Wafungiwa kazini kwa kuhofia Corona

Wafungiwa kazini kwa kuhofia Corona

Analogia Malenga

Platinum Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,292
Reaction score
10,842
Wajenzi hawajaruhusiwa kuziona familia zao tangu mwezi Machi

1597859077828.png

Wajenzi hawajaruhusiwa kuziona familia zao tangu mwezi MachiImage caption: Wajenzi hawajaruhusiwa kuziona familia zao tangu mwezi Machi

Kampuni ya Kichina inayotengeneza kiwandacha saruji katika mji mkuu wa Msumbiji, Maputo imewafungia wafanyakazi wapatao 60, raia wa nchi hiyo katika eneo la ujenzi tangu mwezi Machi.

Wawakilishi wa kampuni hiyo wanasema uamuzi huo ulichukuliwa ili kuzuwia uwezekano wa wafanyakazi hao kumuambukiza virusi vya corona muajiri wao.

Kiwanda cha saruji cha Salamanga kinajengwa katika wilaya ya Matutuone katika jimbo la Maputo.

Uamuzi huo umewafanya wafanyakazi wawe mbali na familia zao.

Wakili Paulino Cossa anasema hatua hiyo inakiuka sharia za kazi.

Muwakilishi wa kampuni hiyo anameahidi kuwaachilia wafanyakazi hao wiki ijayo.
 
Back
Top Bottom