Ndoa ni Kitu kingine kabisaa, sio suala la kumlazimisha mtu. Kumbuka huyo unaejilazimisha kwake utaishi nae miaka yako yote ilobaki, sasa kama hakupendi mtaishije humo ndani????
Hii tabia wanayo wadada wengi kwa kweli hasa wakiona kijana ana uwezo. Tunasahau kuwa ndoa ni zaidi ya mali. Hili linapelekea ndoa nyingi kukosa mwelekeo sababu mmoja wao hakuwa tayari.
Jamaniiii, ndoa huwa hailazimishwi kabisaa. Ukilazimisha madhara yake ni makubwa mnoo, inawaathiri hata watoto wasio kua na hatia.
Tubadilike kama ndoa yako ipo ipo tuuu