Wahadhiri vyuo vikuu vya umma kugoma

Kugoma kwa ajili ya maslahi yako binafsi sio jambo la kiungwana wala kishujaa, these people are self centred.

Watanzania wangapi hawana uhakika wa kula, watanzania wangapi wanakosa matibabu kwa ajili hawana pesa za kulipia matibabu, watanzania wangapi hawana ajira, watanzania wangapi wanashidwa kuwalipia school fees+uniforms watoto wao. Sasa hawa wasomi wenye mishahara mizuri na wengi wao wamesomeshwa bure na Watanzania hawa masikini bado wanagoma eti pension zao ziboreshwe ndio watafanya kazi(kazi ya kulipwa sio bure).

Mimi nilitegemea hawa wasomi wange goma siku nyingi hasa wakati serikali inaondoa sera ya free education kwenye higher institutions. Hawa wasomi nilitegemea wangeweza kubuni mikakati kabambe ya kuondoa umasikini uliokithiri kwenye nchi yetu na kugoma kama serikali ingeshindwa kuitekeleza, sasa hawa tunaotegemea wasaidie Taifa hili nao wanagoma tena kwa ajili ya manufaa yao binafsi. Hii ni hatri kubwa.
Mkuu ni lazima kwanza uzingatie jinsi mfumo mzima wa Kibepari Unavyofanya kazi kabla hujalaumu watu.. Ule Mpango wa kijamaa wa kugoma kwa maslahi ya mtu mwngine ama kundi jingine haufanyi kazi ktk Ubepari..Kila mmoja wetu ktk makundi yetu atasimamia kwanza maslahi yake na wewe unaweza kuwaunga mkono ama kupinga kulingana na tatizo lenyewe..

Hata siku moja usije tegemea kwamba mkulima atakuja tetewa kwa ngomo na mfanyakazi, ama tatizo la wanafunzi kushughulikiwa na wahadhiri hali wao wenyewe kula yao inatokana na wanafunzi..Ubepari ni biashara, ni mfumo wa biashara kwa maslahi ya wote hivyo Ubepari kwanza unawagawa watu kwa makundi kisha wanaanza kujitafuna wenyewe, mwenye nguvu ndiye ata survive..hali Ujamaa unalenga kuwa shida ya mwenzako ni shida yako pia, kwa umoja wenu mnaweza kukabiri tatizo la jirani yako kwa pamoja.

Kilichofanyika ni halali na safi sana.... hili ni somo jipya kwa makundi mengine kujitambua kuwa kila mmoja wetu kaubeba Msalaba wake. Na Uzito wa mzigo huo utajulikana tu ikiwa mbebaji atapiga kelele za kushindwa na kuutua mzigo huo...
 
Wahadhiri wangelitusaidia sana hapa kufanya analysis siyo ya kwao tu, lakini hasa kutafuta tulipokosea ni wapi ili kila kada ipate haki zake inazostahili.

Mheshimiwa swala la wahadhiri kutoa analysis lina ugumu sana kwani mazingira yaliyopo yamefanya academia i operate in a vacuum....

Kazi zao hazijapewa umuhimu na badala yake wengi wamegeuka kuwa research assistant wa nchi zilizoendelea kwa faida ya nchi hizo na si taifa ambalo ndilo lilitakiwa kupata mwongozo na faida toka kwao. Sasa wanasiasa msipoliona hili na mkaendelea kuweka mafungu kwenye mambo ya siasa na administration (wakati wa budget) then usitegemee wahadhiri waka break the ice.... ni ngumu; they are not politicians they are academicians so if used they can be very useful but if ignored they tend to be dormant and thats what is happening kwa sasa.

Most of academicians are asleep in national issues hasa wale ambao hawajajaliwa kuwa na connections na wanasiasa na si wanasiasa wengi wao wako dormant wameamua kuuza maduka, kufungua baa na hata wengine kujilewea bar... a sign of frustration lakini nobody cares huku taifa linaendelea kuzama katika tope la umaskini na ignorance huku statistics zikitoa projections zisizoendana na uhalisia...

