Wafahamu Wavuvi hawa Mashuhuri waliokuwepo kwe Noti ya Shilingi Mia Mbili

Teko Modise

JF-Expert Member
May 20, 2017
1,968
6,137
Mwishoni mwa miaka ya 1980, Benki Kuu ya Tanzania ilitoa noti ya Shilingi Mia Mbili. Noti hii maarufu upande wake mmoja ulikuwa na picha ya wavuvi wawili wakiwa wamebeba samaki mkubwa wakiwa wanaelekea nchi kavu.

Najua wengi wetu hatufahamu kwanini iliwekwa picha ya wavuvi wale? Basi jua haikuwekwa kwa bahati mbaya.

Kwanza kabisa, Picha ile iliwekwa ili kutangaza moja kati ya shughuli ya kiuchumi ifanyikayo hapa nchini. Kwakuwa tuna bahari, Maziwa na Mito basi shughuli ya Uvuvi lazma itafanyika.

Jambo la pili, picha ile ya wavuvi ni picha itokanayo na watu halisi kabisa. Wavuvi hao ni Abdallah Mohamed pamoja na Ibrahim Amanzi wavuvi waliojipatia umaarufu miaka ya 1970 mpaka miaka ya 1980.

Walikuwa ni wavuvi maarufu wenye kuipenda kazi yao hadi kufikia kuwa marafiki wa Rais wa wakati huo JK Nyerere.

Wengine walishuku hao walikuwa ni "wale jamaa zetu" lakini naambiwa hawakuwa.

Kwa mchango wao kwa Taifa, jumlisha ukaribu wao na Mwl Nyerere, wakawekwa kwenye noti ya shilingi 200.

748786E3-A4E3-46EE-8737-DD43916588DA.jpeg


My take: Kama ni uchawa basi hawa ndio walikuwa machawa kwelikweli sio hawa wa siku hizi wanaoishia kulipwa buku 7.
 
Mwishoni mwa miaka ya 1980, Benki Kuu ya Tanzania ilitoa noti ya Shilingi Mia Mbili.

Noti hii maarufu upande wake mmoja ulikuwa na picha ya wavuvi wawili wakiwa wamebeba samaki mkubwa wakiwa wanaelekea nchi kavu.

Najua wengi wetu hatufahamu kwanini iliwekwa picha ya wavuvi wale? Basi jua haikuwekwa kwa bahati mbaya.

Kwanza kabisa,Picha ile iliwekwa ili kutangaza moja kati ya shughuli ya kiuchumi ifanyikayo hapa nchini. Kwakuwa tuna bahari, Maziwa na Miti basi shughuli ya Uvuvi lazma itafanyika.

Jambo la pili, picha ile ya wavuvi ni picha itokanayo na watu halisi kabisa.

Wavuvi hao ni Abdallah Mohamed pamoja na Ibrahim Amanzi wavuvi waliojipatia umaarufu miaka ya 1970 mpaka miaka ya 1980.

Walikuwa ni wavuvi maarufu wenye kuipenda kazi yao hadi kufikia kuwa marafiki wa Rais wa wakati huo JK Nyerere.

Wengine walishuku hao walikuwa ni "wale jamaa zetu" lakini naambiwa hawakuwa.

Kwa mchango wao kwa Taifa, jlisha ukaribu wao na Mwl Nyerere, wakawekwa kwenye noti ya shilingi 200. View attachment 2549333

My take:
Kama ni uchawa basi hawa ndio walikuwa machawa kwelikweli sio hawa wa siku hizi wanaoishia kulipwa buku 7.
... Mzee wetu Mohamed Said ilimpita wapi hii asiianzishie uzi? Hii angeiandikia thesis kabisa hii.
 
Mwishoni mwa miaka ya 1980, Benki Kuu ya Tanzania ilitoa noti ya Shilingi Mia Mbili.

Noti hii maarufu upande wake mmoja ulikuwa na picha ya wavuvi wawili wakiwa wamebeba samaki mkubwa wakiwa wanaelekea nchi kavu.

Najua wengi wetu hatufahamu kwanini iliwekwa picha ya wavuvi wale? Basi jua haikuwekwa kwa bahati mbaya.

Kwanza kabisa,Picha ile iliwekwa ili kutangaza moja kati ya shughuli ya kiuchumi ifanyikayo hapa nchini. Kwakuwa tuna bahari, Maziwa na Miti basi shughuli ya Uvuvi lazma itafanyika.

Jambo la pili, picha ile ya wavuvi ni picha itokanayo na watu halisi kabisa.

Wavuvi hao ni Abdallah Mohamed pamoja na Ibrahim Amanzi wavuvi waliojipatia umaarufu miaka ya 1970 mpaka miaka ya 1980.

Walikuwa ni wavuvi maarufu wenye kuipenda kazi yao hadi kufikia kuwa marafiki wa Rais wa wakati huo JK Nyerere.

Wengine walishuku hao walikuwa ni "wale jamaa zetu" lakini naambiwa hawakuwa.

Kwa mchango wao kwa Taifa, jlisha ukaribu wao na Mwl Nyerere, wakawekwa kwenye noti ya shilingi 200. View attachment 2549333

My take:
Kama ni uchawa basi hawa ndio walikuwa machawa kwelikweli sio hawa wa siku hizi wanaoishia kulipwa buku 7.
Teko...
Mpashaji wangu kanieleza:
"Waziri akaniambia inanihitaji tusafiri pamoja twende Ulaya ya Mashariki kuna kozi inafungwa na sisi tumealikwa kwenye ufungaji.

Basi mimi na Waziri wangu tumekwenda.

Nilipata mshtuko mkubwa sana.

Katika kundi lile lililohitimu kozi ile niliwaona jamaa ambao mimi wakiniuzia samaki pale Ferry."
 
Mzee atakwambia ni watoto wa kleist
Sopho...
Watoto wa Kleist mimi ni baba zangu.

Napata akili zangu nawaona na nimeishi na wao kwa wema mkubwa sana hadi wote wamefariki.

Katika ihsani kubwa waliyonitendea mimi ni kule kukaa kitako na mimi wakanihadithia historia ya ukoo wao.

Katika historia hii vitu vitatu vilinichukua sana.

Kwanza maisha ya baba yao yatima ambaye alifiwa na baba na mama yake akiwa mtoto mdogo sana akalelewa na Affande Plantan mwanzoni mwa karne ya 20.

Pili maisha yao kama watoto hadi ujana wao na waliyofanya katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Katika haya nilipata pia kuyajua maisha ya baba yangu.

Tatu Abdul na Ally walivyokwenda vitani Vita Vya Pili Vya Dunia kama Burma Infantry.

Jinsi baada ya vita walivyompokea Mwalimu Nyerere miaka ya 1950 mwanzoni na yale waliyofanya pamoja katika kupigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana mwaka wa 1961.

Haya yalikuwa katika mazungumzo.

Ihsani kubwa waliyonifanyia ni kunifungulia nyaraka zao nizisome na kuniruhusu kuzitumia nipendavyo.

Ndiyo sababu niko hapa na nyinyi ndugu zangu sasa mwaka wa 10 na zaidi nakusomesheni historia ya Mwalimu Nyerere ambayo hakuna aliyekuwa anaijua kwa ithibati yake ila mimi.

Bwana Sapho....unaweza ukanikejeli mimi na wazee wangu hawa upendavyo sina uwezo wa kukuzuia wala sina uwezo wa kukurejeshea kejeli zako.

1678773680982.png

Kleist na watoto wake 1942
1678772937861.jpeg

Ally Sykes na Mwandishi Muthaiga Club, Nairobi 1989
Zb4ISXEkXAxRcOtrF2_h8d92Nzd57GqksDF8kzzOc3qdimGDxWxvE0tOjjQx3iVKe6fnX3a3kpYVk3uts3jo95YC9I7-Dbgan63taCP3OHB3IM8Kc2i5yZbGlul6H3cJhNVFLY4u1Mfo5KbXATs_M-VeKwurDfbBnKuHITYRPPsckf5X96k4CXnGNcKeP5tCgkI3cjYibY6FfG1xBnU8Y65B5JKF8fra-JSAc4D9mN7R_WLTDsuhKK-V3BTT3CUj2aVcaKD3mSHY-40gscbQETQWinGfM4ToCvcUVYziKCyai7TVfDjYJ5a62xyRdGzKAOLcew5D3w3Wh-eL4V_f_byw9E9hCzC5tfdfuU1hHQZ1ECzX_I_O2KxprMtFBcFXaSPVlfj71b4RJ6InQfTGHRsUpqKKrOd5ZhkaeQ7h_DIchvNvMiBI4EaWvOxXGGkC82iNCO38PhZsYJXd1Ybvyv29QYqKh5Z_kbRocZNlHqO7oGimR2TzPTbSwmmeyNJ6YnA0PTBKWXdCAE1XvmuzwwNF_bfelTyv8WsMyTITZ_lxLb-Wpe5Yw1yEm_sYu39_IFQ80GUVjtiunI2BCSGkK1J2bkHP1o4bzdLuBJfEn19boscIzrsWshC7jC9FOAlK8F5KynHCiNtHSKorvzvRuBySSwCiKtceFXkYivFlxOZIAS_PpwqfIfI6M1pN10TOoHt7HrYdBRrdo1RGDNHInlSUX8y5OX7Ux5bzuPaojEGDHY-LFozKXzBqKvDeepLq08ksmiHpIhsAjqz3MDlAi9p5xTaJ3YfbTijIwPLIELFEP8SM_tAtKufBENLPOUPNauXbHoQlCtnJamzJSTfFDkV2lpMPAi8Ft-N_ISfhXANxKrHL_6XQFtbjzLaO4bqaRMm9rmI-02PajKi4CXIFtN8UYwwippnkBnYLc3_QuF3431ljpKS-IZ44ES1TgT5Lo-Wj8BsRXdc9M8aTgg=w975-h650-no

Balozi Abbas Sykes na Mwandishi, Sea View Dar es Salaam 2012
 
mzee MOHAMEDI. naomba nikuambie jambo moja. kuna tofauti kubwa sana kati ya sisi tuliyozaliwa darusalaam, na wale waliyokuja darusalaam. maneno na majibu kama hayo utayapata kwa wale waliyokuja darusalaam. sisi tuliyozaliwa na kukulia jijini darusalaam tunayajua na tumeyashuhudia mengi katika machache unayoyasimulia. wengi wanaokupinga, ukiangalia uzao wao unaanzia miaka ya 90 kuja 2000. hawana walijualo ktk unayoyasimulia. tena huko mashuleni, wengi wao walikuwa wanakaa madawati ya nyuma. lakini kwavile wanamiliki smartphone, wana haki yaku....... wanachokiamini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom