Kenya 2022 Wagombea huru wa urais kumchagua mmoja atakayewawakilisha uchaguzini

Kenya 2022 General Election

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Wawaniaji huru wa urais walidokeza kuwa watamchagua mmoja wao, ili awawakilishe kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9, kwa minajili ya kuboresha nafasi zao za kuteuliwa
  • Haya yanajiri baada ya Afisi ya Msajili wa Vyama kuthhibitisha kuwa wawaniaji huru zaidi ya 45 walikuwa watawania urais bila kutumia vyama kwenye uchaguzi
  • Wagombea hao walisema kuwa kuteuliwa kwa mmoja wao atakayepeperusha bendera ya wawaniaji huru kwenye uchaguzi huo, kutarahisisha mchakato mzima wa uchaguzi
Wawaniaji huru 12 wa urais walidokeza kwamba watamchagua mmoja wao, ili awawakilishe kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9, kwa minajili ya kuboresha nafasi zao za kuteuliwa.
1.jpg


Mwanamuziki wa nyimbo za injili Reuben Kigame anayewania urais akiwa mgombea huru kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Wagombea hao walisema kuwa kuteuliwa kwa mmoja wao atakayepeperusha bendera ya wawaniaji huru kwenye uchaguzi huo, kutarahisisha mchakato mzima wa uchaguzi.

Wagombeaji hao ni pamoja na, Waweru Mbugua,Warunga Esther, Njenga Kinyanjui, Paul Muriungi, James Irungu, Dkt Joseph Karani, Reuben Kigame, George Munyotta, Stephen Owoko, Duncan Otieno, James Kamau na Kariuki King’ori.

Akizungumza kwenye kongamano la wawaniaji huru lililofanyika jijini Nairobi, siku ya Alhamisi, mwenyekiti wa wagombea wa kujitegemea Stephen Owoko ambaye pia anawania urais, alisema muda umewadia wa kudhihirisha uwezo wao wakiungana.

Kila mmoja akiamua atawania urais kivyake kwenye uchaguzi mkuu, hatuwezi kufaulu. Ni vyema tumuunge mkono mmoja wetu na tumpe kila anachohitaji ili awe rais,” Owoko alisema.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili na mwaniaji huru wa urais Reuben Kigame, aliwarai wagombea kujadiliana na kutafita njia itakayowawezesha kutwaa ushindi.
Hakuna lisilowezekana. Mungu akiwa upande wetu mwishoni tutakuwa na rais ambaye ni mwaniaji huru,” Kigame alisema.

Viongozi hao walieleza kuwa kuungana kwao kutarahisihsa shughuli za uchaguzi ikiwemo ukusanyaji wa saini zinazodaiwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom