Wafanyabiashara Mtandaoni Kujisajili Ndani ya Mwezi mmoja. Faida na hasara zake ni nini? Tufanyeje?

Wafanyabiashara Mtandaoni Kujisajili Ndani ya Mwezi mmoja. Faida na hasara zake ni nini? Tufanyeje?

gabylovestech

Member
Joined
Jul 13, 2025
Posts
20
Reaction score
50
1. Kwanza ni-declare Interest, Mi ni moja ya wanufaika wa Internet. Nimejiajiri kupitia internet na cycle yangu kubwa ni hawa influencers, freelancers, content creators, advertisers, etc.

2. Pili lazima tukubali Kodi ndio inaendesha uchumi wa nchi yoyote Ile duniani.

Huwezi endesha nchi bila kodi, ushuru n.k

Me sio mtaalamu wa masuala ya kodi ila hiki kitu Kuna mahali Serikali inapatia na kwingine inakosea ama Kuna INFO-GAP hapo.

3. Biashara nyingi kama sio zote zinazofanyika Online zinaExist physically.

Mfano nina duka la viatu sinza, ninapopost kiatu Facebook nahitaji tu kufikia wateja wengi sababu hao wateja wanaExist physically, watakuja kuchukua kiatu Dukani, nitawapa risiti ya Efd, n.k

4. Hapo nalipa kodi TRA , nalipa Nemc, n.k

Sasa ukisema nilipe kodi kwa kufanya matangazo Online nalipa kodi mara mbili kwa minajili ipi?

5. Tukija suala la influencers na content creators.

Influencers hawa wanapewa kazi na mashirika, Manuka, taasisi , n.k ambazo zinaExist kwa mujibu wa sheria na zinalipa kodi.

Sasa ukisema wao walipe wanalipa kwa minajili ipi?

6. Content creators, sijui kwa mitandao mingine ila youtube tayari TCRA inalipisha 100,000 nadhani mhe Nnauye Nape alipunguza alipopewa wizara tu.

Sasa huyu pia atadaiwa kodi kivipi na ameshalipia TCRA

7. Nakubali kuwa online Kuna pesa ila baadhi ya hawa influencers na Content creators wanafanya for fun.

Sasa hawa mnawalipisha vipi kodi, utafatilia vipi huyu anafanya for fun ama sio for fun?

8. Kuna influencers na content creators ambao malipo yao sio pesa.

I mean Kuna mtu anatangaza hotel fulani inayolipa kodi kwa mujibu wa sheria, malipo yake ni kwenda kula bure.

Huyu unamlipisha vipi kodi?

9. Kuna watu mfano ni MC ana kampuni ameajiri vijana, analipa kodi.

Sasa akipost content yake au viashara yake Instagram, au YouTube alipe tena kodi?

Hii si sahihi labda nielimishwe zaidi

10. Me nakubaliana na ulipaji kodi lakini Serikali lazima iangalie inatoa Value gani kwenye hao watu kulipa kodi.

Mfano: JPM aliwapa machinga viparata kwa 20,000/=, Value aliyotoa ni Machinga wasisumbuliwe na mgambo.

Ukitaka kukamua ng'ombe lazima ulishe majani

11. Kuna shida nyingi sana.

As much as mnaona vijana wanapata mia mbili mia tatu online, kuna deni kama Serikali inabidi ishughulilie.

Mfano Mabando yako juu, mmefungia baadhi ya mitandao kuAccess hadi VPN Payment gateways nyingi za nje hazifanyi kazi Tz, Vijana ndo kwanza wanaanza kupunguza tatizo la ajira via internet.

Sasa ni vyema tukaweka focus kwenye kukuza na kutoa awareness, hata kuongezea kwenye mitaala kwa muda kidogo ndio tuje kudai Kodi.

Hii influence ya nchi zingine haiwezi kusaidia kwetu.
Mfano Kenya wameanza kupitisha mswaada wa kuTax content creators,
Of which najua hawatatoboa.
Sasa Kenya mtu analipia bundle $15 kwa mwezi.

Hiyo $15 kijana wa Tanzania ndio analipia kwa siku. Mara pengine hata zaidi.

Bado analipia TCRA na kama ana office au duka analipia kodi TRA

Sasa kumTax huyu ni kumuonea bure.

12. Serikali iangalie pia kiasi gani inatax kulingana na Yenyewe imetoa value gani kwa huyu mtu mnampa Tax, itapata mapato mengi sana.

Tuuzieni 1GB kwa 500 Tzs.

Halafu labda 300 nenda katudai TOZO kwenye advertisement, contents etc zilizoleta pesa.

Serikali itapata mapato zaidi kuliko sasa mtu annue bundles juu, bado umpige na TOZO.

Mtakosa hata kidogo mnachotaka.

13. Serikali iangalie sana hizi regulation zisijefanya vijana waanze kuangalia alternatives kwenye nchi zingine.

Kesho msishangae mtu anampa kazi kijana wa US au SA amfanyie matangazo, ampostie contents, etc kwa kukwepa tozo kwenye nchi yake.

Muhimu kwenda polepole kwenye hili suala na kushirikisha wadau.

14.Tanzania bado ni nchi changa ila trust me Kuna vijana wana exposure kubwa sana kwenye haya mambo na wanaweza wasaidia.

Lakini wanapuuzwa. Vijana wanashangaa hadi mifumo mnaenda kutengeneza Dubai kwa pesa nyingi na wao wanaweza leta solutions, kesho unataka TOZO kwake.
Hii si SAWA.

15. Mwisho Tunaipenda nchi yetu. Tunataka kulipa kodi.
Muhimu mjue
👉Biashara zote za online zinaExist offline na zinalipa kodi
👉Ukitaka kodi ni vyema uwape wananchi Value
👉Kuna watu ni influencers,digital marketers content creators for Fun
👉Tujipe muda
 
Wamekurupuka jamaa, badala ya kufuatilia wakwepa kodi busy kufuatilia vijana wanaojiajiri... Hivyo sana!
 
Kwanza ni-declare Interest, Mi ni moja ya wanufaika wa Internet. Nimejiajiri kupitia internet na cycle yangu kubwa ni hawa influencers, freelancers, content creators, advertisers, etc.
Mkuu kwanza tueleweshe vizuri sisi tusio huko mtandaoni.

1. Nini tofauti ya Biashara ya mtandao na Matangazo Mtandaoni?

2. Kitendo cha mtu kumtumia msanii kutangaza bidhaa zake kisha wateja wakaenda Dukani kununua, hii ni biashara ya mtandao?

3. Mtu anayetangaza bidhaa mtandaoni, mteja analipia kisha anafanyiwa delivery bila kufika dukani, hii pia ni biashara mtandao?

3. Kampuni za SImu tiGo, Voda, Airtel wanapotangaza matangazo mtandaoni na wateja wakanunua bundles na vifurushi, hii pia ni biashara ya mtandao?

4. Watu wanaofanya FOREX, CRYPTO currency na wanaingiza kipato kupitia mtandao, je hii pia ni biashara mtandao?

5. Watu wanaofanya Freelancing (Copy writing, Coding, Systems assistance, Translation) na makampuni ya nje kupitia Freelancing apps, hawa pia ni wafanyabiashara wa mtandao?

6. Wasanii wanaouza kazi zao Spotify, Youtube, Tiktok na wanalipwa kwa views, hawa pia ni wafanya biashara wa mtandao?

7. Comedians ambao wanapost clip kisha watu watakaopenda clip zao wanawatumia zawadi (GIFTS) kupitia Tiktok, je hawa pia ni wafanyabiashara wa mtandao?

8. Wale wafanyabiashara ambao wapo CHINA, TURKEY, USA, CANADA,JAPAN ambao wanapost machimbo ya bidhaa na kisha kuwaagizia watanzania mizigo baada ya malipo, wale pia watalipa tuzo tanzania au watalipa nchi walizopo, Na je ile pia ni biashara ya mtandao au ni matangazo?

9. WINGA wa kariakoo ambaye mtaji ni WhatsApp status na Instagram, huyu nae ni mfanya biashara ya mtandao?

Naomba nijulishwe kwenye shughuli nimezitaja hapo juu, Yupi anafaa akafanye Usajili TRA na ni namna gani TRA watafanya ili waweze kupata kodi kwa muhusika.


KODI inahitaji mipango, mijadala, mikakati imara, utekelezaji usio na shaka(kisheria).

Kama Serikali inavyozipenda hela za watu, na watu pia wanazipenda hela zao hivyohivyo.
 
Ni uonevu biashara nyingi zina leseni na zilishalipiwa ushuru wote hadi kumfikia mteja
 
Back
Top Bottom