Wafanyakazi 12 Shule ya Umoja wa Wazazi CCM walia mishahara, waandika barua kwenda kwa Rais Samia

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
img11.jpg

img19.jpg
Waliokuwa watumishi (wastaafu) na ambao bado ni watumishi wakiwemo Walimu katika Shule ya Sekondari Bulima, iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Jumuiya ya Wazazi ya Chama hicho (UWT) wamelalamikia kutolipwa mishahara yao kwa muda mrefu ikiwemo mafao ya mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Wakizungumza na waandishi wa Habari leo, wafanyakazi hao wamesema kuwa suala la ulipwaji wa mishahara limekuwa changamoto kubwa, huku michango yao NSSF ikiwasilishwa kwa kusuasua.

“ Tangu nimeajiriwa hapa, tumekuwa tunalipwa kwa kusuasua sana, kwa mwaka wanaweza kutulipa miezi mitatu hadi minne, na miezi mingine tukabaki tunadai, sasa tangu mwaka huu umeanza shule hii haifanyi kazi,” Amesema Mary Mshana….

“ Wazazi ambao walikuwa na watoto hapa waliwaondoa, na wale ambao tulitarajia kuwasajili kidato cha kwanza mwaka huu, hakuna mtoto hata mmoja aliyekuja, mpaka sasa shule haina mwanafunzi hata mmoja,”

Wafanyakazi hao wanasema kuwa kutokana na hali hiyo, wamekuwa wakifuatilia hatma ya ajira yao kutokana na kukaa muda mrefu bila ya kazi lakini pia hata mshahara hawapati.

“Tumefuatilia barua ya ukomo wa kazi yetu hatupewi, tumekwenda NSSF lakini tumeambiwa kuna malimbiko mengi ya mshahara bado hayajapelekwa kwenye mfuko huo, tumewatafuta viongozi wa Chama bado hatujasaidiwa” Jackson Kangoma, Mwalimu.

Waliostaafu kwa muda mrefu wamesema kuwa wamehangaika kupata mafao yao ya kustaafu lakini bado hawajapata kutokana na michango yao kutowasilishwa NSSF.

Wafanyakazi hao wamemwangukia Rais Samia ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, kuwasaidia ili waweze kupata haki yao, kwani viongozi wengine wa chini yake wameshindwa kuwasaidia.

“ Tunamuomba mama yetu, kipenzi chetu, Rais wa wanyonge, atusaidie kwenye hili, sisi wastaafu na hawa wengine ambao bado wameajiriwa lakini shule haifanyi kazi, tunateseka sana, tunaomba aingilie hili, atusaidie,” amesema Jeremiha Magige.

=============

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shemsa Mohamed, amesema anafahamu madai hayo na anafuatilia ili kuyafanyia kazi.

"Madai yao yamekuwa yakijadiliwa katika vikao vya jumuiya ya wazazi na sisi kama chama, tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hivyo ninaomba niendelee kufuatilia ili nije na taarifa sahihi kuhusu madai hayo," amesema Shemsa.
 
Kumbe Changamoto hii ipo karibia shule zote za wazazi ccm mfano milala secondary iliyopo MPANDa ni kama imekufa maana idadi ya wanafunzi form 1 _4 ha ifiki 50.

Kwa uongozi wa mkuu chasila niliskia yeye ndo alikuwa anawanyonya walimu wenzie yaani ilikuwa inafikia mwisho wa mwezi mwalimu baadala ya kupewa mshahara anapewa Debe la mahindi na kilo tano ya maharage basi unambiwa tumia hivyo ukiwa unasubiri malipo.

Kuna mwl mmoja alikuwa anaitwa kwesi alistafu hata nauli ya kurudi Kwao musoma alikoswa alikuja kubebwa Kwa mchango wa ndugu.

Nilichogunduwa tatizo la haya yote ni wakuu wa chama wamili wa hizi shule.
 
Hili swala ni kubwa Sana me pia ni muhanga meta sekondary mkoa wa mbeya watumishi wote waliopo na waliofukuzwa nikiwepo mimi na waliostafu zaidi ya 40 pesa zetu za mishahara na NSSF na mimi nilifukuzwa baada ya kuanza kudai pesa tunaomba mheshimiwa raisi atusaidie imekuwa genre la wazurumaji
 
Ccm wameshindwa kuziendesha hizi shule,mfano hii bulima Ina miundo mbinu mizuri ila no wanafunzi,nyingine ni kahunda sec- sengerema nayo inaelekea kibra wakati shule iko na majengo mazuri tu,nashauri serikali izinunue shule hizi kwa faida ya watoto wetu
 
Waliokuwa watumishi (wastaafu) na ambao bado ni watumishi wakiwemo Walimu katika Shule ya Sekondari Bulima, iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Jumuiya ya Wazazi ya Chama hicho (UWT) wamelalamikia kutolipwa mishahara yao kwa muda mrefu ikiwemo mafao ya mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Wakizungumza na waandishi wa Habari leo, wafanyakazi hao wamesema kuwa suala la ulipwaji wa mishahara limekuwa changamoto kubwa, huku michango yao NSSF ikiwasilishwa kwa kusuasua.

