Wahaya, wamebarikiwa sana kutunza elimu kubwa katika majina yao.

Manton

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
1,164
1,520
Wahaya ni kikundi cha watu wenye akili sana wanaopatikana katika mwambao wa ziwa Rwelu (Victoria) Magharibi. Mbali na kusambaa kwao dunia kote katika harakati za kuongeza ujuzi na wigo mpana wa maarifa, wamefanikiwa kutunza elimu kubwa katika majina yao, kwa mfano: 1. TIBAIJUKA; liki maanisha, hata watu uwatendee mazuri kiasi gani, daima uwa hawakumbuki chochote kile, japo washukuru tu. 2.TIBESIGWA; umaanisha watu hawaaminiki hata kidogo, chochote ufanyacho usije mwamini mtu. 3.TIBEMOGA, umaanisha watu uwa hawajirudi katika yale wanayokusidia kumtendea mwenzao kwa ubaya. 4. TIBASIIMA, yaani hata watu uwafanyie mema kiasi gani kamwe hawatoshukuru. 5.TIBEKANASHA, umaanisha watu walionuia kutenda jambo lolote kwa nia moja uwa hawakati tamaa hata wakishindwa mara kwa mara katika majaribio yao, mpaka wafikie hatima ya lengo lao. ZINGATIA: hayo ni baadhi tu ya majina, yapo maelfu ya majina. Tuwapongeza Wahaya kwa kuenzi elimu katika vizazi vyake kwa njia ya majina. Karibu, utoe mchango wa mawazo ya nyongeza.
 
Mlokozi jee?
Nina bahati ya kua na marafk wakubwa wawili wa kihaya na wote ni majina ya mlokozii...
Kariba yaooo
alooo wana sound sijapata onaaaa, km una msimamo wako ktk jambo usimpe hata dk ya kuongeaa...

Sent from My iphone 11 Pro Max, nimeinunua jana pale karume karibu na duka la mapajama.
 
TIBAIGANA; Inamaanisha chukua/pora kwa mabavu!
KOKU ; Igawe bila hiyana
ISHENGOMA; Mtu wa kwanza kuanzisha katerero
KAMGISHA; Kamwanamke kamoja ifwact ni uzembe!
RWAIZAURA; Kadri anavyotanua ndivyo raha inapatikana au siyo
 
wahaya wameendeleza ukabila kupitia code za majina..hawa watu huwa siwaelewi kabisa... (all in all shemeji yenu mhaya lakini)
 
Mlokozi jee?
Nina bahati ya kua na marafk wakubwa wawili wa kihaya na wote ni majina ya mlokozii...
Kariba yaooo
alooo wana sound sijapata onaaaa, km una msimamo wako ktk jambo usimpe hata dk ya kuongeaa...

Sent from My iphone 11 Pro Max, nimeinunua jana pale karume karibu na duka la mapajama.
Mulokozi, umaanisha muokozi ama mkombozi.
 
TIBAIGANA; Inamaanisha chukua/pora kwa mabavu!
KOKU ; Igawe bila hiyana
ISHENGOMA; Mtu wa kwanza kuanzisha katerero
KAMGISHA; Kamwanamke kamoja ifwact ni uzembe!
RWAIZAURA; Kadri anavyotanua ndivyo raha inapatikana au siyo
TIBAIGANA= hawalingani (watu). KOKU- ni prefix ya jina la kike mfano. KUKUMARAMARA= Wakuliwaza. ISHENGOMA; Jina la pacha wakiume.KAMUGISHA=wabaraka tele. RWEZAURA= Takaso.
 
wahaya wameendeleza ukabila kupitia code za majina..hawa watu huwa siwaelewi kabisa... (all in all shemeji yenu mhaya lakini)
Ukabila ni ngano ya kisiasa ambayo imebeba hisia hasi kwa walio wengi, kuwa ni hali ya ubaguzi wakati huo wanasahau ya kwamba jasiri haachi asili yake.
 
TIBAIGANA; Inamaanisha chukua/pora kwa mabavu!
KOKU ; Igawe bila hiyana
ISHENGOMA; Mtu wa kwanza kuanzisha katerero
KAMGISHA; Kamwanamke kamoja ifwact ni uzembe!
RWAIZAURA; Kadri anavyotanua ndivyo raha inapatikana au siyo
Huwezi kuwa hujalewa.Tibaigana ni hawalingani,Koku ni kifupi cha jina kikiongezewa maneno ya mwisho ndio linaleta maana sawia ila tu ni kaku....pendwa,Kubeba,kupamba etc Ishengoma ni Mtawala au mwenye madaraka ni jina apewalo pacha wa kwanza kuzaliwa ,mwanaume
 
