Wadada mnisamehe kidogo!

Wadada mnisamehe kidogo!

Simwongelei mtu ni ujumbe kutoka kwa mdau wa masuala ya wanawake anaitwa
Lu-Patie!

Wanaume wengi hawajafikia ndoto zao, wanatamani kupata wanawake watakaowatia moyo kuwafikisha kwenye ndoto zao! Ukweli mchungu ni kwamba wanawake hawawataki wanaume ambao bado wako safarini kuelekea ndoto zao! Wanataka waliokwisha fika, na bahati mbaya zaidi waliokwisha fika wako 'occupied !! Linalotokea ni nini?! Wanawake wanadhani wana bahati mbaya ?!

Unaweza kuwa unalalamika kuwa una mkosi WA kuolewa yaani kila mwanaume anakuja na ahadi nzuri, baadae anakuacha! Lakin upande mwingine huenda maamuzi yako ndiyo maumivu yako.

Kweli huenda we ni mtoto WA kike mzuri wa sura umbo na hata kila kitu ila umenyimwa hekima!

Una mpaparikia kijana mtanashati kisa ana gari na kazii nzuri. Unamwona kijana anaeenda kumbi za usiku ndo mjanja..anae vaa suruali chini ya makalio ndo sahihi kwako lakini yule anaeenda ibada kila ijumaa au jumapili unamwona mruga ruga tu!

Una mpuuza Na kumdharau mtu 'A' kisa tu yeye ni kijana aliye soma ila hana ajira. Ama ni kijana ambae kipato chake hakizidi laki 2 kwa mwezi badala yake una mkumbatia mtu 'B' ambae ni baba fulani na ni mume WA Fulani kisa tu anapesa na shida zako zote anakutatulia...!!

SWALI!!
Utaolewa vipi ikiwa mpaka sasa unapenda toka na waume za watu au vijana wenye magari ya mikopo, au kijana yeyote ambaye unajua huna future naye? Au ndo unam'please ili asiache kukupa pesa!? Nani atakae KUOA wakati vijana wanaotafuta mke wewe una wasema vibaya kuwa hawana hadhi ya kutembea na wewe kisa hawana misuli ya uchumi kwa muda huo?

Funguo ya NDOA utaipata wapi wakati hapo ulipo una mnunia mke wa mtu kisa una toka na mume wake?

DADA maisha yanabadilika mwanaume mpiga debe wa Leo kesho unaweza mbadilisha akawa dereva kisha akamiliki gari lake...hakuna MTU aliye zaliwa kuwa masikini ndo maana juhudi zinahitajika...Mwanaume anae tumia pesa kukufanya uwe wake anafanya hivyo kwa wengi ila usijifanye hujui kisa unafaidika jua muda unaenda.

Weka malengo mbele lini unatamani uwe na ndoa na umri gani uzae kuliko anasa. Mwaka WA ngapi huu bado unatoka na wanaume ambao hawana malengo Na wewe, kazi ni pombe na wanawake?

Umegombana Mara ngapi na Huyo HB wako kisa usaliti na bado upo nae?? Wanaume wangapi wenye pesa mvuto na kila kitu ndani lakin wamekutumia na kukuacha? Lakini bado hujifunzi aina ya mwanaume wa kuwa nae?

Japo vyema acha kujidharau u mrembo onesha kwamba unajipenda kuanzia MAVAZI NA KAULI !
Marafiki zako wangapi waliolewa na wanaume WA kawaida lakin Leo wana mafanikio? Kwa nini usiige..weka uzuri pembeni simama imara kama MKE na MAMA bora WA kesho. Mtie moyo mmeo ajisifu kuwa Na wewe, si kila mara dharau Na kumbeza!!

Kifupi hakuna mwanamme anayependa mke asiyemtia moyo kwa kile kidogo anachofanikiwa kufanya !! Encouragement matters most kwa mwanamme yeyote mwenye akili timamu!
Asante kwa neno mkuu
 
Mawazo kama haya jana nimemwambia mchumba wangu kuwa kama ataendelea na tabia ya kunichit kila muda itafika pahara nisimsamehe tena na moyo wangu ukisha geuka haurudi nyuma. Mimi napenda msichana mwenye kutambua thamani yake na mwenye mawazo ya kimaendeleo hata kwa mtaji wa 10000. Sio kila mda ninunulie gauni lile mara nipeleke kwenye chips.
Aiseee anakuchit na unajua
Kabsa na Bado unamsamehe
Na c mara moja aiseee

Kweli moyo ukipenda co
Mchezo

Ama kweli kipendacho roho
Hula nyama mbich
 
Uko sawa, na sisi wanaume saa ingine tunayasababisha haya.
Ndio mkipendwa hamtaki halafu wadada wengi wanachuna mahali wanawaletea nyie ambao hamna .
Halafu nyie mnawapa vimeo ambao hamna mpango nao kero tu ambao mkiishiwa wanawaacha mmtuchosha.
 
Nilipokuwa nasoma shule nilimpata mwanaume hata nguo hna nilimsaidi mpaka akajitambua akasoma akapata mzungu na akaniacha mimi nasaga viatu.
Wanaume maskini ndio wanashida kuliko wenye nazo.
Kwa hiyo bora mtu apate mtu wa saizi yake .
Tu tena nyie wanaume walokole kerooo kuliko wavuta bangii.
Mnakero shida ukiwa nao nitabu tupu ukiolewa nao watoto wanachanganyikiwa hamtajielewa mnataka nini .
Yaani bora ule raha upewe kila kitu .
Uwachune wakuchune basii uolewe muda ukifika watu ni hovyo unaweza kuwa namtu mzima unadhani mnapanga maisha kumbe kachanganyikiwa.
So becareful sio unatusema huku nyie ndio mnatabu.
Hapo ndipo shida inapoanzi mnapata shida weeee siku kazipata nyingi anakutafutia mchepuko eti pesa yote hii mke 1 haa, kasahau wakati kapuku hakuna aliye mpenda, yeye anitafutie tu nitumie siumizi kichwa, mie katokea atokako eti nakupenda siku 1 eti hama kwenu nenda kapange halafu tutakuja kuishi wote nilicheka kweli
 
Si mara ya kwanza nauona huu uzi. Nadhani niliuona last year, but ni ujumbe mzuri sana worth reading and remembered not only by girls.
 
Very true.

We are women bana.

We give birth to fellow human beings. Thats just how powerful we are.

If we give life, then we can make or break a man.

Let us choose to make than break.
 
Mawazo kama haya jana nimemwambia mchumba wangu kuwa kama ataendelea na tabia ya kunichit kila muda itafika pahara nisimsamehe tena na moyo wangu ukisha geuka haurudi nyuma. Mimi napenda msichana mwenye kutambua thamani yake na mwenye mawazo ya kimaendeleo hata kwa mtaji wa 10000. Sio kila mda ninunulie gauni lile mara nipeleke kwenye chips.
ana kucheat then mpka sasa bado upo nae mkuu ..huko anapokwendaga sidhani kama huwa anakumbuka kuweka msimamo wakuingiliwa na condom..kuwa makini atakuja kukuuwa huyo ..shauri yko
 
mkuu ni mara nyingi tu ila kwa kushuhudia mwenyewe ni mara tatu
hiii jamaaa una roho ngumu ..yaani umegongewa mpka unashuhudia mwenyew na bado unasamehe tena Mara 3 ...huyo mwanamke amekulisha Nyama ya kalio au ??
 
Back
Top Bottom