Mwanamke mshamba, na huyo aliyemtoa out naye mshamba. Mwanamke hayuko food conscious. Dunia ya leo, iliyojaa matatizo ya mabalaa ya njaa, mabadiliko ya tabia nchi, kuacha chakula hivyo ni sawa na kuwatusi wasio na chakula, na kuitusi dunia kwa rasilimali zilizotumika kuzalisha na kusafirisha malighafi iliyotumika kuwezesha hizo chips, kuku n.k. Aliyemtoa out ni mshamba kwa sababu out gani ya kwenda kula junk food? Yaani hadi leo watu bado wanaenda out za kula makuku ya KFC? Hapo nafikiri si chini ya buku mbawa zilimtoka. Sasa kwa elfu 20, si angepata organic food safi kabisa na juisi orijino na chenji kubaki?
Ewe mtanzania, kwenda kula KFC, Merry Brown, Subway, Burger King, Macdonald n.k., siyo ufahari au umatawi ya juu. Ni ushamba na ulimbukeni. Ndiyo maana kila kukicha tatizo la obesity linaongezeka. Mtaanza kupukutika kwa vifo vya ghafla kutokana na magonjwa ya pressure!
Elimu ya lishe bado ni changamoto kwa wengi wetu. Enyi wazazi jitahidini mjenge taifa la kesho lenye watu walio na afya njema. Yaani upatikanaji wa organic food ni wa bwerere, halafu mtu anaenda kujifakamia junkies za bei mbaya.