Shamkware
JF-Expert Member
- Nov 25, 2013
- 1,740
- 2,243
Habari wakuu,
Niende moja kwa moja kwenye maada.
Hivi sasa tunatambua bodaboda imekuwa ni kazi inayowasaidia vijana wengi sana kujikwamua kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu kitu ambacho ni kizuri sana.
Lakini kazi hii baadhi ya maeneo inafanywa kwa kukosa weledi na maarifa ya kibiashara, sijui ni kwa sababu wamekuwa wengi sana au tatizo nini?
Nakereka na tabia ya vijiwe vya bodaboda yaani mtu ukitokeza tu kwenye kona wanaza kukupigia honi na miluzi utafikiri mbuzi au mbwa kaiba mboga wengine kukukimbilia hovyo hovyo. Hivi kwanini msitulie tu kijiweni abiria si tunajua mnapopatikana.
Saa nyingine maeneo ya usafiri ukishuka tu kwenye gari kelele kibao za bodaboda na ukizubaa tu mara huyu kasha chukua na begi yaani tabu tupu.
Kwanini msitulie kijiweni mkawa mnabeba abiria wenu vizuri kwa zamu, akija abiria anaenda na huyu, akija mwingine anaenda na huyu mnakuwa na rotation nzuri kwa ustaarabu ili kila mtu apate mkate wa kila siku hizi papara zenu zina boa bana.
Nawapongeza bodaboda wa Mwanza na Tabora kidogo watulivu na hizi tabia ni chache kwao kama sio hawana kabisa.
Lakini baadhi yenu badilikeni, Pia vaeni vizuri hiyo ni kazi kama kazi nyingine mnajirundika makoti machafu na kofia za hovyo na hiyo miziki ya ajabu ajabu tena kwa sauti ya juu plus kuendesho hovyo.
Niende moja kwa moja kwenye maada.
Hivi sasa tunatambua bodaboda imekuwa ni kazi inayowasaidia vijana wengi sana kujikwamua kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu kitu ambacho ni kizuri sana.
Lakini kazi hii baadhi ya maeneo inafanywa kwa kukosa weledi na maarifa ya kibiashara, sijui ni kwa sababu wamekuwa wengi sana au tatizo nini?
Nakereka na tabia ya vijiwe vya bodaboda yaani mtu ukitokeza tu kwenye kona wanaza kukupigia honi na miluzi utafikiri mbuzi au mbwa kaiba mboga wengine kukukimbilia hovyo hovyo. Hivi kwanini msitulie tu kijiweni abiria si tunajua mnapopatikana.
Saa nyingine maeneo ya usafiri ukishuka tu kwenye gari kelele kibao za bodaboda na ukizubaa tu mara huyu kasha chukua na begi yaani tabu tupu.
Kwanini msitulie kijiweni mkawa mnabeba abiria wenu vizuri kwa zamu, akija abiria anaenda na huyu, akija mwingine anaenda na huyu mnakuwa na rotation nzuri kwa ustaarabu ili kila mtu apate mkate wa kila siku hizi papara zenu zina boa bana.
Nawapongeza bodaboda wa Mwanza na Tabora kidogo watulivu na hizi tabia ni chache kwao kama sio hawana kabisa.
Lakini baadhi yenu badilikeni, Pia vaeni vizuri hiyo ni kazi kama kazi nyingine mnajirundika makoti machafu na kofia za hovyo na hiyo miziki ya ajabu ajabu tena kwa sauti ya juu plus kuendesho hovyo.