Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,195
- 10,709
Miaka ya nyuma niliwahi kukutana na Naibu Waziri wa Fedha huko Dodoma kwenye kongamano moja la vijana kuhusu masuala ya fedha. Nilipata wasaha wa kuzungumza naye mawili matatu kuhusu mambo ambayo yeye yapo kwenye wizara yake.
Katika jambo ambalo nilipata wasiwasi ni kuhusu mfumo wa kodi, Mfano, Ukiwa mfanyakazi unakatwa kodi, pesa yako ya mshahara inaingia katika mfumo wa benki ambapo ili uweze kuitoa lazma kuna makato ya kiserikali katika muamala husika, ukinunua bidhaa unakatwa kodi, ukilipia umeme, pamoja na Maji unakatwa tena kodi.
Ukisema utume pesa kwa wazee kijiji wapate kuona matunda ya kijana ama binti yao, bao makato yanakuhusu.
Wenzetu Wahindi wameanza kuhoji kuhusu utitiri wa kodi ambazo kimsingi ni kodi za kijinga zisizo na tija yotote. Tunaposikia kuwa Mamlaka ya TRA imevunja rekodi ya makusanyo ya kodi inatakiwa iwe neema kuwa miradi ya maendeleo itakwenda kuwa bora na maisha ya watu kuwa mazuri kwa hatua fulani.
Wenzetu wameanza kuhoji kuhusu utaratibu huu ambao kwa wananchi wenye utimamu wanauona ni mfumo wa kuwanufaisha wachache. Je sisi tumeridhika ama tunasubiria mpaka tutoke usingizini?
Katika jambo ambalo nilipata wasiwasi ni kuhusu mfumo wa kodi, Mfano, Ukiwa mfanyakazi unakatwa kodi, pesa yako ya mshahara inaingia katika mfumo wa benki ambapo ili uweze kuitoa lazma kuna makato ya kiserikali katika muamala husika, ukinunua bidhaa unakatwa kodi, ukilipia umeme, pamoja na Maji unakatwa tena kodi.
Ukisema utume pesa kwa wazee kijiji wapate kuona matunda ya kijana ama binti yao, bao makato yanakuhusu.
Wenzetu Wahindi wameanza kuhoji kuhusu utitiri wa kodi ambazo kimsingi ni kodi za kijinga zisizo na tija yotote. Tunaposikia kuwa Mamlaka ya TRA imevunja rekodi ya makusanyo ya kodi inatakiwa iwe neema kuwa miradi ya maendeleo itakwenda kuwa bora na maisha ya watu kuwa mazuri kwa hatua fulani.
Wenzetu wameanza kuhoji kuhusu utaratibu huu ambao kwa wananchi wenye utimamu wanauona ni mfumo wa kuwanufaisha wachache. Je sisi tumeridhika ama tunasubiria mpaka tutoke usingizini?