Wafanyakazi wa NMB Bank!

Wafanyakazi wa NMB Bank!

Shida ya hawa jamaa, wanadhani wateja wao wote sijui ni walimu! Manake wana dharau za kijinga sana

Nyani aoni kundule .... acha kudharau waalimu .... so wewe waalimu umewaeka kundi gani?!
 
tatizo ni kwamba haya matatizo utakayakuta pio ukienda kwenye Ofisi za CHADEMA, na hao wanaowatreat wateja vibaya na kuomba rushwa baadhi yao ni Wanachama wa CHADEMA, na wapo humu kutwa nzima wanamuita
Bw. Lowasa fisadi!
Kaka Kijakazi sikatai kwamba kuna waovu ndani ya chadema, ninachosema mimi ni kwamba ccm wana ridhaa ya kutuongoza katika masuala ya kitaifa, mambo kama haya hayakupewa kipaumbele sio kwakuwa hawayaoni (maana mara kadhaa nawasikia wakiyasema) ila hawajafanya kama tulivyo tarajia ili kulikomboa taifa. Tofauti na chadema,kwao ni suala la mtu mmoja mmoja. lakini suala hili lingechukuliwa kitaifa ingekuwa rahisi kuliwekea mikakati na sera kuanzia kwenye elimu,vipindi vya TV,radio na mijadala ya kitaifa n.k.
Mambo haya hakuna wa kuyafanya isipokuwa anayekusanya kodi na kuandaa bajeti mkuu,cdm watapiga kelele bila serikali kuamka usitegemee mtu mmoja mmoja kubadilika maana imekuwa utamaduni wetu kukaa na kusubiri dili.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kijakazi, kwa ufupi suala zima la ubora wa huduma au kusikiliza wateja (Customer service) hapa kwetu ni tatizo kubwa sana, na sio NMB tu. Nenda bar, nenda mgahawani nenda kwenye makampuni ya simu, mambo ni yaleyale.

Kiasi kwamba mtu akikuhudumia vizuri unashangaa, tena unatamai umuulize wewe ni mtanzania? We need to change

Ila NMB nambari wani asee, ikifika siku natakiwa kwenda NMB hua najiuliza hata mara kumi,niende au niache! wanakera.
 
Na mdada mwingine tawi la udsm chuo kikuu wa NBC, yule dada simpendi sana siku hiyo nimekwenda nilikuwa na shida ya malipo fulani hayakuingia kwenye akaunti yangu basi alinijibu nyodo ile mbaya nikachoma ndani kwa branch manager nikapata msaada mzuri tu..wanafikiri wote tunaoenda bank tuna vimishahara kama vyao!
 
Habari wadau!

Wafanyakazi wa hii Bank nimewanyooshea mikono.Haijalishi ni tawi gani au mkoa gani nitaenda nitakayo kutana nayo ni yaleyale. Naishia kujiuliza wanastress, mishara midogo au ndio hulka zao??Maana ni full nyodo+service kama amelazimishwa vile,unaweza susa na shida ni yako.Sijui ni kwangu tu au ni kwenu nyote

lol...tafuta yeyote kati yao mwenye title ya 'Manager' utaona tofauti
..pesa huongeza morali ya kazi..
 
Nani kakudanganya wahudumu wa bar ni darasa la saba pekee? Wako kila level

understand the difference nimesema waliko jaa hii haimaanishi wote ni darasa la saba but at least some are of other levels of education but there is no difference interms of their performance.
 
Habari wadau!

Wafanyakazi wa hii Bank nimewanyooshea mikono.Haijalishi ni tawi gani au mkoa gani nitaenda nitakayo kutana nayo ni yaleyale. Naishia kujiuliza wanastress, mishara midogo au ndio hulka zao??Maana ni full nyodo+service kama amelazimishwa vile,unaweza susa na shida ni yako.Sijui ni kwangu tu au ni kwenu nyote

Naomba kusema mie ni mteja wa Nmb wa akaunti ya binafsi ila kila nikienda tawi lolote sipati shida kama hizo na ikitokea nimepata basi kuna hatua huwa nachukua na ndio hizo zinazofanya ni enjoy huduma za Nmb
Kwanza tujue ya kwamba ktk huduma yyte lazima mteja ana haki zake sasa kwa hili la nmb liko katika sura zifuatazo;
1.Kama ukijibiwa vibaya au ukipewa huduna vibaya inatakiwa utoe taarifa kwa meneja wa tawi husika na hyo ni haki yako na mie nimeitumia sana,kama meneja wa tawi hajakutendea haki piga namba ambazo zipo ktk bango limeandikwa kukuhudumia ni fahari yangu utaona moto wake kwa aliekujibu kwan hakuna msalia mtume hapo staff huyo atakuwa matatani.
2.Kama hlo tawi wapata huduma mara kwa mara ebu soma jina lake ktk name tag yake mletee hapa jamvin kwam naamin mabos na staff wa nmb wengi ni wanajamvi hapa so itakuwa easy kwao kulifanyia kazi
3.Mtoa mada kidogo ungekuwa waz kwamba mhudumu wa twai flan na jina flan kwan woga wetu watanzania ndio watuponza sana tukiweza semana hadhari najua wataogopa kusema au kutoa huduma mbaya
4.Wewe ndio unaowaweka pake hao wahudumu wa nmb bwana sasa kwann wakujibu mie huwa naenda na kiburi hcho na ukitegemea nina hisa nilinunua ha mbona wanajuta mie wakiniona
 
