Wafugaji wa mbwa kibiashara au ulinzi tukutane hapa

we kama mm siku moja nilikuta linasumbuana na mbwa wangu aisee nilitafuta Gongo moja matata nikamtandika nalo akazima nikajua nimemrahisishia mbwa wangu pambano naye alivyoona paka kazima akamuonea huruma akamuacha nikaingia ndani kurudi sikukuta paka kashasepa.Paka ana kichwa kizito mno yaani hafundishiki aisee.
bahati mbaya sipendagi mapaka mkuu
 
Wakuu kuna hii breed ya mbwa inaitwa Boerboel,asili yake ni South Africa. Very intelligent,muscular na wakali sana.Kuna nchi nyingi sana zinawapiga marufuku kama zinavyopiga marufuku American Pitt Bull terrier/Fila Brasileiro/Dogo Argentino etc etc.Kwa upande wangu mimi na kwa namna ninavyosoma na kufuatilia review za breeds nbali mbali za hawa viumbe,hii breed ni nzuri sana.Huwa wanafikisha mpaka kilo 90,na kwa kuwa wana genes za local African dogs,huwa wanastahimili mazingira na hali ya Africa vizuri sana.Ni guard dog wazuri na pia huwa wanatumika kwa livestock (Ingawa hakuna mbwa ambaye akiwa mmoja anaweza kumzuia simba au chui). Ngoja nijaribu kuweka picha moja au mbili hivi.
1541227712502.png
1541227809432.png
 
Najifunza sana kutoka kwenu ni mwanafunzi siku nikiamua kufuga sijaona kama belgian malinois hawa mbwa hakuna wakufanana nao
 
kuna mdau humu inaonyesha ni mzoefu zaidi juu ya hawa BM
@Tundapori
Najifunza sana kutoka kwenu ni mwanafunzi siku nikiamua kufuga sijaona kama belgian malinois hawa mbwa hakuna wakufanana nao
 
Wakuu kuna hii breed ya mbwa inaitwa Boerboel,asili yake ni South Africa. Very intelligent,muscular na wakali sana.Kuna nchi nyingi sana zinawapiga marufuku kama zinavyopiga marufuku American Pitt Bull terrier/Fila Brasileiro/Dogo Argentino etc etc.Kwa upande wangu mimi na kwa namna ninavyosoma na kufuatilia review za breeds nbali mbali za hawa viumbe,hii breed ni nzuri sana.Huwa wanafikisha mpaka kilo 90,na kwa kuwa wana genes za local African dogs,huwa wanastahimili mazingira na hali ya Africa vizuri sana.Ni guard dog wazuri na pia huwa wanatumika kwa livestock (Ingawa hakuna mbwa ambaye akiwa mmoja anaweza kumzuia simba au chui). Ngoja nijaribu kuweka picha moja au mbili hivi.
View attachment 919728View attachment 919731
mizigo ya ukweli
 
Ni kweli tupu kuwa GS kachakachuliwa sana. Watu wengi wanaofuga GS hawana elimu hata kidogo kuhusu swala zima la uzalishaji GS.

GS anapandwa na jibwa dume lolote tu unategemea nini??

Kwa upande wangu nimeamua kuachana kabisa na GS nimeamua kufunga Belgian Malinois (BM).

Tofauti kubwa kati ya GS na BM ni umbo la mwili tu na miguu ya nyuma.

BM wana mwili mdogo na miguu ya nyuma iko sawa na ya mbele, kwa hiyo wako na umbo la square.

Sifa ya BM:
-Highly intelligent
-More active kuliko GS
-More energetic than GS
-More agile than GS
-Wavumilivu wa magonjwa
-Low cost maintainance
-Hawachoki kwenye mituringa
-Wako sharp mno
-Walinzi wazuri mno.
-Siyo wazuri ukiwa na watoto wadogo, hapa ndo mahali pekee anapo shine GS. GS yuko friendly sana na watoto.
-BM wanatumiwa na wajeshi zaidi sababu ni wepesi kubebeka na wanajeshi wakiwa wanaruka na parachuti zao. GS mzito mno ndo maana anatumiwa na polisi zaidi.

Swala zima la ulinzi linahitaji mbwa wa kukuamusha zaidi kuliko kung’ata. Mbwa anayebweka akiona adui hana tofauti na Security alarm.

GS yupo dunia zaidi ya miaka 1000 iliyopita, ndo maana kachakachuliwe ile mbaya hasa na hawa waswahili wasiozingatia qualities za ku breed mbwa.

Nina mengi ya kusema ila niishie hapa kwa mwezi huu.

GS nawahurumia sana, siyo pure GS tena ila ni GSKOKO.

Wenye pure GS ni wachache mno sehemu kubwa ni kudanganyana tu.
wapi hiyo!! tunune
 
Cha kukuongezea tu

Gs asilimia almost 70 % sio pure breed hapa bongo ndo maana unakuta zinauzwa hadi 200,000 ,kwa GS pure inaanzia milion hadi na nusu ya miezi 2 ,ila angalizo nyingi tulizonazo sio pure ilikuijua iliyopure vigezo ni hivi
1.urefu wa miguu ya mbele ni mirefu kuliko ya nyuma,na urefu ni 22-26 chini hadi bega (akiwa na zaidi ya mwaka)
View attachment 916875
2.masikio yake huwa ni makubwa yaliyosimama wima
View attachment 916876
3.Mkia wa pure breed huwa ni wenye manyoya mengi sana
View attachment 916877

4 ,kUNA AINA ZA MBWA KARIBU 200 ila DNA Hudhihilisha kama iko pure au imechanganyia ,hii ni ghali ndo maana inaepukwa ,

HITIMISHO

Breed nyingi kwa bongo zimechakachuliwa hivyo ukiamua kufuata wazohili zuri la biashara jiongeze sana kushauriwa alienishauri aliniuzia GS kwa 200,000 nimemuhoji ndo kaniambia ukweli kuwa yangu sio pure breed akaniambia niangalie masikio yamelala sana akaniambia ingekuwa pure hata laki 9 sichukui.Aidha gs akikua anauzwa hadi 8000 usd ,wazungu wa migodini ndo wateja wakishamuona na vigezo vyote unakulamzigo ilani aghali sana pia kuwalea
Upo sahihi mkuu ni kweli pure breed bongo wapo wachache na mmi mwenyewe binafsi nimekutana nao hao cross wengi tu.. Ila naomba tu niseme kuwa wapo cross breed German Shepherds ambao ni very good quality.

Nimekutana nao cross breeds wengi wanaoweza kupata mafunzo na kuwa na performance nzuri sana hasa kwa ulinzi.. Tofauti kubwa inakuja kwenye Temparament.. Mara nyingi pure breed anao uwezo mkubwa sana wa kubadilika kua aggressive ndani ya mda mfupi wa kupewa command.. Cross nae utakuta anao uwezo wa kubadilika ila sio kwa haraka na kwa hasira kama pure breed.

Kwaio kwa mtu anaetaka mbwa mlinzi wa nyumbani .. Sioni sababu ya kumkataa cross breed ikiwa ni cross nzuri maana ata hao pure breeds wakiwa majumbani uwaga wanapewa domesticated training.. Hata siku moja mbwa wa nyumbani hatakiwi kupewa training sawa na yule wa jeshini. Atakua ni hatari sio tu kwa maadui lakini pia kwa wenyeji.
 
Back
Top Bottom