Wakuu bajeti inapowasilishwabungeni huwa ni kama hitimisho lamchakato mrefu na wa kisayansi ambao umehusisha wadau wengi sana na zaidiwaheshimiwa wabunge wenyewe. Kamati za kudumu za bunge hupitia bajeti za wizarahusika . Katika vikao baina ya kamati ya kudumu ya bunge na watendajiwaandamizi wa wizara husika wakiongozwa na waziri wao. Waziri huwasilisha rasmuya bajeti ya wizara yake, wabunge huuliza maswali na kutaka ufafanuzi katikamambo ambayo wanadhani hayaeleweki vizuri kwao. Lakini pia wabunge hutoamapendekezo kadhaa ambayo yanaingizwa moja kwa moja katika bajeti.Kamati ya kudumu ya bunge yafedha na uchumi ina jukumu la kuipitia bajeti kuu ya serikali katika kikao chapamoja baina ya watendaji waandamizi wa wizara ya fedha na wajumbe wa kamati yafedha ya bunge. Kwa msingi huo bajeti inayoendelea kujadiliwa bungeni hivi sasainafahamika vema kwa wabunge wote na wote wameshiriki katika kuiunda kutokanana michango ya wabunge katika vikao baina ya wabunge na watendaji wa serikali.Hii ndiyo sababu nikasema tangu mwanzo kuwa bajeti ni mchakato mrefu ambao umehusisha wabunge kwa kina kablahaijawasilishwa bungeni. Kila mbunge anaruhusiwa kuhudhuria vikao vya kamatiyoyote ya bunge hata ambayo haimhusu lengo likiwa ni kumpatia fursa kila mbungekujua kwa kina kinachoendelea serikalini.Jambo la kushangaza ni jazbainayoonyeshwa na wabunge wa pande zote wakati wa kujadili bajeti hii as if nijambo wanaloliona kwa mara ya kwanza. Wabunge wanatumia nguvu nyingi kupinga bajeti hii ilhali walipata fursaya kuipitia kwa kina kabla haijawasilishwa bungeni, huu ni usanii wa kiwangocha juu sana. Hivyo wabunge wetu acheni usanii hii bajeti mnaijua vema namlishaipitia kabla haijawasilishwa bungeni.