Wadada tusilazimishe ndoa

Wadada tusilazimishe ndoa

Kidogo watie moyo wenzio sio wakiona sofa na kitanda wanajua ndo mwanaume umeshajipanga.
 
Habari MMU,

Nimekutana na hii story kwenye group letu uko mdada anasema anapendana vizuri na mpenzi wake na kila mtu anaishi kwake wapo kwenye mahusiano kwa muda mrefu sana. Anasema mwanaume ana kazi nzuri sana ana kila kitu ila akimwambia amuoe mwanaume anamwambia hajajipanga na kuna muda wanagombana akianzisha swala la ndoa.

Wadada wenzangu ndoa hailazimishwi kabisa mwanaume mwenyewe atakuja atakwambia baby nahitaji kukuoa naomba unipeleke kwenu. Haya mambo ya kumlazimisha mwanaume mwisho wa siku ndoa haina amani mwanaume kukurudia usiku wa manane ukimuuliza na kupigwa utapigwa.

Kingine kama Mungu kakuandikia wewe ni wa kuolewa utaolewa tu kama ni wa kudanga utadanga tu, tusikate tamaa hata umri ukienda vipi ipo siku tu.
Jaman wadada kuwa vzr kiuchumi sio ndio tayar kuoa, hayo maswal yanatuchosha mtaan yaani kila KE ukimgusia tu unasikia unamalengo gani na mm. Sasa kwan kila KE ataolewa? Wengine watabaki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom