Wadi mpya Muhimbili 'hazina vyoo'!

Wadi mpya Muhimbili 'hazina vyoo'!

Tatizo watu sio wabunifu, wanasubiri JPM aje kuwaambia la kufanya.

Watumie vyoo vya muda mfupi wakati ujenzi wa vyoo vya kudumu unaendelea, acheni ugoigoi
Kaka watu wamechoka especially hawa madaktari usiseme. Waliopo wanafanya kazi haswa lkn hata mazingira ya kazi kuboreshwa inakuwaje ngumu hiyo ilikuwa ndani ya almost 15yrs ago sasa hivi unakuja unakurupushwa na speed ya Magu, hahahaha.

Hawa viongozi wa kwenye wizara wala rushwa ndiyo mabongolala wa kutupwa. Zero hamna kitu
 
Watanzania hamna shukrani.ushasema mafundi ndio wanajenga sasa unataka nini?


Genius;
Ni kweli unasema au nadhania tu?? Ati Watanzania hamna shukrani. Yaonesha huenda weye ni mangi. Ndo huwa wanasema aksante hata kabla hajakipokea.
Ee bwana eee; jamaa kasema, tatizo ni kukurupushwa. Hao wamama si walikuweko tangu siku akanyage pale siku ya kwanza alipomfuta kazi mkurugenzi yuleeee. Sasa, atamrudisha au?? Kwani kilichomnyima ugali ni hao hao wamama kulala chini. Sasa kilichowafukuza ofisini ni wamama hao hao. Swali ni je, ofisi hiyo kuwa wodi ndo suluhisho?? Tulisema jamani, vitanda sio suluhisho, mkatusema, leo tumesema kuvunja ofisi nalo sio suluhisho. Tanzania hakuna maofisa mipango. Nasema, mlioko ni magumashi tuuuuu.
Ona maji ya mchina, ubungo na kwingineko. Mabomba mpaka yanaozea ardhini. Kwingine kumeachwa mahandaki hatari kwa maisha ya watu. Hata tone la maji hakuna, ni miaka sasa, kuna nini?? Muhumbili hakujaanza jana kujaa, kuna nini?? Suluhu ni kujenga wodi nyingine, kuajiri watendakazi mahiri wa nyongeza nakuimarisha hospitali na vituo vya afya vilivyo kando kando ya Muhumbili.
Magari yawepo pale kuwachukua wamama wajawazito wanaoingia Muhumbili huko ili wajue kuwa hata huko zipo huduma nzuri ka Muhumbili.
Si vinginevyo
 
wakina mama wanalalamika. tena mmoja kasisistiza, 'maamuzi yawe yanafanyika kwa umakini'

Walikuwa wakilala chini tena huku maji ya vyooni yakitirirka sakafuni,sasa wamepata wadi nzuri ina vitanda,na vyoo vinajengwa na soon vitakamilika,bado walalamike? Huo wa kwako ni ujinga shatashata uliokolea viungo.
 
Huko walipokuwa wanalala chini kulikuwa na vyoo vya kutosha?
Lazima kuanzia mahali fulani
 
Akiongea kwa mbwembwe na Wazee wa Dar, rais JPM aliagiza ofisi za taasisi ya afya ya mama na mtoto zibadilishwe matumizi na kuwa wadi za akina mama walioielemea MNH mpaka kulala chini. Cha kusikitisha ni kuwa hakuna huduma nzuri ya vyoo; kwanza havitoshi (mafundi ndiyo wanajenga), havina hadhi ya kutumiwa na akina mama. Wanatumia vyoo vya nje vilivyo mbali na wadi hiyo mpya! Wamejazana kiasi ya wengine kushindwa kuvumilia na kuachia haja (ndogo) pasipo na choo.

Jamani, kuna magonjwa ya mlipuko. Fanyeni hima.

chanzo: EATV
Mimi mwenyewe nimeangalia habari hiyo na wameonesha vyoo viki karabatiwa kuendana na mahitaji ya wahusika....

Kwa sasa wanatumia vyoo vingine japo wanapata shida!
 
Kama vyoo hakuna hao waliokua hapo ofisini walikua wanajisaidia uchochoroni???mwaka huu mtaisoma namba tuu na lazima mnyooke, wabongo mlikua kazi hamfanyi mmekalia umbea na wizi tu...Ngosha aendelee kutumbua majipu tuu...awamu hii lazima muombe poo.LOL
 
Mkuu imekugusa nini, hili agizo ni zuri sana. Patient oriented services.
 
Umesema hazina vyoo na mafundi ndio wanajenga, sasa hapo tatizo liko wapi so watajenga vitaisha na kinamama wataanza kutuma...kumbuka zilikuwa ofisi na sasa zimekuwa wodi huoni lazma kuna mabadiliko yafanyake ili ofisi hizo zifanye kazi mpya, au ulitaka Magu awe kama Mungu aseme na sasa ofisi ziwe wodi na ghafla kila kitu kiwe sawa..

Hhhhhh....umenifurahisha mkuu...
 
Waliokuwa wanafanya kazi humo walikuwa wanaenda kujisaidia wapi? Lakini kama umesema 'havitoshi' ni jambo jingine maana umesema 'mafundi ndio wanajenga'. Ndio maana ya kuwapa watu changamoto.. ulitaka Magufuli awajengee na vyoo? Yeye katoa agizo ni jukumu la watendaji wengine kuhakikisha agizo la Rais linatekelezwa na linatekelezeka.
"If you can't beat them,............"
Naona umefanya kweli mzee menzangu!
Habali ya siku zilee, uko poa, mkijiji?
Angalia shilingi zako mbili, wajanja wanazitupia jicho!
 
Niko hapa MNH naangalia pilika zinavyoendelea. Hakuna nurses wa kutosha kuwa Na ward nyingine ghafla. Hawa kina mama wanaweza kupata tatizo wakiwa wenyewe
Kwa nini hawawapigi kozi ya "fasta" hao wanaochukua kozi ya ukunga ili waje huku kwa kinamama kuwapa "maisha bora"?
 
Sisi yetu macho na masikio.
Mkuu kipindupindu hicho kinarejea tena kutokea Muhimbili.
Ndio madhara ya mbwembwe hayo. Hivi dunia ya leo ukiona mtu anahamia kwa matambo nyumba yake mpya lakini kumbe haina vyoo anashusha kwenye mifuko ya rambo utamweka kundi gani?
 
Zikikuwa ofisi na vyoo vyake vichache... sasa imekuwa wodi... vyoo si ndiyo vinaongezwa kwa kujengwa... mdomo na kimbele mbele cha nini sasa... utalazimisha tofali na cement kukauka unavyotaka wewe...
 
ni dharula sio mbaya mambo yatakua poa soon wameamia kwa mpito vyoo vinajengwa tuliza presha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom