Wafanya biashara k.koo wagomea mashine za EFD

Wafanya biashara k.koo wagomea mashine za EFD

Shine

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2011
Posts
11,481
Reaction score
1,371
wafanya biashara wote k.koo asubuhi ya leo wamegoma kufungua maduka yao kwa madai ya bei juu ya mashine za EFD
source mimi mwenyewe nipo eneo la tukio
 
Kariakoo ni zogo tupu mtaa wa Kongo uko tupu, kabisa kuna fujo ambazo haijajulikana zinatokana nanini, nimegeuza natafuta njia mbadala, wenye access ya kariakoo tupeni updates
 
Trueeee..........kbss hamna aliyefunguaaaa na mimi np hapaa na UMEME umekatwa na Tanesco nw
 
TRA kuna watu ambao wako ki rushwa zaidi. hawawezi kubuni mbinu mpya za kuongeza mapato. waachie ngazi damu changa ije na new ideas. makampuni ya simu yanakua na mkurugenzi mmpya every three four years wanaoleta new ideas mpaka bei ya kutwanga simu zimepungua sana. TRA the same old dogs miaka nenda miaka rudi. wanataka wafie ofcn bila hata kufaidi rushwa iliyolimbikizwa uswiss
 
TRA wabadilike haraka na mashine zao
mambo haya yameanza Mbeya,Moro,
sasa Dar mwisho nchi nzima

Halafu tatizo lao ni porojo tu wakati
wafanyabiashara wamegundua kuwa
bei hii ya laki nane sio sahihi kabisa

Maana Kenya laki mbili,Dubai ndiyo
kama unakwenda kununua Toy.
 
wafanya biashara wote k.koo asubuhi ya leo wamegoma kufungua maduka yao kwa madai ya bei juu ya mashine za EFD
source mimi mwenyewe nipo eneo la tukio

Problem ni kwamba TRA wanalazimisha watu wanunua mashine kutoka maduka flani flani ambayo wana hisa nayo, badala ya kuacha soko huria lichukue nafasi yake. Ambacho wangefanya TRA ni kuruhusu wafanyabishara waaize mashine hizi kwa wingi, then waziunganishe na system yao ya mapato, kama ilivyo kwa kompyuta au simu. Lakini wasilazimishe watu wanunua mashine hizi kutoka kwa suppliers wawili tu. Ukiritimba wa nini kwa dunia ya leo?
 
Hivi kwanini watanzania hatupendi kulipa kodi? Sijui tunafikiri maendeleo yatashuka kutoka mbinguni?
 
Dodoma nako kimenuka nimeona itv jamaa wanajazba nikajisemea eeh Mungu wangu endelea kutupa ujasiri watu wako waamke na wamkatae huyu mwovu sisiem,jangili,mnyonyaji,fisadi na kila aina ya uchafu!!!
 
Hivi kwanini watanzania hatupendi kulipa kodi? Sijui tunafikiri maendeleo yatashuka kutoka mbinguni?
Tatizo hapa c kutotaka kulipa kodi, tatizo ni bei ya hizo mashine na inakuwaje muuzaji awe ni yule tu aliyeamuliwa na tra? Na kuwa kila mwenye mauzo ghafi yanayofikia tsh.45,000 kwa cku lazima awe na mashine hata mwenye genge, mama lishe , muuza mkaa anatakiwa awe nayo, na kuna wengine kama ni bar sehemu ya bia iwe na mashine yake,jikoni hivyo hivyo! Na tatizo kubwa kuliko yote ni kutoona manufaa ya hizo kodi wanazolipa zinakwenda wapi? Kila cku mala bilioni 50 zimeliwa, akienda hospital hata panadol hamna!
 
Kuna mchina kakamatwa na mgambo wa jiji, alikuwa anauza maji kufunga maarufu kama 'kandoro' au 'drip'.
 
Back
Top Bottom