“ Tangu nimeajiriwa hapa, tumekuwa tunalipwa kwa kusuasua sana, kwa mwaka wanaweza kutulipa miezi mitatu hadi minne, na miezi mingine tukabaki tunadai, sasa tangu mwaka huu umeanza shule hii haifanyi kazi,” Amesema Mary Mshana….

“ Wazazi ambao walikuwa na watoto hapa waliwaondoa, na wale ambao tulitarajia kuwasajili kidato cha kwanza mwaka huu, hakuna mtoto hata mmoja aliyekuja, mpaka sasa shule haina mwanafunzi hata mmoja,”

Wafanyakazi hao wanasema kuwa kutokana na hali hiyo, wamekuwa wakifuatilia hatma ya ajira yao kutokana na kukaa muda mrefu bila ya kazi lakini pia hata mshahara hawapati.

“Tumefuatilia barua ya ukomo wa kazi yetu hatupewi, tumekwenda NSSF lakini tumeambiwa kuna malimbiko mengi ya mshahara bado hayajapelekwa kwenye mfuko huo, tumewatafuta viongozi wa Chama bado hatujasaidiwa” Jackson Kangoma, Mwalimu.

Waliostaafu kwa muda mrefu wamesema kuwa wamehangaika kupata mafao yao ya kustaafu lakini bado hawajapata kutokana na michango yao kutowasilishwa NSSF.

Wafanyakazi hao wamemwangukia Rais Samia ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, kuwasaidia ili waweze kupata haki yao, kwani viongozi wengine wa chini yake wameshindwa kuwasaidia.

“ Tunamuomba mama yetu, kipenzi chetu, Rais wa wanyonge, atusaidie kwenye hili, sisi wastaafu na hawa wengine ambao bado wameajiriwa lakini shule haifanyi kazi, tunateseka sana, tunaomba aingilie hili, atusaidie,” amesema Jeremiha Magige.

=============

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shemsa Mohamed, amesema anafahamu madai hayo na anafuatilia ili kuyafanyia kazi.

"Madai yao yamekuwa yakijadiliwa katika vikao vya jumuiya ya wazazi na sisi kama chama, tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hivyo ninaomba niendelee kufuatilia ili nije na taarifa sahihi kuhusu madai hayo," amesema Shemsa.
Huenda utakuta shule hiyo ilikuwa middle school ya serikali CCM wakaiiba kama walivyofanya huko Mbeya.
 
Waliokuwa watumishi (wastaafu) na ambao bado ni watumishi wakiwemo Walimu katika Shule ya Sekondari Bulima, iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Jumuiya ya Wazazi ya Chama hicho (UWT) wamelalamikia kutolipwa mishahara yao kwa muda mrefu ikiwemo mafao ya mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Wakizungumza na waandishi wa Habari leo, wafanyakazi hao wamesema kuwa suala la ulipwaji wa mishahara limekuwa changamoto kubwa, huku michango yao NSSF ikiwasilishwa kwa kusuasua.

“ Tangu nimeajiriwa hapa, tumekuwa tunalipwa kwa kusuasua sana, kwa mwaka wanaweza kutulipa miezi mitatu hadi minne, na miezi mingine tukabaki tunadai, sasa tangu mwaka huu umeanza shule hii haifanyi kazi,” Amesema Mary Mshana….

“ Wazazi ambao walikuwa na watoto hapa waliwaondoa, na wale ambao tulitarajia kuwasajili kidato cha kwanza mwaka huu, hakuna mtoto hata mmoja aliyekuja, mpaka sasa shule haina mwanafunzi hata mmoja,”

Wafanyakazi hao wanasema kuwa kutokana na hali hiyo, wamekuwa wakifuatilia hatma ya ajira yao kutokana na kukaa muda mrefu bila ya kazi lakini pia hata mshahara hawapati.

“Tumefuatilia barua ya ukomo wa kazi yetu hatupewi, tumekwenda NSSF lakini tumeambiwa kuna malimbiko mengi ya mshahara bado hayajapelekwa kwenye mfuko huo, tumewatafuta viongozi wa Chama bado hatujasaidiwa” Jackson Kangoma, Mwalimu.

Waliostaafu kwa muda mrefu wamesema kuwa wamehangaika kupata mafao yao ya kustaafu lakini bado hawajapata kutokana na michango yao kutowasilishwa NSSF.

Wafanyakazi hao wamemwangukia Rais Samia ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, kuwasaidia ili waweze kupata haki yao, kwani viongozi wengine wa chini yake wameshindwa kuwasaidia.

“ Tunamuomba mama yetu, kipenzi chetu, Rais wa wanyonge, atusaidie kwenye hili, sisi wastaafu na hawa wengine ambao bado wameajiriwa lakini shule haifanyi kazi, tunateseka sana, tunaomba aingilie hili, atusaidie,” amesema Jeremiha Magige.

=============

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shemsa Mohamed, amesema anafahamu madai hayo na anafuatilia ili kuyafanyia kazi.

"Madai yao yamekuwa yakijadiliwa katika vikao vya jumuiya ya wazazi na sisi kama chama, tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hivyo ninaomba niendelee kufuatilia ili nije na taarifa sahihi kuhusu madai hayo," amesema Shemsa.
Chama mfu hicho bila policeccm n nec kingeshatoweka
 
Back
Top Bottom