Mtu yuko frustrated unamwambia afanye analysis ipi hiyo? Ya jinsi anavyofuga ngo'mbe na kuku, au kuuza bar au kulewa? Anakumbuka hata maana ya analysis ni nini? Wakati alichelewa kuoa, mtoto wake ndo yuko secondari na mwakani anatakiwa astaafu, kiinua mgongo chake hakitamsaidia huyo mwanae kufika angalau chuo kikuu na akifika chuo kikuu anatakiwa kulipiwa...yet we unaomba huyo mtu akufanyie analysis...

Dr. subiri watakuletea hiyo analysis ni wajuzi kweli wa ku model wata model mpaka wewe utafurahi mwenyewe...kwamba uchumi unakua kwa 18% kwa mwaka na taifa lina uwezo wa kulipa kima cha chini cha mshahara wa 1M yes is that what you want to hear, they are able to enter figures in computers and come up with good projections na watakao kuletea ni wale ambao wanategemea kupata pension through bunge ili kuziba gap wale wenye moral conscious wao pombe kwa kwenda mbele na miradi midogo midogo....
 
...................Tukumbuke haki hizi ni maisha na ni uhai, hivyo hakuna sababu ya kuzitazama kwa msingi wa kiitikadi. tushikamane kutafuta tatizo liko wapi na kwanini haki hizi ambazo ziko wazi zinashindikana kupatikana kwa njia za kawaida? Wahadhiri wangelitusaidia sana hapa kufanya analysis siyo ya kwao tu, lakini hasa kutafuta tulipokosea ni wapi ili kila kada ipate haki zake inazostahili.

........hapo juu tuko pamoja sana Mheshimiwa..........kwa kuwa haya ni maswala ya haki za msingi hivyo basi............fighting in isolation does not help anybody............
 
........hapo juu tuko pamoja sana Mheshimiwa..........kwa kuwa haya ni maswala ya haki za msingi hivyo basi............fighting in isolation does not help anybody............
sasa tushaambiwa wengi wao wana njaa, na kuna too much politics ktk sekta zao for them to conduct independent work. Na waliosalia au tuseme waliojichokea kungoja wameamua kujiunga na mataifa mengine kupata mlo kwa mujibu wa mchangiaji mmoja.

It all make sense na hao waliotaka kugoma. Huwezi kufanya kazi ya maana kwenye academic kama mawazo yako yapo sehemu tofauti na kubaliana na mchangiaji aliesema wanaishia kujilewea tu.

Ni wakati wakupewa priorities, kama mheshimiwa anataka analysis zao serikali inabidi iwekeze kwao. Juzi nimeona kwenye 'you tube' kupitia michuzi serikali imesema inasubiri budget ijayo hili watatue mgogoro. Na hawa nao wameacha mgomo, mbona hiyo serikali haija wahakikishia ni vipi au demand zipi ndizo watakazo watekelezea wao washanyamaza.

Ni lazima na wao sasa wadai wanachokijua au wanachokitaka ki maslahi na si mishahara tu au malupulupu yao. :glasses-nerdy:
 
Mimi nashindwa kuelewa hawa wahadhiri wanachotaka ni nini haswa ? Ninavyojua mimi suala la kiinua mgongo kinaenda kabisa na kiasi unachokatwa kila mwaka, na plan yako -hapa inaweza ikawa NSSF au hiyo ya PPF. Kama hawa wahadhiri wanataka kumove kutoka kwenye plan ya PPF to NSSF nakubalina nao kabisa , na hizo changes zinaweza kufanywa, lakini kama wanataka serikali iwape posho nzito watakapostaafu, wakati kwa miaka mingi wame-enjoy kukatwa hela kidogo ambayo imepelekea wao kuinvest hela kidogo kwenye pension fund yao hiyo ni HAPANA!

Na hata kama serikali itachange plan zao, hizo changes zitakuwa kuanzia hiyo tarehe hiyo sheria ilipopitishwa na kuendelea . Hatuwezi kurudi nyuma na kuwapa kiinua mgongo wasichokilipia.
 
Kufanya kazi kwenye mashirika ya umma/serikalini kuna faida zake na hasara zake...........unapokuwa serikalini kuna utaratibu/kanuni unao-govern maslahi ya watumishi...........bureaucracy zilizopo zina faida zake na hasara zake........."ideally" zimewekwa ili kulinda maslahi ya kila mlipa kodi.................

