Wachambuzi wetu wanachumbua dereva wa bodaboda apigwe na dereva wa fuso

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,315
12,614
Nimeshuhudia dereva wa lori akichomolewa na kupigwa na dereva wa bodaboda baada ya dereva wa lori kumsukumia mtaroni dereva wa bodaboda.

Sio kwamba timu ikiwekeza sana lazima mara zote iifunge timu yenye uwekezaji mdogo. Wachambuzi wetu wanazilazimisha Al-Ahly na Mamelodi izifunge Simba na Yanga kwenye mashindano ya CAF champions eti kwakuwa zina uwekezaji mdogo kuliko al-ahly na mamelodi. Uchambuzi wa aina hii hauonyeshi weledi. Wachambuzi wanasahau factors za muunganiko wa timu, ari za wachezaji (self motivation) na uzuri wa mabenchi ya ufundi ya kila timu.

Ni kweli uwekezaji wa lori ni mkubwa kuliko uwekezaji wa bodaboda na ni kweli lori linapoigonga bodaboda mara zote lori litaiharibu zaidi pikipiki, lakini sio kweli kwamba mara zote dereva wa lori ana nguvu zaidi kuliko dereva wa bodaboda.

Timu zote zina wachezaji waliozifikisha timu zao robo finali, Pale uwanjani wanacheza wachezaji (madereva) sio pesa (malori na bodaboda).
 
Hakuna mchambuzi huko ulaya atasema Man city atafungwa na RB leipzig. Ukweli utabaki hivyo timu yenye uwekezaji mkubwa ndio yenye nafasi kubwa ya kushinda hata kama matokeo yatakuwa tofauti. Ndio maana hata wewe unategemea ushindi kwa yanga ikicheza dhidi ya Ihefu .
 
Hakuna mchambuzi huko ulaya atasema Man city atafungwa na RB leipzig. Ukweli utabaki hivyo timu yenye uwekezaji mkubwa ndio yenye nafasi kubwa ya kushinda hata kama matokeo yatakuwa tofauti. Ndio maana hata wewe unategemea ushindi kwa yanga ikicheza dhidi ya Ihefu .
Huo mfano wako hausadifu hiki ninachokisema hapa. Simba, Yanga, Al-Ahly na mamelodi ni timu ambazo ziko robo finali ya CAF champions, hii inatosha kumfanya mchambuzi mwenye akili kuwa hizi timu uwanjani ziko na ulinganifu hata kama kwenye uwekezaji (pesa na majengo, miundombinu) zimezidiana sana. Kama ni swala la kuwekeza tu ziko timu ambazo zimewekeza sana kuliko simba na yanga lakini hazifika hatua hii ya robo finali, hivyo Kwa mchambuzi mwenye utimamu wa mwili na akili ingetosha kuondoa factor ya uwekezaji na kubakiza factors za upambanaji kiwanjani, teamwork, mbinu za mabenchi ya ufundi na mchango wa mashabiki uwanjani.

Huo mfano wako wa Man city na RB Leipzia ni mwendelezo wa ukosefu wa weredi kwenye uchambuzi kwakuwa Man city na RB haziko zote kwenye robo final ya EUFA champions kama zilivyo simba na al-ahly.

Ukiona mchezaji anacheza Afrika kiwango chake bado ni cha Afrika tu, wachezaji bora duniani wamenyakuliwa na timu za Ulaya, timu zetu za Afrika zina wachezaji wanaolinganalingana na kuzidiana tu viwango vya kujituma, motivation wanazopewa (pesa, mazingira na mabenchi ya ufundi).
 
Nimeshuhudia dereva wa lori akichomolewa na kupigwa na dereva wa bodaboda baada ya dereva wa lori kumsukumia mtaroni dereva wa bodaboda.

Sio kwamba timu ikiwekeza sana lazima mara zote iifunge timu yenye uwekezaji mdogo. Wachambuzi wetu wetu wanazilazimisha Al-Ahly na Mamelodi izifunge Simba na Yanga kwenye mashindano ya CAF champions. Uchambuzi wa aina hii hauonyeshi weledi. Wachambuzi wanasahau factors za muunganiko wa timu, ari za wachezaji (self motivation) na uzuri wa mabenchi ya ufundi ya kila timu.

