Wahindi na utumwa mambo leo

ABUMAN

Member
Dec 8, 2010
52
7
UNYONYAJI NA UTUMWA MAMBOLEO UNAOFANYWA NA WAHINDI KWA WATANZANIA WASIO WAHINDI
WAHINDI NA UFISADI WA RASILIMALI WATU.

Napenda kuchukuwa fursa hii adhiim kuwatanabaisha Watanzania hasa mawaziri wa wizara husika juu ya madhila yanayotokana na ndugu zetu Wahindi kwa Watanzania wenzao ambao si Wahindi.Hili lisipofanyiwa kazi sikumoja yatatokea kama yale yaliyowahi tokea afrika ya kusini,mara baada ya wazawa kuona nafasi za kazi nyingi wanapewa wageni na wao wakishinda vijiweni wakati sifa na uwezo wa kufanya hizo kazi wakiwa nao.

Siku hizi imefikia wakati inatangazwa nafasi ya kazi kama ilivyotokea katika kampuni moja ya madawa Tanga ambayo iliorodhesha miongoni mwa sifa ya mwombaji awe anajua kuzungumza kihindi,sasa huo kama si ubaguzi nini hasa. Serikali inahitajika kuwaandalia sera Wananchi wake amabayo itapelekea kuwawezesha kupata kazi wao katika makampuni mbali mbali ya wawekezaji kutokana na sifa zao za kitaaluma na uwezo wao, na pasiwepo mgeni kutoka nje kuchukua nafasi ya kazi ambayo wapo Watanzania wenye sifa na uwezo wa kuifanya hiyo kazi tena kwa ufanisi mkubwa.

Kwa kufanya hivyo Serikali itakuwa inalinda soko la ajira kwa kutoa kipaumbele kwa Wananchi wake kwanza na pakikosekana mwanachi mwenye sifa ndani ya Tanzania paangaliwe kwa Watanzaniia walio nje na hapo pia pakikosekana ndio angaliwe raia wa kigeni,hili pia litaweza kuepusha athari za Wahindi kuitawala Tanzania kama sehem zinazoshikilia uchumi wa nchi yetu zitakuwa zimeachwa zote ziwe mikoni mwao kama inavyotokea kwa baadhi ya mataifa.

Wahindi kwa maelfu wamejazana katika ofisi nyingi hasa za Makampuni ya Wahindi wenzao au ya waarabu,ni nadra kwa Mhindi kukutwa katika ofisi ya Mzungu au Muafrika kutokana na kutokubalika kwa hulka zao hasa hulka ya fitna,Wahindi wanaubaguzi uliochupa mipaka na wanapendelea sana fitna na majungu kiasi kwamba kila ambaye ameshawahi kufanya kazi katika kampuni inayomilikiwa na Wahindi au kuwa na wafanyakazi Wahindi ataungana na Mimi.

Utakuta mfanyakazi asiye Mhindi anatumika kama Mashine na si kama Binaadam, hatakiwi kupata mapumziko ya haina yoyote akiwa kazini,hatakiwi kula wala kwenda msalani,na kazi yoyote nzuri basi hiyo imefanywa na Mhindi na hata kama imefanywa na asiye Mhindi na kazi yoyote ile yenye mwishilio mbaya hata kama imefanywa na Mhindi atatafutwa wa kusukumiwa nayo Mhindi huwa ni mtu kamili hakosei,kuna kampuni moja ya Wahindi ipo katika barabara ya Nyerere ukipita muda wa asubuhi wale wafanyakazi wasio wahindi wanakunywa chai wakiwa wamesimama tena wakiwa nje na hiyo chai wanahudumiwa na Mama ntilie kupitia nje ya uzio Wahindi wakiwa ndani.

Kuna kazi nyingi za kitalaam zinafanywa na wasio Wahindi ila pesa anayolipwa huyo aliyoifanya ni ndogo ukilinganisha na pesa inayoingia katika kampuni hiyo ya Wahindi, na hili linatokana na mizengwe ambayo Wahindi wengi wamekuwa wakiitoa,kwa sasa Tanzania karibu taaluma zote zimevamiwa na Wahindi ni taaluma chache sana ambazo bado zimesalimika kwa kiasi fulani ingawa si sana.

Wahindi wengi wanatumia vyeti vinavyotia mashaka katika kujipatia kazi za kitaalam na hili limefanya baadhi ya nchi za mashariki ya kati wameanza kukataa wafanyakazi toka India kutokana na utumiaji wa vyeti hivyo,na katika hili Serikali inahitajika kulifuatilia kuhakiki hivyo vyeti na hili linawezekana kwa kuwatumia watanzania waadilifu kuandaa sera hiyo na kuisimamia, kwani uhakiki wav yeti kama unafanyika katika taasisi za umma lengo na madhumuni ni kuwa na watu waliokabidhiwa majukumu ambao na sifa na uwezo kutekeleza hayo majukumu kwa ustawi wa taifa letu na kwa kuzingatia mchango wa taasisi binafsi katika ukuaji wa taifa ni muhimu kwa serikali kulifanyia kazi hili.

Taaluma ambayo imeathirika sana na wafanyakazi kutoka India ni taaluma ya habari na mawasiliano na tatizo hili linawakosesha Watanzania wengi wenye sifa kupata ajira,tatizo lengine ni la kampuni nyingi za Wahindi kutozingatia na kufuata sheria na kanuni za ajira,na hata ikitokea wafanyakazi wakafuatilia watu wa wizara husika wakija katika kampuni husika moja ya hulka ya Kihindi ya mizengwe inatumika na Watanzan
 
Kaka wa kulaumiwa sio wahindi bali ni sisi wenyewe wamatumbi,ebu niambie pale uhamiaji wanapotoa vibali kuna wahindi?,je TRA kuna wahindi,na jde walio ua viwanda ambavyo wamatumbi walikuwa ndio mabosi na hata tulikuwa tunakunywa chai kwenye kantini je ni wahindi,asu hata migomo ya madakitari je ni wahind,na hata wanunuzi wa bidhaa zinazo tengenezwa na wahindi sio wahindi bali ni sisi wenyewe.\kwa kifupi yote hayo yametokana na sisi wenyewe,bila sisi wahindi wasingekuwa na jeuri ya kuyafnya hayo wanayoyafanya ,na kwa taarifa muda si mrefu watakuwa wachina ndio wameshika usukani walianza kidogo kidogo sasa tunao hata Manda,ukiwa pale airport kila ndege zikishuka hazikosi wachina ambao wanaingia(hawatoki

/
 
kulaumu kundi chochote - iwe wahindi, wachagga, wahaya nk ni ishara ya fikra ya kibaguzi. Kuna wahindi, wachagga na wahaya ambao wapo katika hali mbaya. Tulaumu wale walio katika uongozi ya nchi wala rushwa. Rushwa ni adui wa haki. Yote ambayo yanatokea ni kwa sababu ya rushwa. Tuache fikra ya ubaguzi. Tuna wezi wa kila rangi na kila dini na kila kabila nchini. Adui ni mwizi na si mtu wa kabila, dini au rangi fulani.
 
Back
Top Bottom