..........It is unfortunate udhaifu uliopo katika mfumo wa governance yetu wanasiasa wame-capitalise kujinufaisha wao tu............vita hii ya kujiondoa kutoka ktk makucha ya wanasiasa mijizi/mijambazi hatuwezi kuvishinda tukipagana in ISOLATION.............politicians can easily maneuvre staffs........wakituacha tukilia kama mbwa midomo juu as always.............

Felister kule kwenye biashara na uchumi nilipenda sana mchango wako na hasa kwenye suala la sustainability.............vile vile natarajia huku...wasomi wetu watuonyeshe mifano/fikra z/inay/zojenga mapambano ya hakika..............hivi leo kusema eti kwa kuwa wabunge wanapata kiinua mgongo hivi na sisi tupate vile bila kuangalia hili suala na mfumo mzima.........it comes up as very weak fight..........trust me.....they ain't gonna get it............!!
 
Wahadhiri wamekuwa kimya wakati wa saga za wenzao, naamini nao pia wataunganisha nguvu na jamii nzima ili kuunganisha nguvu.
Mheshimiwa nashukuru kwa kutambua umuhimu wa Wahadhiri japokuwa nitofautiane nawe kuhusiana na sualala ukimya la wahadhiri (wa Tanzania). Ukiona nchi ambayo Wahadhiri wa vyuo vya umma wanamigogoro ya kimaslahi na Serikali basi ujue nchi husika ina matatizo ya kisiasa au imejaa wanasiasa wasiojua mambo muhimu ili Taifa liendelee!

Nina hakika utakubaliana nami kwamba hakuna mfumo wa maisha ya kijamii, kisiasa au kiuchumi ambao hauhitaji kufanyiwa utafiti wa mara kwa mara kwa maendeleo endelevu. Ni wazi kwamba wanasiasa (ambao tumewapa kipaumbele kimaslahi) hawawezi kufanya utafiti au/na kutoa maamuzi ya kuisaidia nchi bila kufanya utafiti! Haiwezekana, hata kama unaongoza vichaa, kuendesha maisha ya watu pasipo kuweka miongozo ya kupambanua dira inayokuwezesha kutimiza majukumu yako kwa ustawi endelevu. Swali ni kwamba utawezaje kupambanua mambo kama huna hata 'statistics' za masuala muhimu yanayohusu jamii na uchumi? Hebu jiulize maswala yafuatayo:
- ninyi kama Wabunge mnapata wapi takwimu za kuongea 'facts' mnapokuwa Bungeni iwapo kitengo kama NBS kimechoka na wala hakina 'fund even to outsource researches to keep it up to date'?
- kama NBS imechoka na wahadhiri wanalalamika ninyi mnapata wapi 'guts' za kukaa na kuongea Bungeni ilhali mkijua 'no facts no talk'?
- ain't you, 'in normal sense', gluttonously milking poverty-stricken citizens of URT maana mnachoongea hakina tija kwa ustawi wao?

Swala la wahadhiri kuongea kuhusu "saga za wenzao" sijui unamaanisha nini!!? Lakini, jukumu la kuwafanya wahadhiri waongee mnalo ninyi wanasiasa wa Tanzania hasa ukizingatia kwamba mmejipa nguvu kukiwezesha chombo mnachoona kinafaa. Awali mliamua TRA iwe na nguvu ili isimamie kodi zitazowezesha upatikana wa 'allowances' zenu, tumeona jinsi ilivyofanikiwa. Mkaamua Jeshi liwe na maslahi mazuri kusudi kulinda mkate wenu; uwezi kusikia minong'ono Jeshini tena labda aje mwanasiasa mwendawazimu. Sasa nitajie mahala pengine zaidi ya Bunge ambapo unadhani watumishi wake wanafanya kazi pasipo mkwamo na msuguano wa kimaisha hapa Tanzania?!

Mnatakiwa kuyaongea haya huko Bungeni maana linawafanya hata ninyi muonekane malofa.
 
Back
Top Bottom