Ni kweli uwekezaji wa lori ni mkubwa kuliko uwekezaji wa bodaboda na ni kweli lori linaigonga bodaboda mara zote lori linapogongana na pikipiki, lakini sio kweli kwamba mara zote dereva wa lori ana nguvu zaidi kuliko dereva wa bodaboda.

Pale uwanjani wanacheza wachezaji (madereva) sio pesa (malori na bodaboda).
Pale EPL sijawahi kusikia wachambuzi wanasema Crystal Palace kamwe haiwezi kuifunga Man City. Huu upuuzi uko Tanzania tu.
 
Huo mfano wako hausadifu hiki ninachokisema hapa. Simba, Yanga, Al-Ahly na mamelodi ni timu ambazo ziko robo finali ya CAF champions, hii inatosha kumfanya mchambuzi mwenye akili kuwa hizi timu uwanjani ziko na ulinganifu hata kama kwenye uwekezaji (pesa na majengo, miundombinu) zimezidiana sana. Kama ni swala la kuwekeza tu ziko timu ambazo zimewekeza sana kuliko simba na yanga lakini hazifika hatua hii ya robo finali, hivyo Kwa mchambuzi mwenye utimamu wa mwili na akili ingetosha kuondoa factor ya uwekezaji na kubakiza factors za upambanaji kiwanjani, teamwork, mbinu za mabenchi ya ufundi na mchango wa mashabiki uwanjani.

Huo mfano wako wa Man city na RB Leipzia ni mwendelezo wa ukosefu wa weredi kwenye uchambuzi kwakuwa Man city na RB haziko zote kwenye robo final ya EUFA champions kama zilivyo simba na al-ahly.

Ukiona mchezaji anacheza Afrika kiwango chake bado ni cha Afrika tu, wachezaji bora duniani wamenyakuliwa na timu za Ulaya, timu zetu za Afrika zina wachezaji wanaolinganalingana na kuzidiana tu viwango vya kujituma, motivation wanazopewa (pesa, mazingira na mabenchi ya ufundi).
Sijui unaandika manini wewe jamaa.Kwa hiyo Copenhagen alivyokutana na Man city hatua ya 16 uefa champions unafikiri kuna mchambuzi yoyote aliitabiria copenhagen ushindi? Sijui unafikiri vipi wewe jamaa, unaposema wachezaji wanaocheza Afrika hawajazidiana viwango.Ni rahisi mchezaji wa mamelod au Al ahly kucheza ulaya tena epl ila hao wachezaji wako wa simba na yanga hata kusajiliwa championship ni ngumu.
 
Sijui unaandika manini wewe jamaa.Kwa hiyo Copenhagen alivyokutana na Man city hatua ya 16 uefa champions unafikiri kuna mchambuzi yoyote aliitabiria copenhagen ushindi? Sijui unafikiri vipi wewe jamaa, unaposema wachezaji wanaocheza Afrika hawajazidiana viwango.Ni rahisi mchezaji wa mamelod au Al ahly kucheza ulaya tena epl ila hao wachezaji wako wa simba na yanga hata kusajiliwa championship ni ngumu.
wacha 16 bora, linganisha timu ambazo zimefika zote robo, nusu au finali halafu useme upuuzi kama huo. Hata Al-Ahly na Mamelodi wenyewe hawasemi upuuzi kama huo; maana Al-Ahly wasingehangaika kuja na mapipa kwenye ndege kama wangekuwa wanafuata wanachosema wachambuzi wetu wa mchongo.
 
