A
Anonymous
Guest
Nawakilisha kwa Uchungu Mkubwa sana ukiwa ndani ya moyo wangu kutokana na Dhulma tunayofanyiwa na Katibu wa CCM Mufindi bwana Clement Bakuli.
Soko la Sabasaba lilizuka baada ya sisi wahanga tuliounguliwa na moto katika soko la Mandela mwaka 2016 kupewa nafasi tuanzishe soko lingine. Tulianza kuchangia Ujenzi kwa kuandikwa kwenye vidaftari na kuonyeshwa vyumba vyetu.
Gharama kwa kipindi kile zilikuwa kati ya milioni 3 na 4, kwa bahati mbaya hatukuwa tukidai risiti lakini kila mtu anajua kuwa tulichangia kwa asilimia mia gharama za ujenzi.
Kampuni iliyosimamia jambo hili ni ya bwana Bakuli aliyekuwa kipindi hicho yupo katika ngazi za Chama hapa mkoani Rukwa. Siwezi kuelezea walipeana vipi tenda hiyo,ila tu kiwanja ni mali ya CCM. Mchakato mzima wa upatikanaji wa viwanja humu ndani ya soko ulihodhiwa na mwanae aitwa Jose ambaye hakuna asiyejua jinsi alivyouzia watu vyumba mara mbilimbili hadi Baba yake alipomtoa katika nafasi za kampuni yake. Baada ya kukaa miaka kama minne CCM waligawana vyumba na Mr Bakuli.
Tukapata bahati mbaya ya kubaki na Bakuli, kwani wenzetu walioenda CCM walipata nafuu ya kulipa chumba mwezi mmoja mmoja na bei hadi sasa ni 80,000/- na kurenew mkataba kwao ni bure.! kumbuka mizingwe yote hii tumetenganishwa na corridor tu na wenzetu yaani jengo ni moja
Maajabu ni kwa upande wa Katibu aliyebaki na nusu ya vyumba vyote vya soko:
Kwake kodi kwa sasa mkataba ni 150,000/kwa mkupuo wa miezi mitatu ambayo ni kinyume na Sheria ya Mwaka 2005, kifungu cha 26 sheria no 11 ambayo inasema 🙂Kodi itapangwa na kuongezeka kwa kuzingatia Thamani ya eneo linalopangishwa kwa kutegemea bei ya soko}, na sasa alitupa barua ya kusitisha ukomo wa mkataba, na kila anaeenda kurenew mkataba anatakiwa atoe milioni 2-3..sasa unajiuliza kwa sisi Maskini tuliounguliwa vibanda na sasa ndio madeni ya Mikopo tunaanza kuikamilisha ndio anataka kutunyang'anya vyumba.
Je, tuende wapi na Mayatima wetu? Mbona ndio kama mnatuunguzia soko tena.? Hili jambo la dhulma ya namna hii kilio chetu asikie nani? na ndio kura zetu mnataka octoba? na ndio huko Mufindi mmeanza miradi ya ujenzi wa vyumba? nao yaje yawakute kama yetu?
Soko la Sabasaba lilizuka baada ya sisi wahanga tuliounguliwa na moto katika soko la Mandela mwaka 2016 kupewa nafasi tuanzishe soko lingine. Tulianza kuchangia Ujenzi kwa kuandikwa kwenye vidaftari na kuonyeshwa vyumba vyetu.
Gharama kwa kipindi kile zilikuwa kati ya milioni 3 na 4, kwa bahati mbaya hatukuwa tukidai risiti lakini kila mtu anajua kuwa tulichangia kwa asilimia mia gharama za ujenzi.
Kampuni iliyosimamia jambo hili ni ya bwana Bakuli aliyekuwa kipindi hicho yupo katika ngazi za Chama hapa mkoani Rukwa. Siwezi kuelezea walipeana vipi tenda hiyo,ila tu kiwanja ni mali ya CCM. Mchakato mzima wa upatikanaji wa viwanja humu ndani ya soko ulihodhiwa na mwanae aitwa Jose ambaye hakuna asiyejua jinsi alivyouzia watu vyumba mara mbilimbili hadi Baba yake alipomtoa katika nafasi za kampuni yake. Baada ya kukaa miaka kama minne CCM waligawana vyumba na Mr Bakuli.
Tukapata bahati mbaya ya kubaki na Bakuli, kwani wenzetu walioenda CCM walipata nafuu ya kulipa chumba mwezi mmoja mmoja na bei hadi sasa ni 80,000/- na kurenew mkataba kwao ni bure.! kumbuka mizingwe yote hii tumetenganishwa na corridor tu na wenzetu yaani jengo ni moja
Maajabu ni kwa upande wa Katibu aliyebaki na nusu ya vyumba vyote vya soko:
Kwake kodi kwa sasa mkataba ni 150,000/kwa mkupuo wa miezi mitatu ambayo ni kinyume na Sheria ya Mwaka 2005, kifungu cha 26 sheria no 11 ambayo inasema 🙂Kodi itapangwa na kuongezeka kwa kuzingatia Thamani ya eneo linalopangishwa kwa kutegemea bei ya soko}, na sasa alitupa barua ya kusitisha ukomo wa mkataba, na kila anaeenda kurenew mkataba anatakiwa atoe milioni 2-3..sasa unajiuliza kwa sisi Maskini tuliounguliwa vibanda na sasa ndio madeni ya Mikopo tunaanza kuikamilisha ndio anataka kutunyang'anya vyumba.
Je, tuende wapi na Mayatima wetu? Mbona ndio kama mnatuunguzia soko tena.? Hili jambo la dhulma ya namna hii kilio chetu asikie nani? na ndio kura zetu mnataka octoba? na ndio huko Mufindi mmeanza miradi ya ujenzi wa vyumba? nao yaje yawakute kama yetu?