Ni kweli wakuu Tz mteja hapewi sifa anayostahiki katika sehemu njingi lakini kwa hawa NMB wamezidi
 
Nyani aoni kundule .... acha kudharau waalimu .... so wewe waalimu umewaeka kundi gani?!

Mimi ni mwalimu pia, nimesema hivo kwa sababu ni kweli walimu ndio tunaodharaulika ktk nchi hii kuliko kada yoyote, au kuna mtu hajui hilo!
 
Sio hao tu hata NBC nao usiwaache tabia yao ni hiyo hiyo yaani nakerekaje?



Habari wadau!

Wafanyakazi wa hii Bank nimewanyooshea mikono.Haijalishi ni tawi gani au mkoa gani nitaenda nitakayo kutana nayo ni yaleyale. Naishia kujiuliza wanastress, mishara midogo au ndio hulka zao??Maana ni full nyodo+service kama amelazimishwa vile,unaweza susa na shida ni yako.Sijui ni kwangu tu au ni kwenu nyote
 
wewe umenena jamani kizazi cha dotcom ni tatizo wanazitafuta kazi kwa kila njia ila wakishapata hawajali hizo kazi watu wanafanya kazi kwa mazoea, hakuna ownership kazini yeye anachoangalia ni mshahara si utaingia tu mwisho wa mwezi, ila kama ulivyosema kadri siku zinavyoenda watabadilika tu unaleta nyodo kazini kaa pembeni wenye commitment waendelee
Kwa mtazamo wangu tatizo ni zaidi ya elimu ya customer service, watanzania wengi hatupendi kuwajibika kwenye maeneo yetu ya kazi. Ila kwa hali inavyoendelea na soko la ajira linavyozidi kuvamiwa na wageni tutabadilika tu.

Ushawahi kuona mzungu anasoma kitabu cha time management, au sijui how to be effective at work, anakushangaa kwa sababu hivyo ni vitu amejifunza tangu ngazi ya chini na anajua anachotakiwa kufanya na wajibu wake ni nini kama mfanyakazi/ mwajiriwa.

Sisi mtu una miaka 5 hadi 10 kazini unajigamba umehudhuria semina ya time management unabandika na cheti ofisini.
Sikatai kujifunza hivyo vitu, ila tunachelewa sana.
 
Sasa hivi nipo tawi la nmb Handeni baada ya kusafiri kwa nauli ya sh 6000 kufuata atm card ambayo ime expire mwezi uliopita. Eti naambiwa "mtandao hatuna njoo kesho" kwa kweli ningekuwa na bomu ningelipua. TUMECHOKAAA AH
 
hawana wateja wengi, mie natumia FNB ie. first national bank ni ya south africa, hadi raha unavyohudumiwa....

Hizi benki mpya kwanza zina wateja wachache. Pili, hazina simile na watu wanaofanya kazi kwa mazoea. Mtendaji wa NMB au NBC haziwezi ofisi hizi, la sivyo akubali kubadilika
 
Bandugu urasimu huu haujaishia hapo tu kwa nmb au nbc. Kivumbi kingine nenda ktk ofc za serikali ndo utajuta zaidi. Kwa mfano kuna cku nilikuwa pl tra tawi la mwenge, kwanza nilichoshwa na foleni ya nmb hlf nakujaa ndani tra balaa lilelile na mbaya zaidi alikuja muhaya mmoja hv ht hajakaa foleni kaongeana afisa wa tra lugha yao kapata huduma na kuondoka ilihali akina sisi kutwa nzima tupo pl. Hatari sana hii ya ukabila, urasimu na nyodo ktk kazi.
 
Mimi nimejifunza kwamba kuna unafuu kidogo wa huduma kwenye vibenki vidogodogo kama ACB, Mkombozi, nk

Zaman nilikua nmb nililazimika kuachana nao kwa sababu hizihizi za huduma mbovu nikawajaribu ACB ndio hawapo vizuri sana lkn angalau wanajitahidi.Nataman wangepitia huu uzi waone wenyewe ni kwa kiasi gani watu wamewachoka
 
Back
Top Bottom