Sijui unaandika manini wewe jamaa.Kwa hiyo Copenhagen alivyokutana na Man city hatua ya 16 uefa champions unafikiri kuna mchambuzi yoyote aliitabiria copenhagen ushindi? Sijui unafikiri vipi wewe jamaa, unaposema wachezaji wanaocheza Afrika hawajazidiana viwango.Ni rahisi mchezaji wa mamelod au Al ahly kucheza ulaya tena epl ila hao wachezaji wako wa simba na yanga hata kusajiliwa championship ni ngumu.
Afrika kuna mataifa mengi yenye timu zilizoshiriki mbio za caf champions, lakini ni 8 tu zimefika hatua ya robo finali. Hii ina maana kuwa wachezaji wa timu hizi 8 wana uwezo uliokaribiana sana hata kama timu zina ukubwa wa uwekezaji unaotofautiana sana. Kuna timu zimewekeza (tajiri) sana kuliko Simba na Yanga lakini haziko kwenye robo finali. Wachambuzi wetu wanajikita kwenye ukubwa wa uwekezaji badala ya kuangalia sababu zilizozifikisha timu 8 hatua ya robo fainali.

Wachezaji wazuri saaaana wamenyakuliwa na timu za ulaya, hawa tulionao ni walewale tu wanaotofautiana viwango vya kujitahidi na bahati nzuri kazini.
 
Hakuna mchambuzi huko ulaya atasema Man city atafungwa na RB leipzig. Ukweli utabaki hivyo timu yenye uwekezaji mkubwa ndio yenye nafasi kubwa ya kushinda hata kama matokeo yatakuwa tofauti. Ndio maana hata wewe unategemea ushindi kwa yanga ikicheza dhidi ya Ihefu .
Ghafla unaisahau timu ambayo imecheza robo finali mara 4 mfululizo na ghafla umeshaisahau timu ambayo imecheza finali caf confederation, huu ni utoto au uzembe katika mambo? Inamaana kuwa hizi timu zinahitaji kurekebisha makosa madogomadogo sana ili kuvuka hatua walizokwamia huko nyuma.
 
Jana kwenye kipindi cha soccer Africa dstv mtangazaji wa SA alijipa matumaini kabisa wataifunga Andorra bao 5, akaamini kabisa watacheza michezo yao kama ya Skudu kuburudisha lkn kuna mzee Mamadou aliwaambia soka alipo hivo na akapredict ni droo. Walimuona mpumbavu lkn mwisho wa siku ni droo.
 
Hakuna wachambuzi Tanzania
Huwezi kuona wanachuzi kama Ian Wright, Michael Owen, Carragha
Wanaonesha mapenzi ya team fulani
Nakumbana kuzishusha nyingine kwa kuzikatisha tamaa na uzushi

Kama wafanyavyo pale EFM
 
Hakuna wachambuzi Tanzania
Huwezi kuona wanachuzi kama Ian Wright, Michael Owen, Carragha
Wanaonesha mapenzi ya team fulani
Nakumbana kuzishusha nyingine kwa kuzikatisha tamaa na uzushi

Kama wafanyavyo pale EFM
With all due respect umemtaja na Owen kama mchambuzi mzuri? Ajabu. Au kwa vile anaongea kingereza. Huyo ni kama Oruma tu
 
Nimeshuhudia dereva wa lori akichomolewa na kupigwa na dereva wa bodaboda baada ya dereva wa lori kumsukumia mtaroni dereva wa bodaboda.

Sio kwamba timu ikiwekeza sana lazima mara zote iifunge timu yenye uwekezaji mdogo. Wachambuzi wetu wanazilazimisha Al-Ahly na Mamelodi izifunge Simba na Yanga kwenye mashindano ya CAF champions eti kwakuwa zina uwekezaji mdogo kuliko al-ahly na mamelodi. Uchambuzi wa aina hii hauonyeshi weledi. Wachambuzi wanasahau factors za muunganiko wa timu, ari za wachezaji (self motivation) na uzuri wa mabenchi ya ufundi ya kila timu.

Ni kweli uwekezaji wa lori ni mkubwa kuliko uwekezaji wa bodaboda na ni kweli lori linapoigonga bodaboda mara zote lori litaiharibu zaidi pikipiki, lakini sio kweli kwamba mara zote dereva wa lori ana nguvu zaidi kuliko dereva wa bodaboda.

Timu zote zina wachezaji waliozifikisha timu zao robo finali, Pale uwanjani wanacheza wachezaji (madereva) sio pesa (malori na bodaboda).
We kweli mtu pori. Ndiyo maana mnaambiwa muende shule. Ndiyo umeandika nini.
 
