Hii nchi watu wanataka kumnyonya mlala hoi kila siku iendayo kwa mungu,kwanza wanashangaza zaidi wanapomlazimisha kila mfanya biashara mwenye mauzo ya kuanzia shs 45,000 kwa siku kununua hicho kifaa lakini hawajali mtu huyu anapata faida shs ngapi kutoka katika mauzo hayo, halafu ana mtaji kiasi gani kwao siyo issue kabisa na atapata wapi pesa ili ununue hicho kifaa wao siyo issue kwao ikibidi hata mtaji wa mtu upungue au uishe kabisa wao hawajali wanachotaka ni wewe kununua kifaa hicho kwa laki nane ili mradi wauze hayo mavifaa yao.Vifaa hivyo mbaya zaidi siyo imara na maintenance coast once kikiharibika ni tshs 50000/=ambayo ni gharama ya mfanya biashara,huu ni unyonyaji wa kutisha.wafanya biashara wote k.koo asubuhi ya leo wamegoma kufungua maduka yao kwa madai ya bei juu ya mashine za EFD
source mimi mwenyewe nipo eneo la tukio
TRA wabadilike haraka na mashine zao
mambo haya yameanza Mbeya,Moro,
sasa Dar mwisho nchi nzima
Halafu tatizo lao ni porojo tu wakati
wafanyabiashara wamegundua kuwa
bei hii ya laki nane sio sahihi kabisa
Maana Kenya laki mbili,Dubai ndiyo
kama unakwenda kununua Toy.
Mtaji 500,000,mashine >800,000,Aisee MUNGU hebu shusha gharika tufe maana tumechoka na uonevu!
afu wakina barrick wanatuachia mashimo badala ya kwenda kuwakaba hao.
TRA kuna watu ambao wako ki rushwa zaidi. hawawezi kubuni mbinu mpya za kuongeza mapato. waachie ngazi damu changa ije na new ideas. makampuni ya simu yanakua na mkurugenzi mmpya every three four years wanaoleta new ideas mpaka bei ya kutwanga simu zimepungua sana. TRA the same old dogs miaka nenda miaka rudi. wanataka wafie ofcn bila hata kufaidi rushwa iliyolimbikizwa uswiss
Tatizo hapa c kutotaka
kulipa kodi, tatizo ni bei ya hizo mashine na inakuwaje muuzaji awe ni
yule tu aliyeamuliwa na tra? Na kuwa kila mwenye mauzo ghafi yanayofikia
tsh.45,000 kwa cku lazima awe na mashine hata mwenye genge, mama lishe ,
muuza mkaa anatakiwa awe nayo, na kuna wengine kama ni bar sehemu ya
bia iwe na mashine yake,jikoni hivyo hivyo! Na tatizo kubwa kuliko yote
ni kutoona manufaa ya hizo kodi wanazolipa zinakwenda wapi? Kila cku
mala bilioni 50 zimeliwa, akienda hospital hata panadol hamna!
Unajua wanapokesea TRA ni hapa;
Mfano wewe umekopa bank mil.20 ukaenda kununua mzigo wa kuuza, labda ndani ya mwezi mzigo umeisha mara 2 so umenunua mzigo mara 2, kwenye mauzo hii EFD itakuwa imetuma taarifa ya mauzo yote ya mwezi (20 mil x 2) wakati hapa unatarajia kurudisha mkopo wa bank na riba, ulipie kodi ya frem na umeme, ulipe wafanyakazi na bado wewe ubaki na faida. Sasa kwa sababu kila ninapoandika electronic receipt inatumwa wirelessly TRA (18% ya kila unachouza na kutoa risiti), wao wakija mwisho wa mwezi watasema nina mauzo ya mil 40 kitu ambacho sio sawa maana tunatakiwa tulipe kodi kutokana na faida mtu anayopata na siyo kutokana na mauzo, so hapa mtu alitakiwa ile faida ndo ipigiwe 18% ya TRA na sio huu utaratibu wa kila item kukatwa 18%
So leo hakuna mapato yoyote yaliyoingia TRA toka kwa wafanyabiashara wa Kariakoo maana mashine za wale walio nazo si wamefunga hawajauza? Wajipange.
Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
watu wote wanapenda kulipa kodi , lakini huwezi hela zako zikaenda katika mtiririko ambao siyo , wao wawauzie hivyo vimashine ila si kwenda kununua kwa watu wengine tofauti na tra , hapo ndiyo tatizo na wawaajiri wataalamu wakuzitengeneza wa kwao wenyeweHivi kwanini watanzania hatupendi kulipa kodi? Sijui tunafikiri maendeleo yatashuka kutoka mbinguni?