Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 303
Wahadhiri wa Vyuo Vikuu vya umma nchini wametangaza kuanza mgomo kuanzia Aprili 27, mwaka huu. Hatua ya wahadhiri hao imefikiwa jana kwenye ukumbi wa Cafteria One sehemu ya Mlimani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Wahadhiri wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (Udasa) Dk Damasi Nyaoro alisema wahadhiri hao walifikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na ahadi hewa zinazotolewa na serikali kuhusu malipo ya madai yao.
Alisema kuwa mgomo huo utavihusisha vyuo vikuu vyote vya umma nchini, yaani Chuo Kikuu cha Dar es salaam sehemu ya Mlimani UDSM, Chuo cha Sayansi ya Afya na Tiba Muhimbili, Chuo cha Ualimu Changombe (Duce), Mkwawa (Muce), Chuo Kikuu cha Sokoine (Sua), Chuo Kikuu cha Mzumbe (Mu) na Chuo cha Ushirika Moshi.
Kura zilizopigwa jana za kupata maoni ya kugoma au kutogoma zilikuwa 439 ambapo kura 415 kati ya hizo ziliafiki mgomo na kura mbili ziliharibika na kura 22 hazikuafiki wala kukataa mgomo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wahadhiri wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (Udasa) Dk Damasi Nyaoro alisema wahadhiri hao walifikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na ahadi hewa zinazotolewa na serikali kuhusu malipo ya madai yao.
Alisema kuwa mgomo huo utavihusisha vyuo vikuu vyote vya umma nchini, yaani Chuo Kikuu cha Dar es salaam sehemu ya Mlimani UDSM, Chuo cha Sayansi ya Afya na Tiba Muhimbili, Chuo cha Ualimu Changombe (Duce), Mkwawa (Muce), Chuo Kikuu cha Sokoine (Sua), Chuo Kikuu cha Mzumbe (Mu) na Chuo cha Ushirika Moshi.
Kura zilizopigwa jana za kupata maoni ya kugoma au kutogoma zilikuwa 439 ambapo kura 415 kati ya hizo ziliafiki mgomo na kura mbili ziliharibika na kura 22 hazikuafiki wala kukataa mgomo.