Huo mfano wako hausadifu hiki ninachokisema hapa. Simba, Yanga, Al-Ahly na mamelodi ni timu ambazo ziko robo finali ya CAF champions, hii inatosha kumfanya mchambuzi mwenye akili kuwa hizi timu uwanjani ziko na ulinganifu hata kama kwenye uwekezaji (pesa na majengo, miundombinu) zimezidiana sana. Kama ni swala la kuwekeza tu ziko timu ambazo zimewekeza sana kuliko simba na yanga lakini hazifika hatua hii ya robo finali, hivyo Kwa mchambuzi mwenye utimamu wa mwili na akili ingetosha kuondoa factor ya uwekezaji na kubakiza factors za upambanaji kiwanjani, teamwork, mbinu za mabenchi ya ufundi na mchango wa mashabiki uwanjani.

Huo mfano wako wa Man city na RB Leipzia ni mwendelezo wa ukosefu wa weredi kwenye uchambuzi kwakuwa Man city na RB haziko zote kwenye robo final ya EUFA champions kama zilivyo simba na al-ahly.

Ukiona mchezaji anacheza Afrika kiwango chake bado ni cha Afrika tu, wachezaji bora duniani wamenyakuliwa na timu za Ulaya, timu zetu za Afrika zina wachezaji wanaolinganalingana na kuzidiana tu viwango vya kujituma, motivation wanazopewa (pesa, mazingira na mabenchi ya ufundi).
Daah wewe jamaa Allende yupo sawa na nani kwa Viungo wa Afrika..ulichoongea sio sahihi Madrid hata hao Man City wamefanikiwa na kubeba kombe la Uefa kwa sababu ya Uwekezaji sio kujituma Timu zinazojituma kama Newcastle zipo nyingi...
 
wacha 16 bora, linganisha timu ambazo zimefika zote robo, nusu au finali halafu useme upuuzi kama huo. Hata Al-Ahly na Mamelodi wenyewe hawasemi upuuzi kama huo; maana Al-Ahly wasingehangaika kuja na mapipa kwenye ndege kama wangekuwa wanafuata wanachosema wachambuzi wetu wa mchongo.
Wewe una matatizo kichwani. Kwa hiyo Man city akikutana nusu fainal na Dortmund unafikiri kuna mchambuzi ataitabiria Dortmund kushinda mbele ya man city? Kwa hiyo yanga wakicheza na underdog kama akina Prison huwa wanajiachia tu kisa wanacheza na underdog? Hakuna kufarijiwa uwezo ni mdogo na wachezaji wenu wa kutoa mataulo golini.
 
Hakuna wachambuzi Tanzania
Huwezi kuona wanachuzi kama Ian Wright, Michael Owen, Carragha
Wanaonesha mapenzi ya team fulani
Nakumbana kuzishusha nyingine kwa kuzikatisha tamaa na uzushi

Kama wafanyavyo pale EFM
Wachambuzi wetu wanachambua mpira sawa na watu waliokaa kwenye vijiwe vya matawi ya Simba na Yanga au vile vijiwe vya bodaboda na kahawai. Wanashindwa kuchambua timu na wachezaji ambo wamefika robo finali kwenye kundi ambalo lilikuwa na mabingwa watupu kama al-ahly, CRB, na mediamawa, timu ambayo imefunga goli 5 timu ambayo inajiandaa kumfunga Al-ahly kwenye mechi ya robo final CAF champions, timu ambayo ilitoka sare na na kufungwa goli moja TU na Al-ahly, timu ambayo ilimfumga CRB goli 4.-0. mpira wetu umekuwa lakini wachambuzi wamedumaa.

Timu zetu Simba na Yanga zitafungwa kama sehemu ya matokeo 3 ya mpira na mbinu za nje ya uwanja lakini sio kwa sababu ya uwekezaji mdogo. Mfano, Yanga ilikosa kombe la caf confederation kutokana na mbinu chafu TU na kanuni za mashindano. Simba walikosa kwenda nusu finali kwa kufungwa bahati mbaya na jwaneng hapa nyumbani na kutoka kwa BAO la ugenini, sio timu mbovu Wala dhaifu. Wachambuzi wetu bhanaa!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom