Brainy Chick
Member
- Mar 9, 2013
- 64
- 21
- Thread starter
- #41
Yaani tatizo langu ukishanikera, hata mia mbili sikupi. The same I aaplied kwa trafic police akinisumbua sana kwa usmbufu barabarani aisee tutaenda kituoni ntalipa makosa yote ila uniandikie ile risit yao na sikupi hata jero.
Lakini mtu akinipa huduma nzuri, sidhani kama kuna mtu kati yetu ataacha kufurahi na kumuachia japo hela ya soda ingawa sio mazoea mazuri lakini inatokea pale mtu unapohudumiwa vizuri na ukijua mtu hategemei chochote kutoka kwako ila anakujali kama mteja na anatimiza wajibu wake.
Shule yangu ni ndogo sana, I mean ni dogo(Japo sasa hivi nasoma) ila kila nilipofanya kazi, ubora wa huduma yangu emekua msaada mkubwa sana kufahamiana na watu mbalimbali na hata kupata fursa za kupata kazi sehem ambazo kwa kweli isingekua rahizi kama vigezo na masharti vingezingatiwa.
Kuna kipindi nilikua nafanya kazi na wakenya, walikua wanasema "This is kenyan guy living in TZ" sikua napenda sana hiyo kauli kwa sababu wanaona sisi wa TZ hatuwajibiki kikamilifu.
Kazi yangu ya kwanza ilikua kwnye internet cafe, si jisifu ila huduma yangu ilikua kwenye kiwango cha kuridhisha kiasi kwamba wateja walikua wanadhani ile ofisi ni ya mama yangu na kumbe alikua bosi wangu. Na kutoka hapo cafe nilipata nafasi kwenye ofisi na huo ulikua ni mwanzo wa kujenga professional yangu hadi sasa hivi.
Nakumbuka kuna kipindi mkuu wa kitengo chetu mkenya aliandika barua kwa mkurugenzi akitaka niongezwe mshahara na nipandishwe daraja japo sio graduate, alijenga hoja na hilo lilifanyika. Na siku nilipoamua kuondoka hiyo kampuni baada ya kuwatumikia kwa miaka sita (japo haikua rahisi kunikubalia ombi langu), walinifanyia kasherehe kakuniagata na kwa kweli nipata bahati ya kusikia nikisifiwa sifa ambazo mara nyingi mtu husifiwa akiwa kwenye jeneza, hilo lilitaka kunifanya nibadili maamuzi yangu ya kuondoka.
Lengo sio kujisifu ila nilikua nataka kuonyesha jinsi ukifanya kazi yako bila shurutishi inavyokuletea manufaa binafsi.
Umenena mkuu!!