Wahaya ni kikundi cha watu wenye akili sana wanaopatikana katika mwambao wa ziwa Rwelu (Victoria) Magharibi. Mbali na kusambaa kwao dunia kote katika harakati za kuongeza ujuzi na wigo mpana wa maarifa, wamefanikiwa kutunza elimu kubwa katika majina yao, kwa mfano: 1. TIBAIJUKA; liki maanisha, hata watu uwatendee mazuri kiasi gani, daima uwa hawakumbuki chochote kile, japo washukuru tu. 2.TIBESIGWA; umaanisha watu hawaaminiki hata kidogo, chochote ufanyacho usije mwamini mtu. 3.TIBEMOGA, umaanisha watu uwa hawajirudi katika yale wanayokusidia kumtendea mwenzao kwa ubaya. 4. TIBASIIMA, yaani hata watu uwafanyie mema kiasi gani kamwe hawatoshukuru. 5.TIBEKANASHA, umaanisha watu walionuia kutenda jambo lolote kwa nia moja uwa hawakati tamaa hata wakishindwa mara kwa mara katika majaribio yao, mpaka wafikie hatima ya lengo lao. ZINGATIA: hayo ni baadhi tu ya majina, yapo maelfu ya majina. Tuwapongeza Wahaya kwa kuenzi elimu katika vizazi vyake kwa njia ya majina. Karibu, utoe mchango wa mawazo ya nyongeza.


Katika suala hilo hawana tofauti na wazaramo, Wazaramo utasikia majina ya watoto wao kama, Shida, Tabu, Nyama yao, Mtupeni, Mpigeni, Msemeni, kikulacho, kimavi nk,.

Ni majina ya "Mipasho na umbea" tu, na katika dunia ya leo ya watu waliostaarabika mipasho na umbea kwa kupitia majina haina maana yoyote, tena mipasho ya kuendelea kwa kadiri mtu atakavyoishi.🤣🤣
 
Wahaya ni kikundi cha watu wenye akili sana wanaopatikana katika mwambao wa ziwa Rwelu (Victoria) Magharibi. Mbali na kusambaa kwao dunia kote katika harakati za kuongeza ujuzi na wigo mpana wa maarifa, wamefanikiwa kutunza elimu kubwa katika majina yao, kwa mfano: 1. TIBAIJUKA; liki maanisha, hata watu uwatendee mazuri kiasi gani, daima uwa hawakumbuki chochote kile, japo washukuru tu. 2.TIBESIGWA; umaanisha watu hawaaminiki hata kidogo, chochote ufanyacho usije mwamini mtu. 3.TIBEMOGA, umaanisha watu uwa hawajirudi katika yale wanayokusidia kumtendea mwenzao kwa ubaya. 4. TIBASIIMA, yaani hata watu uwafanyie mema kiasi gani kamwe hawatoshukuru. 5.TIBEKANASHA, umaanisha watu walionuia kutenda jambo lolote kwa nia moja uwa hawakati tamaa hata wakishindwa mara kwa mara katika majaribio yao, mpaka wafikie hatima ya lengo lao. ZINGATIA: hayo ni baadhi tu ya majina, yapo maelfu ya majina. Tuwapongeza Wahaya kwa kuenzi elimu katika vizazi vyake kwa njia ya majina. Karibu, utoe mchango wa mawazo ya nyongeza.
Vyoo bora 7.7%
 
Wanyiramba na wanyaturu njooni hapa. Wanyakyusa kaeni kimya.
Wamakonde semani maana ya Nyerere. Chipoku. Chupaki, Dabgote, Hechiaivii. Kombyuta. Bachikeli. Aitiivii.
 
Majiko je, ni asilimia ngapi? Unaanzaje kushupalia takwimu za kutathimini ubora wa vyoo kama hujui wanapika au la?
Takwimu hupingwa kwa takwimu
Vyoo bora kwenu ni chini ya 10% mtu amejenga nyumba lakini anatumia choo Cha majani ya migomba
Au nyumba lkn ndani katandika manyasi hahaha
 
Mkuu, Luambo Makiadi, Siyashangai sana maneno yako; maana wapo watu mpaka lao wana amini kila kitu kizuri lazima kiendane na viwango vya mzungu.
 
Takwimu hupingwa kwa takwimu
Vyoo bora kwenu ni chini ya 10% mtu amejenga nyumba lakini anatumia choo Cha majani ya migomba
Au nyumba lkn ndani katandika manyasi hahaha
Hivi ukipewa kazi ya kujenga choo cha majini ya migomba, huko Ulaya katika ya jiji lolote mashuhuri ulimwenguni, itakugharimu dola ngapi, kukamilisha? Umaskini tunautengeza wenyewe katika fikra zetu.
 
Back
Top Bottom