Pedra buyer
Member
- Apr 26, 2015
- 97
- 32
Habari zenu wana Jf,
Mke wangu kwa nini unafanya hivyo? Ni swali ninalojiuliza kila ninapomkumbuka,hakuna ambacho anakosa lakini anafanya mambo ya aibu roho inaniuma sana.Nilipigiwa simu nikiwa kazini ilihitaji nifike haraka nyumbani kuna tatizo, baada ya kufika nilishangaa kukuta watu kibao wakishuhudia vijana wawili wakipiga na kutoana damu nyumbani kwangu.
Nilimuuliza mmoja wa majirani zangu kuna nini nikaambiwa muulize mkeo! Mda huo mke wangu alivyoniona kakimbia sikujua kaelekea wapi, nikamuuliza dada wa nyumbani akaniambia "dada alitoka aliporejea alikuja na na mkaka mmoja alinionesha kwa kidole mara gafla ilikuja gari ndogo akashuka kijana yule mwingine na wenzake ndipo walipomuita dada nje alitoka wakiwa wameshikana na na mkaka alioingia naye.
Ndipo ugomvi ulipoanza mmoja akimshutumu mwenzake kwa mini unatembea na mpenzi wangu ndipo walipoanza kutukanana na kupigana''. Ni siku ya tatu leo tangu kutokea kwa tukio nimeshindwa kuchukua uamuzi wa aina yeyote sielewi nifanye nini na ndugu wa mke wangu wananiomba tukae tuyaongee, sasa nawauliza tuongee kuhusu nini? Eti tumuombee msamaha yaishe wakati sikumfukuza wala kumpiga kaondoka mwenyewe.
Naombeni ushauri, maana kila maamuzi nayotaka kuchukua naona sheria itanibana.
Mke wangu kwa nini unafanya hivyo? Ni swali ninalojiuliza kila ninapomkumbuka,hakuna ambacho anakosa lakini anafanya mambo ya aibu roho inaniuma sana.Nilipigiwa simu nikiwa kazini ilihitaji nifike haraka nyumbani kuna tatizo, baada ya kufika nilishangaa kukuta watu kibao wakishuhudia vijana wawili wakipiga na kutoana damu nyumbani kwangu.
Nilimuuliza mmoja wa majirani zangu kuna nini nikaambiwa muulize mkeo! Mda huo mke wangu alivyoniona kakimbia sikujua kaelekea wapi, nikamuuliza dada wa nyumbani akaniambia "dada alitoka aliporejea alikuja na na mkaka mmoja alinionesha kwa kidole mara gafla ilikuja gari ndogo akashuka kijana yule mwingine na wenzake ndipo walipomuita dada nje alitoka wakiwa wameshikana na na mkaka alioingia naye.
Ndipo ugomvi ulipoanza mmoja akimshutumu mwenzake kwa mini unatembea na mpenzi wangu ndipo walipoanza kutukanana na kupigana''. Ni siku ya tatu leo tangu kutokea kwa tukio nimeshindwa kuchukua uamuzi wa aina yeyote sielewi nifanye nini na ndugu wa mke wangu wananiomba tukae tuyaongee, sasa nawauliza tuongee kuhusu nini? Eti tumuombee msamaha yaishe wakati sikumfukuza wala kumpiga kaondoka mwenyewe.
Naombeni ushauri, maana kila maamuzi nayotaka kuchukua naona sheria itanibana.