.
 
mmmh, kiboko yake ni kumuuzia bosi wao tu, badala ya kukukamata wanapiga saluti.
 
hapa bongo jao makahaba walishamwambia KOVA hawawezi naona kawashindwa...
labda hao wa kilimanjaro wanadhibitika.....
 
Wanatumia vigezo gani kuwakamata? Kuna watu wapo maofisini wana kazi zao na bado mwili anauza.... Hao pia wanastahili kukamatwa?
 
i propose the formarion on an wlite group called lords eradication of vices group. hapa kamata kahaba na adhabu ni kufanya ngono na wanyama
 
Back
Top Bottom